Notification texts go here Contact Us Buy Now!

NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU SEHEMU YA 17 - 32


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU- 17

“ Hans? Hans yupi huyo?” Niimuuliza

Kabla hajanijibu, kengele nyekundu ililia kichwani mwangu. Nilijikuta nimeachama mdomo .

“ Dada utaongea na mgonjwa muda mwingine. Naomba tupishe tumuhudumie.” Nesi aliniambia

Nilipiga hatua kuondoka eneo lile bila kujua naelekea wapi. Njia nzima nilimtaja Hans.

“ Inamaaana Hans hakufa? Mmmh hapana, alijinyonga,kwa macho yangu nilishuhudia akiwa kaninginia darini. Na sio mimi tu, ndugu zangu na ndugu zake wote walishuhudia. Hans amekufa, mtu aliyekufa hawezi kuja kumpiga mtu .” Nilijiambia.

“Ndiiiii…” Niligongana na mtu uso kwa uso.

“ Dada kuwa makini, tutavunjana bure.” Aliongea yule kaka.

Sikumjibu, nilimpisha na kuendelea kutembea bila kuongea lolote. Kichwa changu kilivurugwa sana. Maneno ya James kupigwa na Hans yalinichanganya.

“ Hapana, haiwezekani akawa Hans.Huu mchezo utakuwa umefanywa na wazazi wake ili kunivuruga akili. Hans amekufa.” Nilijiambia.

Nilichukua simu na kumpigia Baba. Nilimueleza tukio nzima, pia nilimweleza jinsi ninavyohisi. Nilimwambia wazazi wa Hans wanataka kunichezea akili.Nilimuomba akawaonye na kuwataka wakae mbali na mimi.

………………………………….

Baba badala ya kwenda nyumbani kwa wazazi wa Hans, moja kwa moja alienda polisi. Aliwashtaki wazazi wa Hans kwa kosa la kumshambulia James na kutaka kunichezea akili.

“ Kwanini umeenda kuwashtaki? Si ungeenda kuwaambia kistaarabu ?” Mama alimuuliza baba.

“ Hapana, wanazidi kunizoea. Acha niwaoneshe.” Aliongea baba.

…………………..

Siku ya pili yake, nikiwa jikoni naandaa chai ya kupeleka hospital, nilisikia mlango wa mbele ukigongwa kishari sana.

“Hodi gani wanapiga hivi? “ Niliwaza. Niliwahi kwenda kufungua. Ile nafungua tu ,macho yangu yalikutana na macho ya polisi.

“ Baba yako yupo?” Aliniuliza.

“ Mnashida gani?”

Walinitolea arrest warrant, waliniambia wamekuja kumkamata baba kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi James.

“ Mtakuwa mmechanganyikiwa, baba anaanzaje kumpiga James? Yeye ndiye aliyefungua kesi ya kupigwa James, inakuwaje tena leo mnasema yeye ndio muhusika?” Niliwauliza.

Hawakunijibu, walinisukuma pembeni na kuingia ndani.

Ile kuingia tu, walikuatana na baba akiwa anatoka chumbani.Pale pale walimkamata. Alijaribu kujitetea ilikuwa sifuri, polisi hawakumuelewa. Walimbeba msobe msobe mpaka nje, walimtupia kwenye gari, na kwenda naye kituoni.

Hatukukubali aenda peke yake. Mimi na mama tuliwafata kwa nyuma.

……………………………

Baada ya kuchukuliwa maelezo na kuwekwa mahabusu, tuliomba tumwekee dhamana. Tuliongea na Mkuu wa kituo ,alitukatalia, alituambia kama tunampenda Baba na tunataka atoke basi tukazungumze na baba Hans.

“ Baba Hans ndio nani kwanza mpaka tukazungumze naye? Mtu mliyesema amempiga amekataa, amesema sio yeye” Niliongea.

“ Naomba tupunguze kuongea, nina kazi nyingi sana hapa za taifa. Narudia tena, kama mnampenda baba yenu nendeni mkazungumze na baba Hans.Bila hivyo hii kesi itakuwa kubwa kwenu. Ushahidi tulioupata ni mkubwa sana, unathibitisha bila shaka baba yenu ndiye aliyemjeruhi James.” Aliongea Mkuu wa kituo.

Hatukuwa na namna, tuliondoka na kwenda kuongea na baba Hans.
……………………………….

“ Nilijua mtafika, sasa ipo hivi, uamuzi ni wenu , kusuka au kunyoa. Mchagueni baba yenu au James. Mkitaka nimfutie kesi yake swala la ndoa na James life.” Aliongea.

“ Hilo haliwezekani, haliwezekani kabisa.” Aliongea Mama.

“ Kama haiwezekani basi, naomba muondoke.” Aliongea baba Hans. Tulijaribu kumbembeleza hakutuelewa.

Tuliondoka tukiwa hatujui tufanye nini.

“ Haina shida Mama, James akipona ataenda polisi kumtoa baba.’ Nilimwambia mama.

“ MUNGU mkubwa, atatusaidia tu.” Aliongea Mama.

Gafla, Mbele yetu alitokea Mama Hans.

“ Anayoyafanya mume wangu siyaelewi wala siyapendi kabisa. Kujuana na Mkuu wa Kituo imekuwa shida. “ Aliongea Mama Hans.

“ Lakini sio lazima awasaidie yeye, kuna mtu mwingine anaweza kuwasiadia. Kama hamtajali naomba niwapeleke kwake. Mkiongea naye vizuri atawasaidia tu.” Aliongea mama Hans.

Tuliangalia na mama.

Mama alimwambia atupeleke kwa huyo mtu.

Tuliongozana kuelekea kwa huyo mtu . Tulimkuta.

“ Eeeeeh!..Ndo…..hu…yu..?” Niliuliza.


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU -18

 
“ Ndio, ni yeye.” Alinijibu Mama Hans.

Alikuwa ni yule mbaba aliyetaka kunibaka(Martini).

“ Nayajua matatizo yenu. Najua alichowafanyia Baba Hans. Nawaomba niwasaidie.” Aliongea.

“ Emma mbona unamuangalia hivyo? Huyu mtu ni muhimu sana kwako, atakusaidia kwenye hili na kwenye matatizo yako mengine.” Aliniambia.

“ mmmmh! mbakaji huyu atanisaidia nini mimi?”  

“ Usiniite hivyo tafadhali, naitwa Martini. Najua mara nyingi tumekutana katika mazingira tata. Lakini pamoja na hilo hauna haki ya kuniita mbakaji.” Aliongea.

“ Eti hatuna haki?” Niliongea kwa dharau.

Pamoja na kumjua, nilipomuangalia vizuri nilikumbuka kitu kingine kumuhusu, Pamoja na kuwa ni yeye aliyetaka kunitoa usichana wangu ile siku, alikuwa pia ni yule mtu aliyekuja na mama mkwe akiwa kavaa baibui wakati nimewekwa ndani nyumbani kwa wakwe zangu.

“ Macho yako nimeyakumbuka sasa, bila shaka wewe ndiye yule uliyefika na mama mkwe kuniona kipindi kile nimewekwa ndani baada ya msiba, na ulipomuona baba mkwe amefika ulikurupuka. Ulimsukuma na kukimbia.” Nilimwambia.

Martini na Mama Mkwe waliangaliana.  

“ Ni kweli, ni mimi. Ila yale yalishapita. Naomba tuongee mambo ya msingi yaliyowaleta hapa. Naombeni mniruhusu niwasaidie” Alituambia.  

“ Mbona hammjibu!” Alituuliza Mama Hans.

“ Ruhusa yetu anayo, sisi hatuna shida, kama anaweza kutusaidia atusaidie tu.” Aliongea Mama.

“ Sawa, leo jioni mumeo atatoka.” 

“Sidhani kama anatusaidia bure. Naomba useme kitu unachotaka ili na sisi tujue kama inawezekana au lah.” Niliongea. 

“ Kuhusu ninachotaka nitaongea na Mama yako. Ila naomba uondoe wasiwasi, hakuna chochote kibaya. “ Aliongea Martini. 

Baada ya mazungumzo mawili matatu. Walinitaka niondoke. Niliondoka na kuwaacha wakizungumza na Mama. Nilienda moja kwa moja hospital, nilimkuta James hali yake ikiwa inatengemaa, alikuwa anaendelea vizuri, tofauti na mwanzo.

“ Wameniambia wananiruhusu leo . Nikitoka hapa moja kwa moja nitaenda polisi kushughulikia swala la baba yako. Haiwezekani wakamfunga bila sababu ya msingi.” Aliniambia.

“ Kuhusu hilo achana nalo. Tatizo la baba tumeshalishughulikia. Na kuhusu aliyekupiga sio Hans, Hans alishakufa na kuzikwa. Nazani baba mkwe kuna mtu alimkodi akupige na kumwambia ajitambulishe kama ni Hans.”  

“ Kama baba yako atatoka leo nitawaomba wazazi wangu na wako wakae pamoja ili tuweze kufunga ndoa haraka. Naona kama kuna wingu jeusi linataka kuzuia ndoa yetu.”   

“Ni kweli, hata mimi naona hivyo.” Nilimjibu.

…………………………

Martini, Kama alivyoahidi , jioni baba alitolewa . Kesi yake ilifutwa, sijui Martini alifanya nini mpaka Baba Hans akafuta kesi .  

“ Inawezekana vipi Baba Hans akafuta kesi kirahisi hivi? . Martini na Baba Hans watakuwa wanashirikiana, Lakini inawezekana vipi? Kama wanashirikiana kwanini siku ile alikimbia? Pia kwanini alivaa baibui ili asionekane?” Niliwaza.

Maswali haya niliamua kumshirikisha Mama. 

“ Mama haya mambo unayaonaje? Aliyemfunga baba ni Baba Hans, lakini Martini ndiye aliyemtoa. Na kwa jinsi ninavyokumbuka Baba Hans na Martini hawaelewani? Ni kipi Martini alichofanya kumshawaishi Baba Hans afute kesi? “ Nilimuuliza Mama.

“ Maneno niliyoyasikia mtaani ,Martini ni hawara wa Mama Hans. Hivyo yeye na Baba Hans ni paka na panya, sasa sijajua ni kipi kinaendelea mpaka ikawa hivi.”Aliongea Mama.

“ Mmmmmh! Na wewe Martini alikuambia nini? Mlifikia makubaliano gani mpaka akakubali kumtoa baba?” Nilimuuliza Mama.

“ Achana na hayo, hakuna lolote la maana tuliloongea.” Alinijibu. 

Pale pale alisimama na kuondoka.

…………………………..

Siku zilikatika, harakati za ndoa yangu na James zilianza, kuhusu Send off tuliamua kuachana nayo. Tuliamua tufanye sherehe kubwa moja ya Ndoa.

Vikao vya harusi vilianza kwa kasi. Kwenye vikao Jamaes alikataa kuwachangisha watu michango ya harusi na send off, alitaka watu wapewe kadi na kuja kwenye sherehe. Kila kitu aligharamia mwenyewe.

Wakati harakati zikiendelea, gafla, moyo wangu ulibadika , mapenzi niliyokuwa nayo kwa James yaliyeyuka, nilijikuta nikianza kumchukia, bila sababu nilimchukia.  

Nilijikaza na kujilazimisha kumpenda.

“ James ni sahihi kwangu. Yeye ndiye atakayenioa.” Nilijimbia.

Ajabu, kadri nilivyojilazimisha kumpenda, ndivyo moyo wangu ulivyozidi kumkataaa. 

