Notification texts go here Contact Us Buy Now!

Sukari inavyokuwa sumu mwilini

watu tumekuwa tukitumia sukari kwenye vyakula vyetu. asubuhi kwenye chai, kwenye soda, matunda na vyakula vingine. Na jambo la kusikitisha sana ni kwamba watu sasa hivi wanatumia sukari kwa wingi sana kuliko miaka ya zamani. unakuta hadi watu wazima wanakula pipi ambapo kwa miaka ya zamani pipi zilkuwa kwa ajili ya watoto na pia walikuwa wakipigwa marufuku kula pipi kwa wingi kwasababu zilikuwa zinapelekea meno yao kuoza.
watu tumekuwa tukitumia sukari kwenye vyakula vyetu. asubuhi kwenye chai, kwenye soda, matunda na vyakula vingine. Na jambo la kusikitisha sana ni kwamba watu sasa hivi wanatumia sukari kwa wingi sana kuliko miaka ya zamani. unakuta hadi watu wazima wanakula pipi ambapo kwa miaka ya zamani pipi zilkuwa kwa ajili ya watoto na pia walikuwa wakipigwa marufuku kula pipi kwa wingi kwasababu zilikuwa zinapelekea meno yao kuoza.

Na mbaya zaidi ongezeko la matumzi ya sukari ambayo ni fructose or high-fructose corn syrup ambayo inatumiwa sana na viwanda vya kutengeneza vyakula na vinywaji, hii ni kwasababu sukari hiyo ni bei rahisi na pia ni 20% cheaper kulinganisha na sukari ya kawaida tunayotumia majumbani.



Habari mbaya ni kwambamwili wa binadamu hauna uweza wa kuprocess sukari yote hiyo sana sana fructose. Na pia mwili wako huprocess fructose tofauti nu unavyo process sukari ya kawaida ambapo fructose huwa processed directly na kuwa fats (mafuta) ambayo ni chanzo cha matatizo mengi ya afya.

Kwa wastani mwili wa binadamu unatakiwa kutumia vijiko sita (6) vya sukari. hii namaanisha kwamba sukari ilioko kwenye vinywaji vyako na vyakula vyako vyote ulivyo kula kwa siku ikikusanywa kwa pamoja ndio ifike hivyo vijiko sita. na sina maana kwamba vijiko sita vya ile sukari tunayoongeza kwenye chai japo kuwa na hyo itakuwa kwenye mjumuisho wa sukari utakayo tumia kwa siku nzima mfano sukari iliopo kweye ndizi, machungwa, ugali, juice na vyakula vingine unavyotumia.

Mazara ya matumizi ya sukari kupita kiasi

1. Inachasha na kuharibu ini (liver)
madhara ya sukari kwenye ini hayana tofauti na yale ya pombe. kwasababu sukari yote unayokula inasafirishwa mpaka kwenye ini na ndipo iweze kwena kutumika au kuhifadhiwa. kwahiyo unapokula sukari kwa wingi hasa frutose ini lako kuweza kuprocess sukari yote hupelekea ini kuchoka mapema.

2. Sukari huu fanya mwili wako kuongezeka uzito kwa kasi.
utumiaji wa sukari hasa fructose huufanya mwili wako kuzima appetite control system ndipo hupelekea kuongezeka hamu ya kula na kutokufanya kazi kwa kongongosho vizuri

3. Kuongeza uric acid kwenye mwili
ongezeko la uric acid na hatari kwa moyo na upo hatarini kupata magonjwa ya figo. jihadhari hasa kwa wale ambao wanatumia sukari ya fructose kwa wingi.

4. Husababsha blood pressure
Kama umeshawahi kuhishi na mtu ambaye anasumbuliwa na high blood pressure huwa wanaambiwa na daktari wapunguze matumiza ya sukari. hi ni kwasababu sukari hupelekea ongezeko la mafuta kwenye mishipa ya damu na moyo.

5. Kunenepa kupita kiasi na kuota kitambi.
kama nilivyosema hapo awali utumiaji wa sukari hasa fructose hubadilishwa na mwili kuwa mafuta (fats) ambapo haya mafuta huhifadhiwa kwenye mishipa ya damu na aneo la tumboni (abdomen). ambapo ongezeko hili la mafuta kwenye abdomen ndio kitambi chenyewe hicho. Kwa wale ndugu zangu wenye vitambi na wanapata shida kupunguza vitambi vyao njia ya kwanza ni kukata kabisa mazoea na sukari ukiambatanisha na njia rahisi za kupunguza uzito kitambi utakuwa unakiona kwa wengine wasilolijua hilo.

6. Kisukari
Nazani ipo wazi kuwa ulaji wa sukari kwa wingi ni miongoni mwa sababu za kisukari. hilo halipingiki na lipo wazi. watu wengi huwa hawatilii maanani ubaya wa kisukari na huwa wanadharau ushauri wanaopewa kuhusiana na ugonjwa huu na kuzani i ugonjwa unaowapata wazee au ni ugonjwa wa kurithi. hilo sio kweli unapokula sukari kupita kiasi inapelekea insuline resistance ambayo ni ile hali ya mwili kushindwa kucontrol sukari mwilini.

7. Kuongezeka kwa cell za cancer.
sukari in zilisha cell za canser na kuongeza speed ya ukuwaji wa cell hizo. Fructose hutumika na cell za cancer kuongeza proliferation. sijajua kwa kiswahili tuiiteje mnaofahamu mtanisaidi kwenye comment ili nijua proferation kwa kiswahili inaitwaje lakini kwa ufupi ni ile hali ya kuongezeka kwa kasi kwa cell za canser mfana zilikuwa mbili zinajizidisha zinakuwa ishirini tuseme zinajizidisha, vitu vingine ni bora tuviache kwa kingereza hivyo hivyo but hope nimeeleweka.

Magonjwa mengine ambayo husababishwa na utumiaji wa sukari kwa wigni ni kama demetia, hypertension, magonjwa ya moyo na Polycystic ovarian syndrome ambayo ni chanzo cha tatizo la ugumba kwa wanawake.

Sukari katika hali yake ya kwaida (natural form) sio mbaya ikitumika kwa kiwango kidogo. matatizo huanza unapozidisha matumizi ya sukari au unapotumia fructose ambayo ipo kwenye vyakula vyote ambayo ni processed. So kiufupi epuka vyakula ambayo ni processed kama juice ambazo ziko processed. kuliko ukanunue juice ya chungwa ilivyokuwa processed ni bora zaidi ukanunue chungwa ule.
Mtaji ambao utakuwa nao mpaka mwisho ni mwili wako. Tunza mwili wako kulko gari au nyumba yako kwasababu usipo kuwa na mwili wenye afya hivyo vyote utavifurahia kwa mda mrefu.


Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.