CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA KWANZA (01)
MTUNZI: Minnah De Embaccas
Whatsapp :0656282898
SEHEMU YA KWANZA (01)
Ilikuwa alfajiri moja nyepesi, katika jiji la dar-es-salaam, katika mtaa mmoja tulivu sana mbezi beach, dio kwanza nikama pilika zilikuwa zinaanza, yalionekana magari machache ya kifahari, yakikatiza kwenye viji barabara vya mtaa, na kupoteea barabara kuu, watu wakikwep foleni kwa kuwai makazini na mashuleni, au sehemu mbali mbali za kijamii, mapema namna hii, huku watu wachache walio tembea kwa miguu wakionekana wakitembea haraka kuelekea barabarani,
Ndani jumba moja la kifahari lililo zungukwa na uzio(fensi) wa ukuta mkubwa, ilisikika sauti ya msichana mmoja, mrembo mwenye asili ya Kihindi akiongea na mama yake, ilionekana alikuwa anataka kutoka. "mama mi naondoka naenda shule, maana kuna mitihani muhimu nawahi ingekuwa bila ya hiyo mitihani nisingeenda" alisikika binti mwenye sauti kinanda, akimwambia mama yake, ambae pia, ni mwenye asili ya Kihindi,japo alionekana ni mama wa makamo, lakini akika alifanana na binti yake., maana unge weza kuona uzuri wa mama huyu, japo tayari alisha kuwa mkubwa, "basi haya, chukua gari hiyo nyeusi, uwahi mwanangu" alisema mama huyu huku anawonyeshawanae funguo ya hili gari alilo mtajia, "hapana mamy, ntaomba lifti huko huko, leo sijisikii kuendesha" alijibu binti mrembo, huku akichukuwa begi lake juu ya meza na kuanza kuondoka, akiufwata mlango mkubwa wa kutokea nje. "haya basi baadaye mwanangu, jitazame huko uendako" aliongea mama huku anamsindikiza kwa macho binti yake, ambae toka akiwa mdogo amekuwa nae makini sana, ungesema amezaliwa peke yake, "ok mumy" alijibu binti chotara, huku anainua mkono wake na kuchezesha vidole, akimaanisha ana mpungia mkono mama yake, kisha akatoweka.
Naam huyu ni binti mrembo NIRAM, ni binti wakihindi, mwenye sura nzuri ya kuvutia, macho ya duara, pua iliyochongoka vizuri, mwenye midomo mipana ambayo kila anapo tabasamu, basi uacha vijishimo mashavuni mwake, alikuwa na urefu wa futi tano, na pointi kadhaa, kifua cha wastani na tumbo dogo, kiuno chake kilibeba makalio ma nene kihasi na pia, vi hips vya kumwagika vilivyojazia na kuchomoza pembeni, vilizidi kumpendezesha, asa anapokuwa katika mwendo, kiufupi mdau wa story hii, ilikuwa si rahisi upishane nae, ushindwe kumgeukia, iliuone uumbaji.
Huyu anaitwa Niram Popat, baba yake ni mfanya biashara mkubwa, na kwa sasa yupo nchini Uingereza, kwa shughuli zake za kibiashara, binti huyu akualiwa peke yake, Niram alikuwa na kaka yake, ambae kwa sasa yupo chuo kikuu cha Indira Gandhi nchini india akijichukulia masters yake, kifupi katika familia yao wamezaliwa wawili tu! yani yeye na kaka yake, Niram alipendwa kuliko kawaida.
Hiyo ndo historia fupi ya niram, ebu tuendelee na kisa hiki cha Chaguo langu, Niram alitembea taratibu akiongozana na watu waliokuwa wanaelekea huko kwenye kituo cha dala dala, dakika chache baadae, Niram alifika kituoni, nakuwakuta watu wengi wakisubiri usafiri,binti huyu, alijitenga pembeni kabisa na abiria wengine, usafiri ilionyesha ulikuwa wa shida sana siku hiyo, maana magari yalifika pale yakiwa yamesha jaa, hivyo waliofanikiwa kupanda, walijibana kama nyanya kwenye matenga, Niram alijikuta ana kumbuka gari ambalo amelikataa nyumbani,”haaa, kwanini niliamua hivi?” alijilahumu binti huyu mzuri, ambae asilimia tisini ya wanaume waliokuwepo pale, walikuwa wanamkodolea macho, wakisanifu uumbaji,
Lakini wakati anawaza hayo,mara ghafla ilisimama range nyeusi, mbele yake na paka shushwa vioo, ilionekana sura moja matata sana, ya mwanaume mtanashati, hakika alifaa kuitwa handsome wa Kiafrika "hellow" yule kijana ndani yagari alimsabahi Niram, nae akajibu kwa kichwa, yule jamaa akatabasamu kidogo, "naweza kukupa lifti? Aliuliza kijana yule. na Niram akuwa mbishi, aliitikia kwa kichwa kama kawaida yake, hapo ukafunguliwa mlango Niram akaingia. na kufunga mlango, sasa akawa ametulia kwenyeseat yake, huku macho mbele, akitegemea kuona gari linaondoka, na maswali yanaanza, lakini zika pita dakika kadhaa na gari halikuondoka.