“ Nina nini mimi? Kwanini namchukia huyu mtu gafla hivi?” Nilijiuliza moyoni.

……………….

Usiku mmoja kabla ya harusi, nikiwa chumbani kwangu, nilikuwa nawaza kuhusu hali yangu.

“ Hivi ni kweli simpendi James? Au kuna kitu nimefanyiwa?” Nilijiuliza.

“ Na kama kweli simpendi inakuwaje nakubali kufunga naye ndoa. Kwanini nakubali kufunga ndoa na mwanaume ninayemchukia kiasi hiki?” Nilijiuliza. Nikiwa nawaza hayo, mlango wa chumba changu ulisukumwa. Aliingia Mama.Alikaa kitandani na kunishika bega.

“ Mwanangu kesho ndio siku ya harusi yako. Ukishafunga ndoa na James hakuna kurudi nyuma tena, yeye atakuwa mwanaume wa maisha yako. Nakushauri, kabla ya kufunga ndoa tumia usiku wa leo kujiuliza vizuri. Jiulize kama ni kweli unampenda James au lah? “ Aliniambia. 

“ Nakuacha ufikirie hilo, ila kwa upande wangu, kama mimi ningekuwa wewe, wala nisingekubali kufunga ndoa na James, kamwe nisingekubali kuolewa na mwanaume nisiyempenda.” Aliongea Mama. Maneno yake yaliniacha kinywa wazi. Nilimtazama Mama nisijue niseme nini.

“ Amejuaje kama simpendi? Amejuaje? Hakuna mtu yeyote niliyemwambia, hii imekuwa siri ya moyo wangu peke yangu. Yeye amejuaje kama simpendi? Amejuaje kama namchukia james?” Nilijiuliza maswali mfululizo.  

Haraka ubongo wangu ulikumbuka maneno ya baba aliyosema Mama ameharibu maisha yake na pia anataka kuharibu yangu, nilimuangalia kwa jicho kali kisha nikamuuliza swali.

“ Umejuaje kama simpendi? Umejuaje?” Nilimuuliza. Nilikazia macho.

“aaa…..aaaaa…..aaaa…..” Alishikwa na kigugumizi.  


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU -19

“ Aaaaa….aaaaa…..aaaa..” Mama alishikwa na kigugumizi.

“ Naomba niambie mama. Nini kinaendelea? Umejuaje kitu ambacho sijawahi kumuambia mtu yeyote?”  

“ lakini….”

“ Hakuna cha lakini Mama, naomba niambie! Umejuaje kuwa simpendi James. Umejuaje? Au wewe ndio chanzo. Kuna kitu umefanya nisimpende James. Niambie mama! Naomba niambie ukweli, maana sielewi, inakuwaje gafla tu naanza kumchukia James. Lazima kuna kitu kimefanyika, na mtu aliyefanya ni wewe, hakuna mwingine zaidi yako.”  

‘ Lakini kwanini unanifikira hivyo mwanangu? Kitu gani mimi nifanye ili usimpende James? .Kumbuka mimi ni Mama yako, najua kila kitu kuhusu wewe, nikikuangalia najua kama una furaha au hauna. Kwa siku kadhaa nimekuangalia na kugundua hauna furaha, na nimegundua chanzo ni James. Nimegundua haumpendi.” Aliniambia.

“ Lakini umejuaje?” .

“ Unakumbuka wakati wa kikao nilikufata na kukuuliza kama upo sawa? Unajua kwanini nilikufata? Kwa taarifa yako nilikufata baada ya kuona unamuangalia James kwa chuki. Sijui nini kimetokea, lakini kwa jinsi ninavyokuona nimegundua haumpendi James. Na kama mawazo yangu ni sahihi, naomba usikubali kufunga ndoa na mwanaume usiyempenda.” Aliniambia..

“ Kumbe hadi naonekana! Hadi watu wa pembeni wameanza kuona hisia zangu.” Nilijiambia. 

Mashaka yangu kwa Mama yalipotea. Maneno yake yalinifanya nimuamini. 

“ Kwahiyo nikikataa itakuwaje? James hawezi kunichukia?”.

“ Hata akikuchukia sio shida, la msingi ni Amani ya moyo wako. Kuolewa na mwanaume usiyempenda ni shida sana. Maisha yako yote yatakuwa ya tabu sana. Ni vyema ukakataa tu. Tena ukiniambia saizi,nitaenda kumwambia baba yako, na kwa pamoja tutajua tukusaidie vipi.”  

Nilimwambia anipe muda nifikirie. Aliondoka na kuniacha ndani. Niliwaza na kuwazua. Akili yangu ilinitaka niendelee na ndoa lakini moyo wangu ulikataa kata kata. Nilikuwa njia panda. Baada ya kuwaza sana, niliamua kuendelea na ndoa. Nilimwita mama na kumweleza.

Mama alinisisitiza nisiendelee na ndoa. Aliniambia sio busara kufunga ndoa na mtu nisiyempenda. Nilimwambia nitajilazimisha kumpenda, nilimwambia nitamuaomba MUNGU aniwezeshe kumpenda.

Mama hakukubaliana na uamuzi wangu. Alienda kumwambia baba . Baba alinifata na kuniuliza kama ni kweli simpendi James. 

“ Sielewi nini kinaendela kwenye mwili wangu! James mwanzo nilikuwa nampenda sana. Lakini gafla nimeanza kumchukia .Sijui kama nimerogwa au lah.” Nilimwambia baba.

“ Yaani ulikuwa unampenda halafu gafla tu umeanza kumchukia? Hiyo sio dalili njema. Kuna kitu katikati, ili kukomesha icho kitu, ndoa itafungwa kama kawaida.”  

“ Hapana Baba Emma, usifanye hivyo! Ni hatari sana. Sio kitu kizuri Mtoto kufunga ndoa na mwanaume asiyempenda.” Aliongea Mama.  

Mama alitushawishi sana. Alinisisitiza tuachane na habari ya ndoa.

Kadri alivyokuwa anaongea nafsi yangu ilianza kuingia mashaka naye.

“ Mama ndiye aliyemleta James kwangu, yeye ndiye aliyeniambia ni mtu mzuri. Yeye ndiye aliyetukutanisha na kunitaka niolewe naye. Inakuwaje saizi anataka nisiolewe naye? Kitu gani kimebadilika? Ndo kusema kisa simpendi au?” Nilijiuliza. 

Sikupata majibu. Pamoja na kukosa majibu, niliamua kuendelea na ndoa. Nilimwabia Baba msimamo wangu. Nitafunga ndoa na James hata kama moyo wangu haumpendi. Nilimwambia nina imani baada ya muda chuki niliyokuwa nayo kwa james inaweza kuondoka.

Msimamo wangu ulimfanya Mama akose amani. Alikuwa mnyonge . Baada ya kuzungumza sana, majira ya saa tisa usiku, baba na mama waliondoka chumbani kwangu na kuniacha peke yangu. 

Nilikaa kitandani na kuwaza mawili matatu kuhusu maisha yangu na James yatakavyokuwa. Nikiwa nawaza hayo, Usingizi ulinisumbua, nilijiegesha kitandani.

Nusu saa mbele, mlango wa chumba changu uligongwa. Nilisimama na kwenda kufungua. 

Alikuwa baba.

“ Mama yako yupo wapi?” Aliniuliza.

“ Mama si uliondoaka naye?”  

“ Alirudi tena huku, aliniambia amekuja kuongea na wewe tena.” 

“ mmmh hapana! Huku kwangu hajafika .” Nilimjibu. 

Tulimtafuta kwa simu hatukumpata. Namba yake haikupatikana.Usiku ule ule tulienda kwa mashoga zake kumtafuta, ilikuwa bure, hatukufanikiwa kumpata.Hadi kunakucha Mama hakupatikana. Alikuwa amepotea kama upepo.

“ Tunafanyaje ! Asubuhi ikifika yakupasa uende kanisani kufunga Ndoa?” Aliniuliza baba.

“ Hata sielewi! Au niachane nah ii habari ya ndoa?”

“ Hapana, usifanye hivyo. Ukifanya hivyo itakuwa unampa mama yako anachotaka.Mama yako si mtu mzuri kama unavyofikiria.Bila shaka anataka kukuchezea, anataka kuharibu maisha yako.”

“ Kwanini kila siku unaongea hiyo kauli! Kwanini unaamini mama anataka kuniharibia maisha yangu?” 

“ Siamini, ila ni kweli.” Aliongea Baba. Alinishika mkono na kunipeleka chumbani kwake. Aliinama uvunguni na kutoa mabegi maatatu ya nguo, alizunguka nyuma ya kitanda na kuyatoa mengine tena. Aliyachukua yote na kuyatupa mbele yangu. Alichukua bahasha zenye dawa na kuzimwaga mbele yangu.

“ onaaaa…onaaaaaaaa…ushenzi wa Mama yako.” 

“ Sikuelewi, haya mabegi yanauhusiano gani na kuniharibia maisha?” Nilimuuliza.

“ Mwa..na..ngu….ma..ma…..ya…..k….o………a……..aaa…….” Alishindwa kumalizia.

“ uuuuuuuuuuuuuu……uuuuu……….” Alihema kwa nguvu. Alinishika mkono na kunitazama machoni.

“ Naomba nisikilize mwanangu! Sitaki kukueleza mambo ya mama yako, ila naomba niamini, endelea na ndoa yako. Na hii ni kwa faida yako.”

“ Sawa baba, nimekuelewa. Wewe unamjua Mama kuliko mimi. Nitaendelea na Ndoa kama kawaida, nitafunga ndoa na James, na nitaenda ukumbini kusherekea.” Nilimwambia baba.

Kabla baba hajanijibu, simu yake iliita. “ ngrriiiiiiiiii…nriiiiiiiiiii..ngriiiii……”Iliita. Aliipokea na kuiweka sikioni.

“ eeeeeeeh!”. 

 


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU- 20

“ kuna nini baba?” Nilimuuliza.

“ aaa…aaaa….ha..ku..na…….hakuna……”   

“ Hakuna nini? umepewa taarifa mbaya?”

“ Usijali mwanangu! Hakuna lolote baya. Endelea na maandalizi ya harusi yako.Hakuna baya litakalotokea.” Aliniambia na kuondoka.   

Niliamua kuendelea na maandalizi. Nilijipa moyo, nilijiambia kwakuwa baba alinitaka niendele na mandalizi ,haina haja ya kuendelea kujiumiza kichwa. Niliendelea na maandalizi.

Majira ya saa moja asubuhi , walifika wapambe wangu, walinichukua na kunipeleka saloon. Nilipambwa na kuandaliwa vizuri. Nilirudishwa nyumbani. Niliwekwa chumbani kwangu kusubiri muda wa kwenda kanisani ufike. 

Kutokuwepo kwa mama kulizua minongono. Watu walinongonezana na kuteta.

Sikujali wala sikuwatilia maanani. Muda wa kwenda kanisani ulipofika msimamizi wangu alifika kunichukua. Kwa pamoja tuliongozana mpaka kanisani. Tuliingia ndani, Nilimkuta James na ndugu zake wakiwa tayari wameshafika.

Misa ya ndoa yetu ilianza. Tukiwa kati kati ya misa, James aliniuliza swali.

“ Uliniambia mama ameondoka kiutata na wala hamjui aliko, lakini mbona na baba naye simuoni.Tangu nimefika nimekuwa nikiangaza macho kushoto na kulia kumtafuta lakini simuoni kabisa.” Aliniambia James.

