Njia ambayo wengi tumejifunza kuweka malengo imekuwa inatupoteza na
ndiyo maana wengi wamekuwa wanaweka malengo lakini hawayafikii.
Njia tuliyozoea kuweka malengo ni kuanza na lengo tunalotaka kufikia,
kuchukua hatua za kulifikia, kupata matokeo na kisha kupata hisia baada ya kuwa na matokeo ya lengo hilo.
Njia hii imekuwa siyo sahihi kwa sababu sisi binadamu ni viumbe wa kihisia, tunasukumwa zaidi na hisia kuliko kitu kingine.
Na njia hiyo tunayotumia inaweka hisia mwisho, baada ya kupata
matokeo, kitu ambacho ni kigumu.
Njia sahihi ya kuweka malengo ambayo utayafikia ni kuanza na hisia kwanza, zile hisia ambazo unataka kuwa nazo baada ya kufikia lengo, ndiyo unaanza nazo kabla hata hujafikia lengo.
Ukishakuwa na hisia hizo, unaangalia ni
matokeo gani unayotaka kuzalisha, na hatua zipi unazopaswa kuchukua ili kuzalisha matokeo hayo.
Kwa kuanza na hisia, matokeo na kisha kuchukua hatua, moja kwa moja unafikia lengo lako.
