SIMULIZI ZA JOSHUA / 8 months ago

JIJI LA KICHAWI
0713111547 whatsapp
``ok mpenzi wangu’’
``USIJE UKALOGWA UKAFANYA MAPENZI NA MWANAMKE MWINGINE POPOTE PALE SASA NYOOSHA MKONO WAKO’’
Msichana Yule wa kipepo alinyoosha mkono na kumvisha isaya pete ya kichawi ,pete isiyoonekana ‘’
Isaya hakuwa na kipingamizi alivaa pete ile ndani ya dakika moja binti Yule alitoweka
Isaya alijiketia chini na kuanza kulia .,alilia sana huku akijisemea
``bora ningemsikiliza sharifu balaa gani limenikuta daaaaah’’
Isaya hakuweza kulala tena alibaki macho mpaka asubuhi ilipofika asubuhi simu yake iliita
Alipoitizama aliona namba ya sharifu
``we mzee acha bata hujatosheka njoo chukua gari ‘’
``nakuja mzee baba ,nakuja sasa hivi’’
``ok’’
Isaya alijikongoja na kuanza kuondoka kuelekea kazini
Kazi ilianza isaya aliendelea kufanya ruti zake akiwa na daladala ,sharifu alikuwa akimtazama isaya tu toka asubuhi mpaka mchana ule ,hakuelewa hali ya mwenzake ,isaya alikuwa amenyongonyea sana akionekana kama mtu mwenye mawazo mengi,sharifu alivunja ukimya na kumuuliza mwenzake
``hey mzee leo kuna nini au kahaba kakuchosha kama hujazoea mapigo bob lazima u blow’’
``wapi mwanangu hamna ‘’
``nini shida sasa kama tatizo siyo hilo’’
``usijali mzee niko poa sana’’
Sharifu alipomwona isaya anakwepesha mada ,aliamua kumwachilia tu ila kiukweli hali ya isaya ila mshangaza sana …
Ilipofika jioni isaya alirudisha gari ,kisha alijipanga kurudi katika chumba chake alichopanga ,isaya alikuwa anawaza sana kurudi geto kwani vituko alivyokuwa akiviona kila siku vilikuwa vinamtesa sana na kumtisha
Isaya alifika mlangoni na kufungua mlango wake akiwa na hofu kubwa sana ,aliingia ndani na kuwasha redio yake kisha alielekea bafuni kuoga ,baada ya kuoga alijitupa ndani na kuanza kulala
Isaya alimwomba Mungu siku hiyo amwepushe na vioja ,kila siku toka afike pale hajawahi kulala bila usumbufu ,
Isaya alishangazwa sana na siku hiyo hakuamini kama imefika asubuhi bila ya chochote kibaya kutokea, isaya aliamka asubuhi na kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake ,alielekea kazini akiwa na furaha sana
Alipofika tu alikutana na sharifu ameshatia kambi
```oi oi oi oi niaje mzee baba’’
``vipi wewe mbona raha sana man’’
``raha lazima mkuu’’
Walichukua gari na tayari kuingizana mjini
Isaya alipofika stendi dada mmoja alimjia dirishani akiwa amebeba karanga na maandazi
``karanga karanga kaka chukua ‘’
Isaya alinunua karanga huku akimtazama binti huyo kwa matamanio makubwa sana
Binti Yule alikuwa mrembo na mwenye kuvutia sana ,isaya alijikuta akimwambia binti yule
``samahani dada jina lako nani’’
``naitwa ashura kaka yangu ‘’
``ohoooo ashura waweza ingia ndani ya gari tuongee’’
``sawa kaka usijali ‘’
Bila kipingamizi ashura alijepenyeza siti ya mbele alipo dereva
JE NINI KITAENDELEAAAAAAA