Kauli yake ilinifanya niangaze kushoto na kulia. Nilitazama kila kona ya kanisa, sikumuona baba. Kwa ishara nilimuita shangazi hidaya. 

“ Baba yuko wapi? Mbona simuoni hapa?” Nilimuuliza.

“ Hata mimi sijamuona. Tangu asubuhi nimekuwa namtafuta lakini simuoni.” 

“ Umejaribu kumpigia?” Nilimuuliza.

“ Ndio, lakini simu yake haipatikani.” Aliniambia.

“ Naomba mtafute, ni muhimu yeye kuwepo .” Nilimwambia shangazi. Shangazi aliondoka na kuniacha. Akili yangu iliniambia kivyovyote vile ile simu aliyopigiwa baba ndiyo iliyomfanya asionekane.

“ Aliambiwa nini? Kitu gani kimemfanya asihudhurie ndoa yangu.” Nilijiuliza. Furaha ndogo ya kujilazimisha niliyokuwa nayo , nayo iliyeyeku kama barafu. Mwili wangu ulikuwa kanisani lakini akili yangu haikuwepo pale.  

…………….

Shangazi naye tangu alivyondoka hakurudi hadi misa ya ndoa ilipoisha. 

Tukiwa tunatoka kanisani na kuelekea kwenye gari , Mwenyekiti wa kamati ya sherehe aliniita pembeni.

“ Kuna nini kinaendelea? Baba yako na mama yako wapo wapi?” Alinuliza.

Badala ya kumjibu swali lake, nilijikuta natoa machozi.

“ aaa..aaaaa…usilie sasa…usilieee…” Alinituliza mwenyekiti. Akiwa ananituliza alitokea shangazi. Alisogea hadi tulipo.

“ Nimemtafuta kila mahali nimemkosa!” Alituambia.

“ mmmh! Kwa hali hii sherehe itabidi tuisimamishe. La msingi ni ndoa, habari za ukumbuni na manjonjo mengine itabidi yasimame kwanza.” Aliongea Mwenyekiti .

“ Hapana, huwezi kusimamisha sherehe saizi. Shughuli ziendelee kama kawaida. Kaka na wifi nina uhakika watarudi. Kuna kitu inawezekana hakipo sawa kwao, ila niaminini mimi ,watakuja tu.” Aliongea shangazi.

Mwenyekiti aliafiki , James alinifata na kunichukua, nilipanda kwenye gari lake na msafara wa kuelekea nyumbani kwake ulianza. Njia nzima James alieleza jinsi alivyonipenda. Aliniambia jinsa atakavyohakikisha naishi kwa amani na furaha.

Alinibusu mkono na mashavu.

“ Nakupenda sana Emma.” Aliniambia.

‘Nakupenda pia James..” Nilimwambia. Maneno haya yalitoka mdomoni mwangu, Moyoni sikuwa nampenda hata kidogo, na wala sifahamua kwanini ilikuwa hivyo.

Masafara wetu wa magari ulichanja mbuga mpaka nyumbani kwakina james, tulishuka kwenye gari na kuingia ndani. Watu walikuwa wengi, pilika pilika zilikuwa nyingi sana.

“ Najua hauna furaha kwasababu ya wazazi wako, ila naomba uondoe shaka, kila kitu kitaenda sawa, nina uhakika watapatikana wakiwa wazima wa afya.” Aliniambia James. Masaaa yalikatika. Pilika za sherehe ziliendelea.

……………………..
Majira ya saa moja jioni, gari lilifika kutuchukua na kutupeleka ukumbuni.

“ Hivi ni sawa mimi kuendela na sherehe wakati sijui mama wala baba wapo wapi?” Nilimuuliza James.

“Sio sawa . Nazani hii sherehe tungeihairisha.” 

“Basi mpigie simu mwenyekiti wa kamati mwambie sherehe imehairishwa.” 

“ Sawa,” Aliongea James. Alichukua simu na kumpigia mwenyekiti wa kamati ya sherehe. Alimweleza jinsi ilivyokuwa vibaya kuendelea na sherehe wakati wazazi wangu hawajulikani walipo, mwenyekiti aliomba dakika kadhaa aweze kuongea na wanakamati.

Baada ya dakika kadhaa kupita, mwenyekiti alitupigia simu na kututaka tuende ukumbini. Alituambia shangazi yangu amefanikiwa kuongea na baba, na ametutaka tuendelee na sherehe. 

Moyo wangu ulipata amani, nilienda ukumbini.

Tukiwa katikati ya sherehe, kuna kijana mmoja alinifata pale mbele na kunipa kikaratasi kidogo . Alinipa kwa mficho sana ili James asikione. Nilikifungua haraka kuutazama ujumbe .

“ Mmmmmmh” Niliguna.


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU 21

“ Mmmmh!” Niliguna.

Nilisimama haraka na kumfata yule kijana, Ajabu sikumuona. Niliangaza macho ukumbuni kumtafuta. Kwa mbali nilimuona. Nilipiga hatua kumfata. Nilimshika bega. Aligeuka kunitazama.

Hakuwa yeye, nilimfananisha. 

“ Kuna tatizo ?” Aliniuliza yule kijana.

“ Hapana, nimekufananisha.” Nilimwambia. Nilitazama kila pande ya ukumbi kumtafuta, sikumuona.

“ Unafanya mambo gani? Rudi kwenye kiti chako.” Aliniambia mpambe wangu. 

Nilirudi.  

“ Unanini Emma?” Aliniuliza James.

“ Aaaa..a.aa….Nipo kawaida…” Nilimdanganya James. Sikutaka ajue kuhusu ujumbe niliopewa. Ujumbe ulikuwa umetoka kwa Mama. Ujumbe ulinitaka nisikubali kufanya mapenzi na James ule usiku. 

“ Wakati nafunga ndoa na marehemu Hans aliniambia hivi hivi! Na leo tena kaniambia hivi hivi? Kuna nini kinaendelea? Kwani James akiutoa usichana wangu nini kitatokea?” Nilijiuliza maswali mfululizo. 

Maswali yalinizidi, kichwa kilianza kuniuma.Nilihisi balaa lilitokea usiku wa harusi yangu na Hans linaweza kutokea tena. 

“ Hapana, MUNGU nisiaidie , Baba yake James asinifanyie kama alivyonifanyia Baba Hans.” Niliomba kimoyo moyo. Mapigo ya Moyo yalinienda kasi. Nilianza kutetemeka.

Nilijikuta nimetoka kwenye kiti na kuchuchumaa chini, nilikishika kichwa kwa nguvu na kukibinya. Mpambe wangu alininyanyua na kunikalisha tena kwenye kiti.

“ Unanini? Emmaa..Emma..” Aliniita James.

Kwa mbali niliona nyota nyota, sikuwaona watu vizuri. Nilihisi nataka kupoteza fahamu. Nilichukua maji na kujimwagia kichwani, Watu walinishangaaa.

“ Tumtoe hapa,, mshikeni tumtoe. Tumuwaishe hospitali…” Aliongea James. Pale pale watu walinibeba juu juu na kunitoa nje ya ukumbuni. Waliniingiza kwenye gari na kutaka kuniwaisha hospital.

Nikiwa kwenye gari baba yake James alifika kuniona.

“ Emma… kuna nini Mwanangu “ Aliniuliza.

“ Toka, usinishike. Tokaaaaa, mwanaharamu mkubwa wewe. Tokaaa, nimejua mbinu yenuu.” Nilimwambia. Nilimvamia na kumuangusha chini.

“ mbakaji wewe…..mbakaji…” Nilimwambia baba mkwe huku nikimpiga pale chini.

James alinishika kwa nguvu na kunitoa. Aliniingiza kwenye gari.

“ Emma amerogwa au?” Nilisikia wakiulizana.

“ Una nini Emma? Kwanini umemfanyia vile baba yangu? Umesahau kama yule ni baba mkwe wako? Kwanini umemuita mbakaji?’ Aliniuliza James. Sura yake ilionyesha kuumizwa sana na maneno yangu.

Sikumjibu, machozi yalinitiririka kwenye mashavu yangu.

“ Itabidi nikupeleke Hospital, unataka kuchanganyikiwa.” Aliniambia. 

Nilitikisa kichwa kukubaliana naye. Alitoka nje na kuwaaga ndugu zake. Aliingia kwenye gari na kutaka kuliondoa.

Lakini kabla hatujaondoka. Alitokea baba.

“ Mzeee ulikuwa wapi. Ona Emma anataka kuchanganyikiwa kwasababu yako.” James alimwambia baba. Baba haraka aliingia kwenye gari nililokuwepo. Alinishika mkono kwa nguvu na kuniuliza tatizo nini.

Uwepo wake ulituliza pressure yangu, kiasi nilihisi nafuu.

“ Kuna nini kinaendelea baba?” Nilimuuliza.

“ Hakuna lolote baya mwanangu, hakuna chochote cha kukutia wasiwasi. Kama ulikuwa na hofu kwasababu yetu naomba ondoa hofu yako. Naomba uwe na amani. Halafu huyu ni baba James, sio baba hans, umekosea kumtukana .” Aliniambia.

“ Mama yuko wapi? …” 

“ Mama yako sifahamu aliko, ila nina uhakika aliko yupo salama. Haupaswi kumuwaza . Haupaswi kuhairisha sherehe kwa ajili yake. Nakuomba jikaze tuendelee na sherehe yako, au kama umechoka nakuomba nenda hotelini ukapumzike na mumeo. Swala la mama yako achana nalo. Mama yako yupo salama, nina uhakika wa hilo, hata kama sijamuona ila nina uhakika wa hilo.” Aliongea baba.

“ Kuna vitu nataka nimuulize,, kuna vitu sivielewi …” 

“ Kama kuna chochote alikuambia na kina kupa ukakasi achana nacho. Naomba usikiwaze hata kidogo, kuna vitu vya kipumbavu mama yako amevifanya, ila havipaswi kukuumiza kichwa. Kuwa na amani mwanangu. Niamini baba yako.”  

Moyo wangu kidogo ulitulia. “ Bila shaka baba anajua kitu, kuniambia kwake niwe na amani inamaana anajua hakuna baya litakalo tokea.” 

Niliwaza. Nilimtazama James na kumwambia twende hotelini. 

Tuliondoka kuelekea Hotelini. Tuliacha watu wakiendelea na sherehe. Waliendelea kunywa na kufurahia ndoa yetu.

………………………..

“ Inaonekana unawapenda sana wazazi wako! Kutowaona siku moja kulikufanya utake kuchanganyikiwa. “ Aliniambia James.

“ Naomba tusiongee kuhusu hayo James, naomba tuongee mengine, naomba nisaidie kuyasahau yote yaliyotokea. Kichwa changu hakipo sawa, kuna mengi yananichanganya. Hapa nilipo sipo sawa kabisa.” Nilimwambia.

James alinishika mkono na kunibusu.

“ Usijali mpenzi wangu, nitafanya kila kitu kuondoa mawazo yako .” Aliniambia.

Tulifika hotelini. Tulichukua funguo na kuelekea kwenye chumba tulichopangiwa.

James aliingiza funguo kwenye kitasa na kufungua mlango. Aliusukuma, kwa pamoja tukaingia ndani, chumba kilikuwa na giza nzito, James alipapasa ukutani na kuwasha taa. 

Ajabu, tulimkuta Hans akiwa kitandani.