Muda wote haku endesha gari, alikuwa ameduwaa, kumshangaa msichana alie ingia garini mwake. Alizidi kushangaa "sorry kaka mimi nashuka vituo vinne mbele ndipo ilipo shule yetu"aliongea niram. Maskini kijana yule aligutuka, akababaika huku anaondoa gari, "oooh! aaagh sawa unasoma shule ipi dada?" aliongea huku gari ikienda taratibu "shadhiliya slamic internation school" alijibu Niram, "ooh ile shule ya kiislam "aliuliza kijana. "yap! nasoma kidato cha tano pale" alijibu niram "ok mi mwenyewe nasoma pale st joseph international school kidato cha sita "alisema kijana "aah kumbe" alisema Niram kwa uchangamfu kidogo, akiona kuwa yupo na mwanafunzi mwenzie, "ndiyo ninaitwa Vincent, sijui naweza kulijuwa juna lako kama hutojali?" aliuliza Vincent huku anatabasamu, kidogo wengee lilianza kumtoka, "mimi naitwa Niram..” alisema Niram lakini kama alistuka kidogo, “ooh! kaka nishushe unapitiliza" aliongea niram kwa mshtuko "ooh sorry, kwa kweli" alijibu Vincent,huku ana peleka mguu wake wkulia katikati na kukanyaga bleack, akippunguza mwendo na kuweka gari pembeni ya barabara, kisha akasimama,
Niram alishuka, na akashukuru Vincent kwa kupitia kwenye dirisha la upande aliokaa, na kuondoka zake. Vicent alibaki kaduwaa, maana alishangazwa na uzuri wa aina yake, kwa yule msichana. "daah nimesahau kuomba namba" alijilahumu Vicent, lakini hakuwa na lakufanya, akawasha gari akasepaaa.
Anaitwa Vicent Ngosha, ni mtoto wa mzee Emanueli Ngosha mfanya biashara mkubwa nchini Tanzania na nje ya nchi.Vincent alikuwa ni mvulana wa kisukuma, mama yake ni muhaya, Vicent ni mtoto pekee kwenye familia yao, ni familia yenye uwezo mkubwa, baba yake alikuwa mkoani kibiashara, hivyo alibaki pale nyumbani na mama yake, pamoja na house girl, Vicent alifika shuleni akiwa na mawazo lukuki, “ok! mdau huu nimwanzo wa mkasa huu wakusisimua, ......
MTUNZI: Minnah De Embaccas
Whatsapp :0656282898
SEHEMU YA KWANZA (01)
Ilikuwa alfajiri moja nyepesi, katika jiji la dar-es-salaam, katika mtaa mmoja tulivu sana mbezi beach, dio kwanza nikama pilika zilikuwa zinaanza, yalionekana magari machache ya kifahari, yakikatiza kwenye viji barabara vya mtaa, na kupoteea barabara kuu, watu wakikwep foleni kwa kuwai makazini na mashuleni, au sehemu mbali mbali za kijamii, mapema namna hii, huku watu wachache walio tembea kwa miguu wakionekana wakitembea haraka kuelekea barabarani,
Ndani jumba moja la kifahari lililo zungukwa na uzio(fensi) wa ukuta mkubwa, ilisikika sauti ya msichana mmoja, mrembo mwenye asili ya Kihindi akiongea na mama yake, ilionekana alikuwa anataka kutoka. "mama mi naondoka naenda shule, maana kuna mitihani muhimu nawahi ingekuwa bila ya hiyo mitihani nisingeenda" alisikika binti mwenye sauti kinanda, akimwambia mama yake, ambae pia, ni mwenye asili ya Kihindi,japo alionekana ni mama wa makamo, lakini akika alifanana na binti yake., maana unge weza kuona uzuri wa mama huyu, japo tayari alisha kuwa mkubwa, "basi haya, chukua gari hiyo nyeusi, uwahi mwanangu" alisema mama huyu huku anawonyeshawanae funguo ya hili gari alilo mtajia, "hapana mamy, ntaomba lifti huko huko, leo sijisikii kuendesha" alijibu binti mrembo, huku akichukuwa begi lake juu ya meza na kuanza kuondoka, akiufwata mlango mkubwa wa kutokea nje. "haya basi baadaye mwanangu, jitazame huko uendako" aliongea mama huku anamsindikiza kwa macho binti yake, ambae toka akiwa mdogo amekuwa nae makini sana, ungesema amezaliwa peke yake, "ok mumy" alijibu binti chotara, huku anainua mkono wake na kuchezesha vidole, akimaanisha ana mpungia mkono mama yake, kisha akatoweka.
