******#QUEEN_OF_DARKNESS******
****#WITH_QUEEN_NIRMARY***
**** 04 ****
Aisee Ngoma bado yaendelea kurindima taratiiibu na kukufanya wewe mpenzi msomaji usiishiwe hamu ya kuisoma hii story na ukitamani isiishe kabisa 😀😀😀😀. Kipande hiki kinaanzia upande wa baharini baada ya mwanamke yule kujifungua mtoto wa kike kasri lote lilifurahi kusikia hivyo kwani inasemekana. Mfalme wa kasri Hilo alifariki muda mreeefu Sana na kumuacha mkewe akiwa ni mjamzito na kwasasa ameshaa jifungua kijana wa kiume na hatakiwi kutawazwa kuwa mfalme mpaka pale atakapo mpata mwanamke ambae kwa hapo baadae atakuja kuwa malkia wake yaani mke wake mtarajiwa.
Sijui tumeelewana mpenzi msomaji!!? Naomba utulize akili ili kupata uhondo wa story hii kwa uzuuri zaidi. Sasa Baada ya mwanamke huyo kujifungua mtoto wa kike. Mama wa yake 🤴 ambae kwa Sasa anatarajia kutangazwa mfalme alimpenda na kusema huyo mtoto ndie atakae kuwa malkia wa hapo mbeleni.
Basi taratibu zilianza kufanywa na mtoto yule alihamia kwenye kasri la mama wa prince... Siku hiyo hiyo prince huyo aliyekuwa na umri wa miaka mwili kwa wakati huo alitawazwa na kuwa mfalme ilhali akiwa na umri mdogo Sana. Huku nako haka katoto kalicho zaliwa siku hiyo kalipewa upako wa kuwa malkia kwa siku zijazo huko mbele.
Kasri zima la baharini lilifurahi kupata mfalme kwani kwa miaka mingi walikuwa wakiongozwa na malkia mstaafu ambae mume wake alifariki muda mreeefu ulio pita.
Duuuuuuuh hatari tukirudi huku nchi kavu mwanamama huyo aliwahishwa hospital na kuanza kupewa matibabu. Hali yake haikuwa mbaya Sana hivyo alipewa vidonge na kuandikiwa tarehe ya kurudi Tena duniani kuangalia vizuri afya ya mtoto wake na yeye mwenyewe. Bado akili yake na mawazo yake yote. Alijua yule ndo mumewe masikini kumbe mumewe alishaa fariki kabla hata yeye hajajifungua. Na ajuza yule aliendelea kuuvaa uhusika wa marehemu mume halali wa mama huyo. Mwanamama wa nchi kavu kwa jina halisi aliitwa MONALISA na mwanae aliitwa TRACE
#INAENDELEA....