“ Hansiiii…………”  


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU- 22


“ Hansii……” Nilitamka kwa mshangao.  

Mapigo yangu ya Moyo yalienda kasi, Jasho lilinitoka. Nilianza kuona giza, macho yangu yalipoteza nuru. Niliishiwa nguvu.

“ Ndiiii..” Nilianguka chini. 

Nilipoteza fahamu pale pale.

……………..

Sikuelewa kilichoendelea. Nilikuja kupata fahamu na kujikuta nipo Hospital, nilikuwa nimezungukwa na ndugu zangu.

“hansi…hansiiii…..” Nilimtaja Hans punde baada ya kupata fahamu.

“ Emmaaaa mwanangu..” Alitamka mama na kunikumbatia kwa nguvu.

“ Ulikuwa wapi mama?” Nilimuuliza.   

Kabla hajanijibu, nilikumbuka tukio la Hotelini. 

“ Hansiii hajafaaa…alifika hotelini.” Nilitamka.

Maneno yangu yalionyesha kuwaumiza sana ndugu zangu . Sura zao zilionesha huzuni . 

“ Pole sana mwanangu..” Aliongea mama. Kabla sijamjibu ndugu zangu nao walinipa pole 

“ Pole sana Emma! Ila MUNGU mkubwa haya yote yataisha. Kwa uweza wake yote yataisha shangazi yangu.” Aliongea Shangazi. Kauli yake hii ilinifanya nihisi kuna kitu ambacho hakipo sawa. Pamoja na mimi kuzimia , nilihisi kuna jambo ambalo limetokea.

“ Nini kimetokea?” Niliuliza.

Kabla sijajibiwa, mlango wa hospital ulisukumwa. Aliingia baba, moja kwa moja alikuja kumshika Mama na kumvuta.

“ Toka hapa! Sitaki kukuona, ondoka haraka.” Alifoka baba.

“ Baba Emma nisamehe, nimekosa, naomba nisamehe.”  

“ Naomba ondoka, nenda ulikokuwa, sitaki kukuona hapa. Kwanza wewe ndio chanzo cha yote haya. Kama sio wewe haya yasingetokea. “ Alifoka baba kwa hasira.

“ Kaka usiseme hivyo, utampa wifi yangu matatizo. Unaposema yeye ndio chanzo maana yake hata haya mauaji yeye ndiye aliyesababisha.” Aliongea shangazi.

“ Mauaji? Mauaji ya nani? Nani kafa?” Niliuliza.  

Swali langu lilifanya chumba kizima kiwe kimya. Watu wote walikaa kimya. Waliangaliana kwa wizi , ni kama kila mmoja alimtaka mwenzie aseme. Baba alimvuta Mama mpaka nje ya wodi kisha akaingia tena ndani.

Aliwaomba ndugu wote watoke nje. Walitoka, tulibaki mimi na yeye.

‘ Nani kauwawa tena? “ Nilimuuliza .

kabla hajanijibu nilimkumbuka mume wangu, James.

“ James yuko wapi? Tangu nipate fahamu sijamuona? Yuko wapi James.” Niliuliza.

Baba alinishika mkono kwa nguvu, aliniangalia, macho yetu yaligongana. Ndani ya macho yake niliuona uchungu mzito.  

“ Emma…” Aliniita.

“ A.be…eeeee…” Niliitika.

“ Pole sana, Jamii mpaka sasa inaongea mengi sana. Kila mmoja anaongea lake kuhusu wewe. Lakini nakuomba uwe imara. Haya yote yatapita. Kwanza haya yote wewe sio chanzo. Usije ukajiona ni chanzo. Usije ukajiona unagundu.” Aliniambia.

“ Kuna nini baba, kwanza mume wangu James yuko wapi? ”  

“ James hayupo tena?” 

“ Hayupo! Hayupo kivipi? Nini imetokea?” 

“ Mumeo ameuwawa, amuewawa kikatili sana.”  

“ Eeeeh” Nilijiziba mdomo kwa mikono yangu, niliitoa ,Nilitaka kutamka maneno nilishindwa. Nilihisi kizunguzungu.  

“ ..ha…ns..iiiii….” Nilitamka. Baba alinifuta machozi na kuniambia muuaji amepatikana.

“ Wamemkamata hansi?” Niliuliza kwa hamaki.

“ Hapana mwanangu! Muuaji sio Hans, Hans alishakufa muda mrefu. Hans ni marehemu, muuaji sio hansi, muuaji ni Martini. Ushahidi umepatikana, kisu kilichotumika kumuua Hans amekutwa nacho Martini, pia hata alama za viatu vilivyokanyaga damu ni vya martini.”  

Maneno yake hayakuniingia akilini. Ubongo wangu uliniambia muuaji ni Hans na sio Martini.

“ Lakini mle ndani tulimkuta Hans, wala hatukumkuta Martini.”

“ Hans amekufa muda mrefu mwanangu! Mtu aliyekufa hawezi kuja kusababisha mauaji.” Aliongea baba.

“ Na mama anahusikaje na haya yote? Kwanini ulisema bila yeye haya yasingetokea?” Nilimuuliza baba.

“ Ipo hivi mwanangu, mama yako……..”


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU -23

“ Ipo hivi mwanangu, mama yako…..” Alisita. 

Aliangalia kushoto na kulia kisha akaendelea.

“ Mama yako tamaa imemzidi. Tamaa yake inataka kuharibu maisha yako.”

“ Tamaa yake kivipi? Kafanya nini? Kwanza alikuwa wapi. Na inakuwaje hiyo tamaa yake ikaharibu maisha yangu.?”  

“ Ni……” Kabla hajaongea, Mlango wa wodini ulisukumwa,aliingia Mama Hans.  

“ Baba Hans anawachezea akili, Martini hausiki na haya yaliyotokea. Yeye kumua James sio kweli. Sio kweli kabisa.” Aliongea Mama Hans. Tulitazamana na baba. Baba alimgeukia.

“ Polisi wamepata vithibitisho vya kumtia hatiani! Kinachoniumiza kichwa ni kitu kimoja tu, Kwanini amuue James? Kwanini?” Aliuliza baba.

“ Mnapoteza muda, muhusika sio Martini. Muhusika ni Baba Hans.”  

“ Kwanini unamtetea Martini na kumchongea mumeo?” Nilimuuliza.

“ Anamtetea Martini kwakuwa ni hawara yake. Yaani anaona bora bwana wake wa ndoa afungwe hawara yake aachiwe. Mwanamke hana maana huyu.” Aliongea baba. Kauli ya baba ilinikumbusha kauli ya mama kuwa Mama Hans na Martini ni mtu na hawara yake.

“ Sio kweli, Martini si hawara yangu. Ninachotaka mimi ni haki itendeke. Martini hajausika kabisa na mauaji ya James. Nina uhakika hata Emma anajua hilo, yeye alikuwa na James hadi hatua ya mwisho.”  

“ Inawezekana Hans ndiye muuaji? Lakini nikisema nani atanielewa? Wote wanaamini Hans ameshafariki.” Niliwaza Moyoni.

“ Emma ongea, wewe unajua nani ni muuaji?” Aliniambia Mama Hans.

“ Sifahamu nani aliyemuua James, tulipoingia mimi nilianguka na kupoteza fahamu.”  
“ Kitu gani kilikufanya upoteze fahamu? Naomba niambie kitu kilichokufanya upoteze fahamu.” 

“ Hansiii…nilimuona hansii chumbani…”  

“ Emma unaongea nini? Hansi alishakufa na tukamzika? Au uliona mzuka wake?” Aliuliza baba.

“ Hapana! Sio mzuka, mtu niliyemuona sio mzuka. Ni hans kweli.”

“ Si unaona. Kama ulimuona Hans . Maana yake aliyemuua James sio Martini ni Hans. Martini mnamuonea tu.”  

“ Mbona sielewi! Inamaana Mwanao Hans hakufa? Aliyejinyonga ni nani? Na yule tuliyemzika ni nani pia?” Aliuliza baba.

“ aaa….aaaaa……..a…..a’…..” Mama Hans alishikwa na kigugumizi cha gafla, bila shaka maneno aliyoongea aliyaongea kwa bahati mbaya. Akili yake haikutaka kuyaongea ila mdomo wake uliyoangea bila mwenyewe kuelewa.

Baba alimsogelea na kumshika mkono.

“ Niambie ukweli! Nifafanulie kila kitu. Kama aliyemuua James ni Hans, yule tuliyemzika ni nani? Aliyekufa ni nani? Na kama Hans hakufa kwanini mlitudanganya kuwa alikufa? Sababu ya kufanya yote haya ni nini? Kwanza alikuwa wapi kipindi chote hiki?” Aliuliza baba.  

Mama Hans alikuwa kimya. 

“ Mama mbona haujibu?” Nilimuuliza.

“ Aliyemuua James sio Martini, ni mtu mwingine. Swala la Hans silifahamu. Ninachojua ni Hans alikufa na akazikwa.” Aliongea Mama Hans.

“ Mmmmh!” Niliguna, kwa mshangao, tulitazama na baba. Mama Hans alikuwa anajichanganya, dakika hii alisema hans ndiye aliyemua James, dakika nyingine alisema anajua Hans amekufa.

“ Unamaana gani? Mbona haueleweki?” Baba alimuuliza. 

Badala ya kutujibu, Mama Hans alisimama na kuondoka. Aliondoka huku akisema Martini hausiki na mauaji ya James. 

“ Unauhakika uliyemuona ni Hans?” Aliniuliza baba.  

“ Ndio, ni yeye, nina uhakika wa asilimia zaidi ya tisini. Wala haukuwa mzuka wake, ni yeye mwenyewe.” 

“ Basi kama hivyo hata kipindi kile James alichovamiwa na kupigwa mtu aliyempiga ni Hans.” Aliongea baba.
.
“ Lakini inawezekana vipi? Mbona hainiingii akilini, mtu aliyekufa na kuzikwa anawezaje kuja na kuleta maafa?” Aliuliza baba. 

“ Ni kweli baba, haya mambo hayaingii akilini. Lakini mimi tangu wakati wa msiba wa Hans nilikuwa na mashaka. Kuna vitu niliviona haviko sawa.”  

“ Vitu gani havikuwa sawa?” Aliniuliza. Bila kumungunya maneno nilimueleza maduku duku yangu yote.

“ Kama ni hivyo kunauwezekano Hans yupo hai, lakini ilikuwaje wakafoji kifo chake. Mbona tulishuhudia akiwa ananinginia mle ndani? Lakini kwanini wafoji kifo? Kwa faidi ipi? Kitu gani kilichowafanya wafoji kifo?” Aliuliza baba.

“ Kuna mengi yamejificha , mfano ule usiku mama na mama mkwe walinitaka nisifanye mapenzi na Hans, kila nikilifikiria hili sipati jibu. Nazani linaweza likawa linauhusiano na haya.” Niliongea.

“Walikuambia usifanye mapenzi? ….basi nimejua….” Aliongea baba.  



NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU – 24

“Walikuambia usifanye mapenzi? ….basi nimejua….” Aliongea baba.  

“ Umejua?” Nilimuuliza kwa hamaki.

“ Ndio nimejua! Sasa nimepata mwanga.” Aliniambia. Kabla hajanifafanulia vizuri, alisimama na kuondoka. Aliniambia ataniambia kila kitu baada ya kurudi. Aliniambia kuna vitu vichache yampasa kuvihakikisha.

Aliondoka na kuniacha nikiwa na maswali .

………………….