Naam huyu ni binti mrembo NIRAM, ni binti wakihindi, mwenye sura nzuri ya kuvutia, macho ya duara, pua iliyochongoka vizuri, mwenye midomo mipana ambayo kila anapo tabasamu, basi uacha vijishimo mashavuni mwake, alikuwa na urefu wa futi tano, na pointi kadhaa, kifua cha wastani na tumbo dogo, kiuno chake kilibeba makalio ma nene kihasi na pia, vi hips vya kumwagika vilivyojazia na kuchomoza pembeni, vilizidi kumpendezesha, asa anapokuwa katika mwendo, kiufupi mdau wa story hii, ilikuwa si rahisi upishane nae, ushindwe kumgeukia, iliuone uumbaji.
Huyu anaitwa Niram Popat, baba yake ni mfanya biashara mkubwa, na kwa sasa yupo nchini Uingereza, kwa shughuli zake za kibiashara, binti huyu akualiwa peke yake, Niram alikuwa na kaka yake, ambae kwa sasa yupo chuo kikuu cha Indira Gandhi nchini india akijichukulia masters yake, kifupi katika familia yao wamezaliwa wawili tu! yani yeye na kaka yake, Niram alipendwa kuliko kawaida.
Hiyo ndo historia fupi ya niram, ebu tuendelee na kisa hiki cha Chaguo langu, Niram alitembea taratibu akiongozana na watu waliokuwa wanaelekea huko kwenye kituo cha dala dala, dakika chache baadae, Niram alifika kituoni, nakuwakuta watu wengi wakisubiri usafiri,binti huyu, alijitenga pembeni kabisa na abiria wengine, usafiri ilionyesha ulikuwa wa shida sana siku hiyo, maana magari yalifika pale yakiwa yamesha jaa, hivyo waliofanikiwa kupanda, walijibana kama nyanya kwenye matenga, Niram alijikuta ana kumbuka gari ambalo amelikataa nyumbani,”haaa, kwanini niliamua hivi?” alijilahumu binti huyu mzuri, ambae asilimia tisini ya wanaume waliokuwepo pale, walikuwa wanamkodolea macho, wakisanifu uumbaji,
Lakini wakati anawaza hayo,mara ghafla ilisimama range nyeusi, mbele yake na paka shushwa vioo, ilionekana sura moja matata sana, ya mwanaume mtanashati, hakika alifaa kuitwa handsome wa Kiafrika "hellow" yule kijana ndani yagari alimsabahi Niram, nae akajibu kwa kichwa, yule jamaa akatabasamu kidogo, "naweza kukupa lifti? Aliuliza kijana yule. na Niram akuwa mbishi, aliitikia kwa kichwa kama kawaida yake, hapo ukafunguliwa mlango Niram akaingia. na kufunga mlango, sasa akawa ametulia kwenyeseat yake, huku macho mbele, akitegemea kuona gari linaondoka, na maswali yanaanza, lakini zika pita dakika kadhaa na gari halikuondoka.
Muda wote haku endesha gari, alikuwa ameduwaa, kumshangaa msichana alie ingia garini mwake. Alizidi kushangaa "sorry kaka mimi nashuka vituo vinne mbele ndipo ilipo shule yetu"aliongea niram. Maskini kijana yule aligutuka, akababaika huku anaondoa gari, "oooh! aaagh sawa unasoma shule ipi dada?" aliongea huku gari ikienda taratibu "shadhiliya slamic internation school" alijibu Niram, "ooh ile shule ya kiislam "aliuliza kijana. "yap! nasoma kidato cha tano pale" alijibu niram "ok mi mwenyewe nasoma pale st joseph international school kidato cha sita "alisema kijana "aah kumbe" alisema Niram kwa uchangamfu kidogo, akiona kuwa yupo na mwanafunzi mwenzie, "ndiyo ninaitwa Vincent, sijui naweza kulijuwa juna lako kama hutojali?" aliuliza Vincent huku anatabasamu, kidogo wengee lilianza kumtoka, "mimi naitwa Niram..” alisema Niram lakini kama alistuka kidogo, “ooh! kaka nishushe unapitiliza" aliongea niram kwa mshtuko "ooh sorry, kwa kweli" alijibu Vincent,huku ana peleka mguu wake wkulia katikati na kukanyaga bleack, akippunguza mwendo na kuweka gari pembeni ya barabara, kisha akasimama,
Niram alishuka, na akashukuru Vincent kwa kupitia kwenye dirisha la upande aliokaa, na kuondoka zake. Vicent alibaki kaduwaa, maana alishangazwa na uzuri wa aina yake, kwa yule msichana. "daah nimesahau kuomba namba" alijilahumu Vicent, lakini hakuwa na lakufanya, akawasha gari akasepaaa.
Anaitwa Vicent Ngosha, ni mtoto wa mzee Emanueli Ngosha mfanya biashara mkubwa nchini Tanzania na nje ya nchi.Vincent alikuwa ni mvulana wa kisukuma, mama yake ni muhaya, Vicent ni mtoto pekee kwenye familia yao, ni familia yenye uwezo mkubwa, baba yake alikuwa mkoani kibiashara, hivyo alibaki pale nyumbani na mama yake, pamoja na house girl, Vicent alifika shuleni akiwa na mawazo lukuki, “ok! mdau huu nimwanzo wa mkasa huu wakusisimua, ......