QUEEN_OF_DARKNESS
****#WITH_QUEEN_NIRMARY***
******* 01*******
Eeeeh bwana eeeeehh hatari Kwanza kabisa nikupongeze wewe ulie weza kukichagua kigongo hiki kikali kiendacho kwa jina AMAZING hapo juu. Natumai Kila mmoja anashauku ya kutaka kujua ndani ya story hii Kuna vitu gani au ndani ya story hii Kuna funzo gani!?
Twende sambamba usikose kufuatilia kipande kimoja badala ya kingine. Na endapo ukikosa kipande kimoja tuu kwenye hii story aisee utajilaum maana sio kwa Moto huu 🔥🔥 🔥🔥 🔥 nimeuwasha nao umewaka. Big up Sana kwa wewe usomae story hii. Sasa Anza nayo ukamuadithie best yako.
Ni katikati ya jiji la DAR ES SALAAM sehemu fulani hivi yenye utulivu wa hali ya juu iitwayo posta.
Usiku wa manane wakazi wa eneo Hilo wakiwa wamelala. Ghafla milio ya kunguru wakali wenye njaa ya ajabu walikuwa wakilia na kuendelea kuelea angani kwa kutanua mbawa zao. Milio hiyo iliambatana sambamba na mpasuko mkali wa radi ulio pasua anga na kutokea ardhini. Mlio huo ulitoboa Ngoma za Kila mkazi wa eneo Hilo kwenye sikio lake.... Mwanamama mmoja aliyekuwa na ujauzito wa miezi Tisa alistuka huku jasho likiwa linamtiririka na kuanza kuomba kwa woga.
"Jesus crust"
"Vipi mke wangu!!? Hebu pumzika unaona Hali imechafuka wewe unataka kuomba hata Mungu anaona hali uliyo nayo hivyo atatulinda tuu"
Mumewe alimzuia kwa kumlaza kitandani. Akiwa anataka kulala ghafla uchungu ulianza kumuuma na kupiga kelele.
Tukirudi upande wa baharini mawimbi yalikuwa yakienda na kurudi bahari ilichafuka kwa balaa lililo kuwa likiendelea. Inasemekana Kuna mwanamama chini ya bahari nae alikuwa akiugulia uchungu wa kutaka kujifungua.
Alafu Hawa watu wa baharini wanaonekana sio binadam wa kawaida yaani ni majini. Unaona mambo hayo mpenzi msomaji!?
Basi unaambiwa nchi kavu ambako wanaishi watu wa kawaida mfano Mimi na wewe palikuwa Ni hatari vivyo hivyo baharini Napo mambo yalikuwa si shwari.. Eeeh bhana eeh
😃😃😃😃😃 Huu Ni mwanzo tuu Tukutane sehemu ya pili my dear.
#INAENDELEA..