Majira ya jioni, niliruhusiwa kutoka hospital, Mama alikuja kunichukua na kunipeleka nyumbani. 

“ Nimekuja kukuchukua kwasababu ya kiburi changu tu, baba yako akinikuta hapa anaweza kuniua. Sijui kwanini ananichukia sana siku hizi.”  

“ Baba hawezi kukuchukia bila sababu, umemkosea, umemkosea yeye pamoja na mimi. Kitu pekee unachoweza kukifanya ni kutueleza ukweli. Yakupasa utueleze Kila kitu.”  

“ Ni kweli, ili kuiokoa ndoa yangu yanipasa kuweka sawa kila kitu. Najua baba yako anajua chanzo cha yote ni mimi, lakini ukweli haupo hivyo, inawezekana kwa kiasi Fulani nikawa nimechangia, lakini kwa kiwango kikubwa sisi wote tumechangia hili swala, mimi, wewe, baba yako na shangazi zako. Sisi wote ni chanzo cha haya yote.”  

“ Hapana Mama, ukisema hivyo unakosea? Kwa mfano Mimi nimechangiaje haya? Kosa langu ni lipi?” 

“ Inamaana mpaka sasa haujui kinachoendelea mwanangu?” 

“ Ndio, sijui, naomba nifafanulie.” Nilimwambia.

“ Chanzo cha yote ni wewe mwanangu, kama usingefanya uliyofanya haya yote yasingetokea.”

“ aaaah! Mimi tena? Mbona sikuelewi?”

Badala ya kunijibu aliniuliza swali. “Unajua saizi unamiaka mingapi?”  

“ Miaka yangu imekujaje tena .”

“ Nijibu, unamiaka mingapi sasa?” 

“ 29..”

“ Sasa miaka 29 kuwa hivyo ulivyo unazani ni kawaida? Dunia ya sasa kuwa hivyo hadi leo sio kawaida.”

“ Unamaanisha nini?” 

“ Tumefika nyumbani, naomba niishie hapa, kule siendi. Baba yako ataniua.” Aliniambia mama.

“ Lakini…..”

Mama aliondoka. Hakusikiliza nilichotaka kumwambia, aliniacha nikiwa nimeduwaa. “ Makosa yake mwenyewe halafu anataka kunitupia lawama . Mimi kosa langu lipi? Nimefanya nini kusababisha haya yote?” Nilijiuliza. Niliamua kumpuuzia, Niliingia nyumbani.

Nikiwa mlangoni baba alitokea ndani.

“ Umerudi peke yako? Si ungepiga simu ningekuja kukuchukua.” Aliongea baba.

‘ Nilijua utakuwa bize, uliniambia unaenda kufatilia mambo.”  

“ Ni kweli, nimefatili baadhi ya vitu nimevijua. Twende ndani nikakueleze vizuri.” Aliniambia.

“ Lakini unajua kinachoendelea kuhusu James? Wazazi wake wametuzuia kuhudhuria mazishi yake. Hawataki wewe wala sisi tuende. Wanasema sisi ni chanzo cha yote yaliyotokea.”  

“ Hapana, lazima niende. James tayari alishakuwa mume wangu. Yeye na mimi , ni mke na mume, ni lazima niende kumuaga, ni lazima niudhurie msiba wake.” 

“ Ukifanya hivyo italeta shida zaidi, kwakuwa hawataki uende achana nao. Tena achana nao kabisa, kwanza wanajifanya wema wakati na wao wamechangia .” Aliongea baba.

“ mmmh! Unazidi kunichanganya baba, wamechangia kivipi?”

“Ni hivi, kwanza unakumbuka Usiku wa harusi yako na Hans uliniambia mama yako alikufata na kukuambia usilale na hans?”

“ Ndio, aliniambia usichana wangu nisimpe Hans.” 

“ Basi sababu ya yeye kukuambia vile ni wazazi wa James, wao ndio chanzo cha Mama yako kukuambia vile..”

“ mmmmmh! Unanichanganya baba. Wazazi wa James wanauhusiano gani na maneno ya mama. Kwanza wao nimejuana nao walipokuja kujitambulisha.”

“ Hivi vitu vinachanganya sana, lakini ipo hivyo, wao ni chanzo cha kauli ya mama yako. Walimwambia mama yako vile ili……..” Kabla hajamaliza nilimkatisha.

“ ili iweje, ili niolewe na mtoto wao halafu badae afe au?” Nilimuuliza.


NAJUTA KUTUNZA USICHANA WANGU – 25

“ ili iweje, ili niolewe na mtoto wao halafu baadae afe au?” Nilimuuliza.

“ Sidhani kama walijua kama atakufa.” Alinijibu baba.

“ Lakini kwa jinsi ulivyoniambia inamaanisha walikuwa wanauhakika nitaachana na Hans .Ndio maana walimwambia Mama anishawishiwi nisifanye mapenzi na Hans. Katika lugha nyingine walitaka mwanao anioe wakati nikiwa na usichana wangu. Hii kwangu ni kitu cha ajabu sana, unaendaje kwa mzazi wa mtu kumwambia amshawishi mtoto wake asifanye mapenzi na mumewe? Tena wakiwa wamefunga ndoa?” 

“ Ukifikiria sana haileti maana . Ila jamii yetu ina imani nyingi kuhusu bikra, ukute baada ya kusikia ni bikra waliamua liwalo na liwe. Ndio mana walimlaghai Mama yako akuambie usikubali kuutoa usichana wako. Pia wao wenyewe walikuwa wanaendelea na mbinu zao kuhakikisha ndoa yako na Hans haidumu.” 

“ Mbinu zao zipi? Au ndio waliomuua Hans ili niolewe na mtoto wao?”

“ Kuhusu hilo mwanangu Mimi sijui, ninachojua Mama yako alikuambia usilale na Hans kwakuwa alifanya mazungumzo na wazazi wa James. Kuhusu kifo cha Hans sielewi kabisa.”

“ Duuuh! Kwahiyo pamoja na kujua kuwa nimeolewa na Hans, wazazi wa James walimshawishi mama ili niolewe na James. Hivi kwanini walifanya haya yote, au ndio kwasababu ya bikra yangu?”  

“ Nahisi hivyo ila ukweli wote anaujua mama yako, nazani yeye anaweza kutusaidia.”

“ Tumuite tuongee naye. Naomba umsamehe kama atasema ukweli.” Nilimwambia baba. 

Baba alitikisa kichwa, ishara ya kukubaliana na maoni yangu.

……………….

Tulimwita mama.

“ Nimekuita hapa ili tuyatatue matatzio yanayotukabili, mwanao mpaka sasa roho yake ipo juu juu, haelewi kinachoendelea. Anajihis anamkosi . Naomba utueleze kila kitu. Usifiche kitu. Kila kitu ukikiweka wazi nitakusamehe.” Aliongea Baba.

“ Mnataka kujua nini?” Aliuliza Mama.

“ Yote, hasa kuhusu kifo cha Hans na uhusiano wake na wazazi wa James.Lakini kabla ya kutueleza hayo yote tuambie kwanini ulimzuia Emma kushirikiana na Mume wake. Sababu ilikuwa nini?”

“ Kuhusu hili mbona nilishawahi kuwaambia. Sababu kubwa ni kumlinda mwanangu, sikutaka usichana wake upotee kwa mtu asiye sahihi, ndio mana nilimwambia vile. Mtu sahihi kwake alikuwa James na sio Hans.” Aliongea mama.

“ Lakini hata huyo James mwishoni ulimkataa. Haukutaka niolewe naye ?” Nilimuuliza.

“ ..aaa…aaaaa……” Alishikwa na kigugumizi Mama. 

“ Unashindwa kujibu nini ? si umwambie ukweli, ulitaka James amuoe Emma kwakuwa wazazi wake walikuhonga hela, Martini alipokuhonga hela nyingi kuliko wao uliwaona hawana mana, ukataka mwanao asiolewe na James..” Aliongea Baba.

‘ Mimi niolewe na Martini?” Niliuliza kwa mshangao.

“ Ndio , mama yako alitaka uolewe na Martini, na ndio mana mwishoni alikuwa hataki uolewe na James. Martini alimpa hela nyingi. Kwakushirikiana na Martini walikuchawia ukamchukia James.”

“ Eeeeeh!” Nilistaajabu.

“ Kipindi cha harusi yako ,Mama yako hakupotea , alivyokuwa kwa Martini , Martini alimteka na kumtaka ampe hela yake.Mama yako alishindwa , hivyo akamfungiwa ndani. Na hata ule ujumbe wa kutaka usifanye mapenzi na james ulitoka kwake, Martini alimlazimisha Mama yako aandike .” Aliongea baba.

“ Mmmmmh! inamaana haya yote chanzo ni bikra yangu? Ina nini hii bikra? Mama uliwahi kuniambia mimi ni chanzo, naomba nifafanulie, kuna nini kinaendelea kwenye hii bikra yangu?”  

Ajabu, badala ya kunijibu, Mama aliangua kicheko. Kama mwenda wazimu alicheka.

“ aaahahaha..ahahaha..ahahahaha…ahaha…..” Alicheka hadi akapaliwa .

Tuliangalia na baba kwa mshangao. Hatukuelewa ni kitu gani kinamchekesha.

 “ahahaha..ahahaha…..ahahaha…..”  


NAJUTA KUTUNZA USICHANA WANGU- 26

“Aahahahah…ahahahaha…ahahaha…..” Alicheka.  

“ Unamaanisha nini kucheka hivyo ?” Nilimuuliza. Badala ya kunijibu aliendelea kucheka.

“ ahahaha..ahahahah…ahahahah….”  

“ Mama Emma unatupotezea muda, mwanao amekuuliza swali, badala ya kumjibu unacheka. Maana yake nini? “

“ aah…ahaha..ah…ahaa……..u..na….ju…a…….ahaha….ahahah……” Aliendela kucheka. Kila alipotaka kuongea alishindwa. Baba uvumilivu ulimshinda. Alimpiga kibao .

“Acha upumbavu! Kitu gani kinachokuchekesha?” Aliuliza kwa ukali. 

Kibao kilimfanya atulie.

“ Ndio unipige?” Aliuliza.

“ Niambie kinachokuchekesha.”

“ Kwahiyo umeona kunipiga ndio dawa . Sasa sisemi, kama unaamua kuniacha ,niache, ila sisemi.” Aliongea kwa hasira. Alisimama na kutaka kuondoka. Kitendo kila kilimkera zaidi baba. Alimvamia na kuanza kumpiga.

“ Najuta kukuoa wewe mshenzi…” Aliongea Baba. Alimshika mkono na kumpiga shavuni. Kabla hajakaa sawa,alimpiga mateke na mangumi. Kama mzigo Mama alianguka chini. Baba hakujali, alimvamia na kuendela kumpiga. Nilisimama kumzuia. Nilishindwa. Baba alinisukuma pembeni.  

“ ..nipige….nipigee tu…” Aliongea mama.

Maneno yake ni kama yaliamsha mashetani kwa baba. Aliendelea kumpiga . Taratibu moyo wangu ulianza kuingiwa na simanzi, nilimuonea huruma.

“ niue…niuee…..” Aliongea mama.

“ Niueee…puuuuu….Niue….puuuuuu….nNiue…puuuu….” Kila mama aliposema niue baba alimpiga. Hali ya mama ilianza kuwa mbaya, alitoka damu puani na masikioni. Nilimsihi baba amwache, baba hakumuacha, aliendelea kumpiga.

“ Nisameheee….nisameheeeeeee……” Aliomba samahani mama . Kipigo kilimzidia. 

“ Nisameheee, nimekosa… nisameheeee…”   

“ Puuu…puuuu…” Baba aliendela kumpiga huku akimtaka aeleze ukweli.  

Mama alieleza. Alieleza kila kitu alichokijua.

“ Kama umenipiga sababu ya kucheka umenionea, umenionea bure mume wangu. Kilichonichekeza ni maneno ya Emma. Kwa jinsi alivyouliza swali lake ilibidi nicheke ila naomba mnisamehe kama nimewakwaza, ila kiukweli hakuna ninachojua zaidi ya niliyowaambia. Na kili makosa yangu kuwa nilimshawishi Emma asikubali kutolewa bikra na Hans kwakuwa nilishaongea na wazazi wa James, na waliniahidi kama nitafanikiwa kuivunja ndoa ya Hans na Emma basi wangenipa hela nyingi, lakini kuhusu kifo cha Hans sijui kitu, japo kifo chenyewe kinautata mwingi” Aliongea mama.

“ Na kuhusu kupotea kwangu ni kama mume wangu ulivyoeleza, Martini aliniteka baada ya kuona unafunga ndoa na James wakati nilimuahidi atakuoa kama atamtoa baba yako gerezani”

“ Kwahiyo baada ya kuona nataka kuolewa na James akaamua kukuteka?” Nilimuuliza.

“ Ndio, alipoona vile,Martini alichukia na kuamua kuniteka, na hata ile karatasi ya kukutaka usilale na James ilitoka kwangu kweli. Martini alinilazimisha niandike.”  

“ Na vipi kuhusu mauaji ya James, ni kweli Martini kahusika?’ Aliuliza baba.

“ Kuhusu hilo sifahamu, na sina uhakika sana. Ila kwa jinsi vielelezo vyote vinavyomtaja Martini nakuwa na mashaka. Kama Martini angekuwa Muuaji basi vielelezo visingemtaja yeye.Ni lazima angeondoa ushahidi, kitendo cha kila kitu kumtaja yeye inaonesha kuna mtu kapanga Martini aonekana muuaji.”  

“ Hata mimi nahisi hivyo.” Aliongea baba.

“ Lakini pamoja na maelezo yako yote, hujajibu swali langu. Kwanini hawa watu wote wahangaike hivi na mimi? Shida ni hii bikra yangu au kuna kitu kingine?” Nilimuuliza mama.

“ Kuhusu hilo hata mimi mwenyewe sielewi, nashindwa kuelewa kwanini watu wanapambana hivi hadi kutaka kuuwana kisa bikra, nashindwa kuelewa kuna nini kwenye hiyo bikra, nazani tukiwapata wenyewe watatueleza vizuri.”  

“ Huu ni mtihani, kuna nini kilichojificha kwenye huu usichana wangu? Hii bikra yangu ina nini cha ajabu? Kipi hasa?” Nilijuliza moyoni. 

NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU -27

“ Hii bikra yangu ina nini? Kuna Kitu gani cha ajabu kwenye huu usichana wangu?” Nilijiuliza moyoni. 

Sikupata jibu, Kila nilipowaza kichwa changu kilizidi kuuma .

Nilichukua vidonge vya kutuliza maumivu na kuvimeza.

…………………………..

Siku ya pili yake, ilikuwa ni siku ya msiba wa James. Pamoja na baba kunionya nisiende. Nilienda. Nilijitanda na kuelekea msibani.

Nikiwa maeneo ya msibani, watu waliniteta na kuninyoshea kidole. Kila mmoja aliongea lake, Sikujali, niliingia ndani ,moja kwa moja nilienda kwenye chumba cha wafiwa.

Nilimsogelea Mama James na kumpa pole. Ajabu, hakunijibu kitu, hata mkono wangu hakuupokea, alinitazama kwa jicho baya sana, Sikujali, niliwasalimia ndugu wengine, nao hawakunijibu, niliamua kukaa mle ndani kusubiri taratibu nyingine.

“ Hiki ni chumba cha wafiwa, wewe ni nani umeingia huku?” Aliniuliza wifi yangu.

Kabla sijamjibu Mama James alidakia.

“ Umemuua James halafu bila aibu unakuja kwenye msiba.” Aliongea Mama James..

“ Huyu binti kumbe anadharau sana, halafu hatupaswi kuongea naye hivi.” Aliongea shangazi James na kunivamia. Mama James alimzuia na kumtaka aniache. Pamoja na kunitetea, mama James alinitaka niondoke mle ndani, alinitaka nitoke nikakae nje.

“ Lakini James ni mume wangu! Tulishafunga ndoa kanisani.” Niliwaambia.

“ Ndoa yenu nilishaifuta, wewe hujawahi kuwa mke wa mwanangu, kama ungekuwa mke wake usingeruhusu mahawara zako wamtoe roho.” Aliongea wifi.

“ Hawara?” 

“ Ndio, unajifanya kuuliza kwa mshangao, kwani unadhani siri. Kila mmoja anajua kuhusu hilo. Malaya mkubwa wewe, Unajifanya bikra kumbe hauna lolote lile.” 

“ Lakini…..”

“ Hakuna cha lakini Malaya wewe, hebu toka kwanza humu ndani.” Aliongea Mama James.

Kuondoa shari, niliamua kusimama na kutoka mle ndani. Nilienda kukaa nje na watu wengine.Ajabu, nao pia walinikwepa, walisogea pembeni na kuniacha peke yangu.

“ Huyu dada anamkosi, sio bure.” Niliwasikia wakinongonezana. 

Maneno yao yalinifanya niishiwe nguvu, nilitamani kuondoka nilishindwa. Kihere here changu cha kwenda msibani kiliisha. Kinyonge sana, nilijikaza na kuendelea kubaki.

Masaa yalikatika. Muda wa kuzika ulifika. Tofauti na msiba wa Hans, huu buriani ilifanyika. Watu walipita kuaga mwili wa marehemu. Baaada ya misa na buriani, tulielekea makaburini kuzika. Taratibu zilifanyika, marehemu akazikwa. 

Wakati shughuli yote inafanyika sikushirikishwa kwa lolote, hata kuweka taji sikwenda, Pia hata kwenye wasifu wa marehemu hakuna sehemu waliyotaja kama marehemu ameacha mke. Nilijisikia uchungu sana lakini sikuwa na namna. Baada ya kumaliza kuzika,sikukaa, nilichanja mbuga kurudi nyumbani.

Kichwani nilielemewa na mengi.

“ Hivi ni kweli ninagundu?” Nilijiuliza.

‘ Gundu imetokana na nini? ni hii bikra yangu?” Nilijiuliza Tena.

“ Yanipasa kufanya jambo, bila ya hivyo maisha yangu yanaweza kupotea kizembe. Kitu cha kwanza ni lazima nitafute ukweli kuhusu bikra yangu. Kitu gani kinafanya watu waitake kwa udi na uvumba. Pili ni lazima nitafute ukweli kama nina gundu au lah.” Nilijiambia.

Nilitembea taratibu kurudi nyumbani.  

Nikiwa barabarani peke yangu, nilihisi kuna mtu nyuma yangu, nilitaka kugeuka, kabla sijageuka alinishika bega. Niligeuka kumtazama.

“ aaaaaah” Nilistaajabu. Hofu na mshangao vilinishika . Alikuwa Hans. Wakati mimi nimeduwaa, sijui nifanye nini, yeye alitabasamu, meno yake yote 32 yalikuwa nje kwa tabasamu.

“ Hatimaye nimekupata.” Aliniambia.


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU -28

“ Hatimaye nimekupata.” Aliniambia

Alitabasamu na kuangua kicheko. 

Mwili wangu ni kama ulichomwa sindano ya ganzi, nilitetemeka kwa woga, kwa shida nilipiga hatua kurudi nyuma. 

“ Usiogope Emma. Ni mimi, ni mimi mumeo. James hajawahi kuwa mumeo, hata makaburini wameshindwa kukupa heshima yako. Taji hujamwekea wala kwenye wasifu hujatajwa.” Aliniambia.  

Niliendelea kurudi nyuma, alinisogelea, nilipoona anakaribia nilitimua mbio.

“ Emmmaaaa…Emmmaaa…..” Aliniita.

Hakuniacha, alinifukuza kwa nyuma. Sikusimama, nilikimbia. Barabara ilikuwa ndefu, hakukuwa na mtu wala nyumba pembeni.

“ Emma simama. Mimi sio mzuka kama unavyodhani. Simama tuongeee. Simama nitakueleza kila kitu.” Aliniambia. 

Maneno yake hayakunishawishi kusimama. Nilitimua mbio kama mwenda wazimu. 

Kadri sekende zilivyozidi kukata, Pumzi nazo zilianza kuniishia, nilipunguza mwendo, Hans naye alipunguza mwendo.

“ uuuuuu….uuuuuuu…..” Nilimsika akihema kwa nguvu.

“ Uuuuuu…uuuuuuu…..” Nami nilihema kwa nguvu.

“ Simama tuongeee. Simama nikuambie kila kitu. Haupaswi kuwa na mashaka juu yangu.” Aliniambia. 

Kiasi Fulani moyo wangu ulianza kumuamini, lakini pamoja na moyo kumuamini, ubongo wangu ulikataa kumuamini.

“ Hapana, sipaswi kudanganywa kirahisi hivi.” Niijiambia. Nilijikaza na kuendelea kukimbia.

…………..

Kadri muda ulivyoenda nilikuwa nikiishiwa pumzi zaidi , Uwezo wangu wa kukimbia nao ulipungua. Hans alinikaribia, nilijitahidi kukimbia nilishindwa. Hans alifanikiwa kunishika. Nilimsukuma.  

“ Niacheeee…sitaki …niacheeee…” Nilimwambia.

“ Tulia…tulia…..”  

“ Sitakiiii…niacheee…” Nilimwambia. Nilimngata mkono alionishika, akaniachia, nilitimua mbio tena, lakini kabla sijafika popote, nilipigwa na kitu kizito kichwani. Pale pale nilianguka chini na kupoteza fahamu.
……………………..

Nilikuja kushtuka nikajikuta kwenye kachumba kadogo kenye giza totoro, mlango ulifunguliwa akaingia Mtu ambaye sikumjua kutokana na giza. Nilijaribu kusimama , nilishindwa, nilikuwa nimefungwa kamba miguuni, yule mtu alisogea ukutani na kuwasha taaa.

Baada ya kuwasha taa nilimjua, alikuwa Hans.

“ Tatizo lako Emma mbishi sana, muda wote nakuambaia nisikilize hutaki. Ona sasa nimetumia nguvu na matokeo yake umeumia.” Aliniambia. Mguuni nilikuwa nimechubuka kidogo, damu zilikuwa zikinitoka.

“ Kwanini unanifanyai hivi? Kosa langu ni lipi? Kosa langu kukupenda au?” Nilimuuliza.

“ Kunipenda? Acha masihara Emma? Wewe mimi hujawahi kunipenda. Toka tumejuana haujawahi kunipenda. Wewe na ndugu zako mlipenda hela zangu. Ulikubali kuolewa na mimi kwasababu ya hela zangu, wala haukunipenda..” 

“ Hans leo unasema hivyo? Mapenzi yangu yote yalikuwa bure kwako, au kwakuwa nilikataa kufanya mapenzi kabla ya ndoa?”  

“ ahahaha..ahahaha….” Alicheka Hans.

“ Acha kunichekesha Emma, sikuambii haya kwasababu ya kufanya mapenzi kabla ya ndoa. Tangu nikujue sikuwahi kutamani kufanya mapenzi na wewe, sikuwahi kuvutiwa na wewe wala na bikra yako.” 

“ Mmmmmh sasa kwanini ulitaka kunioa? Sababu ya kulipa mahari nyingi vile ni nini?” 

“ Sababu utaijua leo, ila jua sikuwahi kukupenda. Kwanza nilikuoa kwasababu ya mtu mwingine wala sio mimi. Nilikuoa hili bikra yako nimuuze mtu. Na nilishachukua hela kwa mtu kwa ajili ya bikra yako.” 

“ Ulinioa kwasababu ya mtu mwingine, nani huyo?” Nilimuuliza.

 Hakunijibu, alisogea mlangoni na kufungua mlango.

“ Ingia..” Alimwambia Mtu aliyekuwa nje.

Alinigeukia na kuniambia.

“ Mtu mwenyewe Huyu hapa……”


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU -29

“ Huyu hapa…” Aliniambia.

Nilimwangalia mtu aliyeingia, alikuwa baba yake mzazi. 

“ Ulinioa kwa ajili ya baba yako?” 

“ Ndio, kama nilivyokueleza mwanzo, sijawahi kukupenda. Nilikutongoza kwa ajili yake.” Aliniambia Hans.

“ Usiku wa Harusi yetu tulipanga tukufanyie mchezo Hotelini. Baadae tulibadilisha mipango baada ya Martini na Mama kuingilia mpango wetu. Mama alikuwa anataka hawara yake ndiye atoe bikra yako. Hivyo aliandaa mazingira ya kukupeleka kwa hawara yake. Alikodi chumba na kumuweka Martini ndani. Nilishtukia mchezo wao, nilimteka Martini na kumwambia Baba aende yeye.”

“ Ndio maana ulimruhusu Mama yako anichukue kirahisi pale Hotelini? …”

“ Ndio, kabla ya kuja alinipigia simu na kunidanganya eti anataka akakufunde, nilijua mpango wake, hivyo nilimkubalia kwakuwa na mimi nilishapanga mipango yangu.” 

“Eeeeeh!”

“ Usishangae, ndio ilikuwa hivyo. Mama huku akijua anakupeleka kwa Martini alikupeleka kwa Baba. Lakini kabla baba hajafanikiwa ulileta ushenzi wako, ukamsukuma baba na kumdhuru, kitendo kile kiliharibu mpango wetu, ilibidi tuingie kwenye mpango wa pili. Mpango wa pili ulikuwa ni mimi kutengeneza mazingira ya kufa ili urithiwe na baba. Tulimuandaa mzee saidi aseme mila zetu zinataka hivyo, lakini Mzee Saidi naye alikuwa upande wa Mama.”

“ Waliwakodi vijana wakamkamata Baba na kumweka kwenye mfuko, walimtoa nje wewe ukiwa unafanyiwa tambiko uwanjani.” Aliongea Hans. 

Nilikumbuka, ni kweli siku ya tambiko vijan walitoka nje wakiwa wamembabe mtu kwenye mfuko.

 “ Lakini kama wale vijana walitumwa na mama yako kwakushirikiana na Martini, mbona wale wale walikuja kunitoa mle ndani tena?” Nilimuuliza.

“ Baada ya kumtoa baba nje niliwafata na kuwashawishi wakuokoe, niwalipa hela nyingi kuliko waliyolipwa na Martini akishirikiana na mama.” Alinifafanulia Hans.



“ Kwanini mfanye haya yote, lengo kubwa ni nini? Kwahiyo baba yako akinitoa usichana wangu anafaidika na nini?” .

“ Utajua baada ya kutembea naye, hapa hautatoka mpaka bikra yako itoke.” 

“ Hapa hauna ujanja, hakuna mtu wa kukusaidia, mpinzani wangu Martini yuko jela.” Aliongea Baba Hans.

“ Kwanini mnanifanyia hivi?”

“ Utajua baada ya tukio, la msingi ni kuwa mpole. Halafu kipindi kile kunamakosa tulitaka kufanya. Nilitaka kukutoa usichana wako wakati hauko hedhi, ili mambo yaende vizuri yanipasa niutoe usichana wako wakati ukiwa hedhi. Tutakufungia mpaka upate hedhi. Ukipata hedhi nitakuja kutoa usichana wako. Baada ya hapo utajua kwanini nafanya haya yote.” Aliongea Baba Hans.

“Wakati tukisubiri upate hedhi, tutakupa adhabu kwa usumbufu uliotupa. ” Aliongea Hans.

“ Lakini nimekukosea nini? Kosa langu ni lipi? Kwanini mnanifanyia hivi?”  

“ Upumbavu wako ndio umekuponza. Usingemsukuma baba siku ile haya yote yasingetokea, Zoezi lingeisha kistaarabu, wala mimi nisingejifanya nimekufa ili urithiwe na baba. Upumbavu wako umenifanya nidanganye kufa ili urithiwe na baba, lakini pamoja na hilo bado ilishindikana, gundu zako zilipelekea Mama naye atake hawara yake akubikiri yeye,mambo yetu yote yameharibika. Maisha yangu yote yanipasa niishe kama nimekufa. Baba akisha kubikiri nitaondoka, nitaenda kuishi mbali.” Aliongea Hans.

“ Unamwambia hayo yote ya nini? Huoni kama muda unaenda.”  

“ Ok sawa…” Aliongea Hans. Alielekea mlangoni na kutoka nje.

“ Ni lazim uilaani siku uliyozaliwa, ila usiwaze sana,Maisha ndivyo yalivyo, Ni lazima uumie ili mimi nipone. Ni kama mbugani hivi, swala wanalia kwa maumivu lakini Simba wanafurahi kwa mlo. Maumivu yako ni furaha yangu.”  

“ Haupaswi kunifanyia hivi, hakuna kosa lolote nililokufanyi kustahili ubaya huuu, na kama lipo naomba unisamehe. Nisamehe …”  

“ Hakuna utakachofanya kitakachokusaidia hapa, nimeisubiri hii siku kwa muda mrefu sana. Leo imekuja halafu nikuachie kirahisi rahisi . Hilo haliwezekani, haliwezekani kabisaa .” Aliniambia. 

Mlango wa kile chumba ulisukumwa tena. Aliingia Hans akiwa kashika kikopo kidogo cha mafuta. Alikifungua na kuanza kunipaka mwilini, alichana nguo na kuanza kunipaka mafuta. Alinipka kila sehemu hadi sehemu zangu za siri.

“ unataka kunifanya nini?” Nilimuuliza.

“ Nataka nikupe kumbukumbu, kumbukumbu ambazo ukizikumbuka utatamani kufa.” Aliniambia huku akiendelea kunipaka mafuta maeneo ya nyuma.

“ Mnataka kunifanya nini?”   

NAJUTIA KUUTUNZA USICHANA WANGU- 30

Nilihisi kitu walichotaka kunifanya. Nilipiga kelele kuwaomba waniachie.

“ Msinifanye hivyo tafadhali.” Niliwaomba.

Hawakujali, baada ya kunivua nguo zote na kunipaka mafuta. Hans na baba yake walivua nguo zao na kujipaka mafuta sehemu zao za siri.

“ Wanataka kunibaka?” Nilijiuliza.

“ Hapana, walisema mpaka nipate hedhi.” Nilijijibu.

“ Lakini kunipaka mafuta makalioni kuna maana gani? Wanataka kuninajisi au?” Nilijiuliza.  

“ Hans niambie, mnataka kunifanya nini?” Nilimuuliza. 

Hakunijibu, Baada ya kumaliza kunipaka mafuta walinisogelea. Hans alinishika kwa nguvu na kunilaza kwenye kagodoro kadogo kalikokuwepo mle ndani.

“ Hivi hivi atatusumbua huyu.” Aliongea baba Hans.

“ Kwahiyo ulitaka tumfanyaje?” Aliuliza Hans.

“ Tumfunge kamba.” .

“ Sawa.” Alijibu Hans. Aliangaza mle ndani kutafuta kamba. Aliipata. Alinikamata na kunifunga mikono.

“ Mikono inatosha. Haina haja ya kumfunga miguu.”

“ Haina shida….Lakini mwanangu . Kuna kitu nakiona hakipo sawa. Kufanya sasa sio sawa, ni busara na vyema kama tukimfanya baada ya mimi kumtoa usichana wake. Tusubiri apate hedhi, nimtoe usichana wake ndipo tulifanye hili.” Aliongea baba Hans.

“ Sababu kubwa ni ipi ya kufanya hivyo?”

“ Sababu kubwa ni najisi, unajuwa tukimfanya huyu mtu atakuwa na roho uchafu ya uzinzi. Siku nitakayomtoa usichana inawezakana kabisa ninachokitaka nisikipate kwakuwa tayari atakuwa ameshachafuka.”

“ Lakini hayo hayakuwa makubaliano yetu. Hatukukubalina hivyo.”

“ Najua hilo, ila kwasasa naomba nielewe. Naomba tufanye kile ambacho mimi nakuambia. Na hii ni kwa faida yetu wote. Hivi utajisikiaje kama mimi nitamtoa usichana halafu mipango yetu ishindwe kufanya kazi? Huoni kama itakuwa balaaa, italeta shida sana. Nina uhakika hata wewe hautaniamini na mwishowe mimi na wewe tunaweza kugombana maana kila kitu kinategemea hili zoezi letu.” 

“ Nimekuelewa mzee wangu.” Alijibu Hans. Alinisogelea na kunifungua kamba.

“ Ahsante…” Nilimshukuru.

“ aaah! Ahsante? Unazani tunakuacha?” Aliniuliza kwa dharau. Alimtazama baba yake kwa pamoja wakacheka. Walicheke kwa nguvu mpaka nikaogopa. Huku wakicheka, waliondoka na kuniacha peke yangu.

………………..
Siku zilikatika nikiwa nimefungiwa mle ndani. Asubuhi, mchana , jioni, Hans alikuwa akiniletea chakula. Sikuwa na hamu nacho kabisa. Sikusikia njaaa, Hans alinilazimisha kula. Aliniambia nile nongeze damu. Aliniambia nikipata hedhi baba yake ataninitoa usichana wangu.  

Nilijaribu kila mbinu kumbembeleza aniache , nilishindwa. Aliendelea kuniletea dharau na kunifanyia vitu ambavyo vilinifanya nizidi kumchukia . Alikuwa ananilamba lamba na kuniambia ananitamani sana.

“ Umeanza kunivutia, tatizo nimeshakubaliana na baba. Siku nilizokuwa hapa nimeanza kukutamani. Nakutamani sana..” Alionea Hans huku akinilamaba shingo. Niligeukia pembeni na kujaribu kumkwepa, ilikuwa bure, alizidi kunilamba.

“ Daaaah! Mzee wangu ataenjoy sana..” Aliniambia huku akinilamba.

Akiwa ananilamba, nilihisi kitu sehemu zangu za siri. Nilihisi kitu kikitoka.  

“Mungu wangu, nimeanza kubridi.” Nilijiuliza moyoni. Niliibana miguu na kujaribu kumzuga Hans asigundue.

Nilimuongelesha na kumkazia macho ili aniangalia usoni, sikutaka aangalie chini. 

Nilijitahidi kuibana miguu na kumuongelesha Hans.

“ mmmh! Mbona kama umebadilka gafla?” Aliniuliza.

“ Nimebadilika?” 

“ ndio..” Alinijibu Hans.

Haraka alirudi kwa nyuma na kunitazama. Aliniangalia kutoka juu mpaka chini. Alinisogelea na kunitanua miguu. 

“ ahahaha…ahahaha……” Alicheka kwa nguvu. Alitoka mle ndani mkuku , sekunde kadhaa mbele alikuja na baba yake.

“ Tayari, amepata hedhi” Aliongea. Baba yake alinisogela na kunitanua miguu, kwakutumia vidole vyake alipapasa sehemu zangu za siri.

“ yaaah! Ni kweli..” Aliongea. 

Kwapupa alianza kuvua suruali yake.  

“ Hatimaye leo nimefanikiwa, nimefanikiwaa…” Aliongea.


NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU- 31

“ Hatimaye leo nimefanikiwa, nimefanikiwa…” Alitamka kwa Furaha Baba Hans. Sura yake ilijaa furaha isiyokuwa na kifani.

Wakati yeye akiwa anafurahi , mimi nilikuwa nalia kwa uchungu. Furaha yake ilikuwa maumivu kwangu. Nilijiuliza nimemkosea nini MUNGU. Nilijilauma kuutunza usichana wangu. Nilijutia, nilijiona mpumbavu sana.

Tabasamu la Baba Hans lilinifanya nikumbuke maneno ya mwalimu wangu shule. Aliwahi kuniambia binadamu ni wanyama hatari, aliniambia afadhali ya Simba kuliko mwanadamu, kipindi kile ananiambia sikumuelewa, lakini sasa nilimuelewe na kumuamini. Macho yangu yalithibitisha ukatili wa wanadamu.

Wakati Baba yake akiwa na shauku kubwa, Hans ni kama alikuwa na jambo.

“ lakini mzeee….” Aliongea Hans.

‘ Nini tena?” Aliuliza Baba Hans

“ Uliniambia kabla ya tukio utatimiza nusu ya ahadi. Naomba utimize kwanza.”

“ aaaah! Inamaana Hans hauniamini baba yako? Yote tuliyoyafanya pamoja leo unakuja kukosa imani na mimi?”

“ Hapana baba, sio kwamba nakosa imani. Ni vyema ukatimiza makubaliano kabla jambo halijatendeka. Unajua mimi ndiye nitakaye pata tabu. Maisha yangu yote yatanipasa kuishi kama mtu aliyekufa. Tena inabidi niende mbali. Sasa mambo yakienda kombo na wewe usipotimiza ahadi yako itakuwaje? Sura yangu nitaiweka wapi? Aliuliza Hans.

“ Mwanangu mbona nashindwa kukuelewa? Unaanzaje kulete vikwazo saizi? Yaani muda wote uliovumilia saizi unashindwa kuvumilia saizi?”  

 “ Si……” Kabla Hans hajamaliza kuongea, Baba yake aliniacha na kutoka nje.

“ Kwenye hela hakuna baba wala mama. La msingi hapa ni mzigo wangu.” Aliongea Hans baada ya baba yake kuondoka.

“ Kwahiyo unaniuza kwa baba yako?”  

“ Tunza nguvu zako, kuongea hakukusaidii lolote.” 

“ Ukinisaidia sasa nitasamehe na kusahau yote. Nisaidie Hans, najua uenda kuna kitu kibaya nilikufanyia.Naomba nisamehe kwa huo ubaya ambao siujui.” Nilimwambia.

“ Emma…” Aliniita.

“ Abeee….”

“ Kitu gani kilikufanya ujitunze mpaka leo? Kitu gani kilikupa nguvu ya kuwakataa wanaume wote na kuhifadhii usichana wako mpaka leo?” 

“ Unataka kujua ukweli?” 

“ Ndio, “

“ Sababu kubwa ni imani niliokuwa nayo. Maisha yangu yote nimekuwa nikiamini kufanya ngono kabla ya ndoa ni kosa kubwa, ni uasherati. Pia, mwalimu wangu wa dini aliwahi kuniambia mtu atakayenitoa usichana wangu anapaswa kunioa .” 

“ Unaroho ngumu sana, lakini sidhani kama hiyo ndio sababu ya pekee, lazima kuna kitu kingine.”

“ Kitu kingine kipo , na kitu hicho ni chuki zangu kwa tendo lenyewe. Kiukweli Ngono imejaa kinyaa sana. Mara zote nilipowasikia watu wakiizungumzia niliichukia. Kitendo cha kufanyika mkiwa uchi wa mnyama kinatia kichefuchefu sana. Na ndio mana nilijitahidi sana kukikwepa hadi ndoa, lakini bahati mbaya baada ya kupata furaha ya kuutunza uke wangu na kumkabidhi Mume wangu naambulia majanga, ni majanga juu ya majanga.”  

“ Nakuonea huruma lakini sina namna, sina jinsi ya kukusaidia, baba akija na mzigo wangu nitaondoka na kukuacha naye. ”

“ Sawa, kama umekataa kunisaidia basi naomba uniambie kitu kimoja tu.” 

“ Kitu gani?” 

“ Ni kuhusu bikra yangu, ina nini mpka mnaigombania hivi?”

Kabla hajanijibu, aliingia Baba yake. Alivua nguo zake na kunisogelea.Aliniangusha kwenye godoro, kama mbuzi alinishika miguu kwa nguvu na kutaka kuniingia.

“ Mzee mbona unakuwa sio muelewa? Mzigo wangu uko wapi?” Aliuliza Hans

“ Nenda chumba cha mwisho kule, utakuta mzigo wako. Tena sio robo kama tulivyokubaliana.” Aliongea . Hans pale pale alitoka na kuelekea alikoambiwa.

Hans akiwa naondoka, alinishika miguu kwa nguvu na kutaka kuniingia, lakini kabla hajafanya lolote, kilisikika kishindo kikubwa kutoka kule alikoenda Hans.

“ aaaaa…aaaaaa……” Kwa mbali nilimsikia Hans akipiga kelele. 

Baba yake hakujali, alitabasamu.

 
NAJUTA KUUTUNZA USICHANA WANGU -32

Baba yake hakujali ,alitabasamu.

Alinishika miguuu kwa nguvu na kutaka kuniingia.

“ Nakubaliji nidharilishwe kirahisi hivi?” Nilijiuliza moyoni.

“ Hapana, inanipasa kupambana.” Nilijiambia. Pale pale nilianza kuibana miguu yangu kwa nguvu. Nilimsukuma baba hans kwa mwili wangu na kuibana miguu.

“ paaaaah! “ Alinipiga kibao.  

“ Unajichosha bure, ni bora ukawa mstaarabu . Hiki unachokifanya hakitakusaidia lolote.” Aliniambia. Aliishika miguu yangu kwa nguvu na kuitanua. Alizishika nyeti zake na kutaka kuniingia, kitendo cha kuzishika nyeti zake kilinipa mwaya wa kubana miguu tena. Niliibana.

“ paaaah! “ Alinipiga kibao cha shavuni tena.

“ Kwanini unataka nikudhuru? Kwanini hautaki kuwa mstaarabu.” Aliniambia.

Sikumjali, niliinuka mzima mzima na kumvamia. Wote kama mizigo tulianguka chini. Niljaribu kukata kamba walizonifunga nilishindwa.Kwakutumia mwili wangu nilijaribu kumzuia asiinuke pale chini.

“ ahaha..ahaha….” Alicheka . Kwake ilikuwa kama mzaha. Nikiwa nimemkandamiza chini, maziwa yangu yalimgusa usoni.

“ ahaha..ahaha…” Alicheka na kuanza kuyalamba. Niliyakwepesha na kumng’ata mkono. Nilimngata kwa nguvu bila kumuachia.

“aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah! …aaaaaaaaaaaaaaaaaaa.” Alipiga kelele. Aliokota kipande cha jiwe na kunipiga nacho kichwani. Niliona nyota nyota, Kama mzigo nilianguka chini na kupoteza fahamu.

………………………………….

Nilizinduka na kujikuta nipo chumba tofauti, pembeni yangu alikuwa amelala Hans. Alikuwa amepasuka kwenye paji la uso, Damu zilikuwa zikimtoka.

“ Unajifanya jeuri wakati kuzimia haukawaii.” Aliniambia Baba Hans.

“ Nilikuwa nakusubiri uzinduke tuendelee na kazi yetu.”  

Moyo wangu ulikufa ganzi, mwili haukuwa na nguvu. Nilijiuliza maswali yasiyokuwa na majibu. Nilimuangalia Hans pembeni yangu, alikuwa hatamaniki, damu nyingi zilimtoka. Alipigwa na chuma kichwani. 

Nilikata tamaa kabisa, sikuona sababu ya kuendelea kupambana naye.

“ Acha afanye atakavyo, hakuna chochote nitakachofanya ambacho kitamzuia kutimiza azma yake.” Niliwaza.

Nilikaa kidhaifu na kumpa uhuru baba Hans afanye atakacho.

Naye bila ajizi, alinishika miguu na kuitanua. Alijiweka sawa .

“ Ahsante sana, hivi ndivyo inavyotakiwa. Kwakuwa umekuwa mstaarabu nitakufanya kwa ustaarabu . Kwanza haitakuwa kama nakubaka.” Aliniambia. Alianza kuzilamba sehemu mbali mbali za mwili wangu. Alinilamba na kunipapasa kila kona.Bila kinyaa bila aibu alizilamba hadi damu zangu za hedhi.

“ kwa ajili yako nipo tayari kwa lolote, zawadi unayonipa leo ni kubwa sana. Sipaswi kuichukulia kimzaa mzaaa.” Aliniambia huku akiendelea kunilamba.

“ Nazani sasa mwili wako umepata joto, ni wakati muafaka wa kufanya jambo letu.” Aliniambia. Aliniinua miguu juuu na kutaka kuniingia, kabla hajafanikiwa nyuma yake alitokea Martini , alikuwa akinyata, mkononi alikuwa ameshika kipande cha gogo.

Baba Hans alihisi kitu, haraka aliniacha na kugeuka nyuma, ile anageuka tu,alipigwa usoni na kipande cha mti, pale pale kama mzigo alianguka chini. Alitulia tuli.

“ Shenzi sana huyu….” Aliongea Martini. Alinishika mkono na kuninyanyua.

“ Pole sana mke wangu.” Aliniambia.

Kitendo cha kuniita mke wake kilinishtua, kilitoa ishara ya hatari zaidi.

“ Ahsante sana..nashukuru..nashukuru sana…” Nilimwambia huku nikitafuta nguo zangu nijisitiri. Pembeni ya chumba nilikiiona kipanda cha nguo, nilikifata na kukichukua, haraka nilizifunika sehemu zangu za siri.

Nikiwa najifunika , Martini aliniangalia kwa macho ambayo sikuyaelewa maana yake. Ni kama alikuwa na uchu. Kwenye koromeo lake niliona akimeza mate. Alipiga hatua kunisogelea nilipokuwa.

“ Hapana,,usinifateeee…usinifateeeee…niacheeee…” Nilimpa tahadhari.

Nikama nilikuwa nampiga mbuzi gitaaa, alinisogelea na kunikamata kwa nguvu. Aliniangusha chini na kunitoa kile kipande cha nguo. Nilibaki mtupu . Alinishika miguu kwa nguvu na kuitanua.

“ aaaaa……” Nilipiga kelele. Aliniziba mdomo kwa nguvu.

“ Tulia..” Aliniambia.

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.