Notification texts go here Contact Us Buy Now!

JINSI YA KUPIKA BIRIANI



Mahitaji ya kupika Biriani

1.Mchele wa Basmat 1/2 Kg

2.Nyama ya Mbuzi Stake 1/2 Kg

3.Viazi mbatata vikubwa 1/4Kg 

4.Vitunguu maji 1/2 Kg 

5.Nyanya Kubwa 4

6.Nyanya ya Paket 1

7.Biriani Masala 1/2 Kijiko cha chakula 

8.Viungo vya pilau 1/2 Kijiko 

9.Sukari 1/2 Kijiko 

10.Chumvi kiasi 

11.Mtindi 1/2 Kikombe 

12.Vinegar au Ndimu 

13.Kitunguu thomu kilotwangwa Kijiko cha chai 

14.Tangawizi iliotwangwa kijiko cha chai 

15.Karot ilioparwa 1

16.Pilipili hoho iliokatwa 1

17.Mafuta ya kupikia 1/2 Lita

18.Rangi nyekundu 

19.Maji Kiasi 

20.Curry Powder 


Maandalizi ya kupika Biriani

1.Osha mchele na uroweke kwa robo saa

2.Kata kata nyama osha weka tangawizi, chumvi, curry powder na kitunguu thomu

3.Menya vitunguu osha na katakata weka pembeni 

4.Menya viazi osha weka rangi vipete vizuri 

5.Saga nyanya au zipare 


Jinsi ya kupika Rosti la Biriani 

1.Weka nyama acha ikauke kidogo kisha weka maji taratibu mpaka iive iwe laini sana 

2.Weka mafuta kwenye karai yakipata moto vizuri weka vitunguu maji vikaange mpaka viwe na rangi ya dhahabu 

3.Toa vitunguu weka viazi mbatata kisha vikaange kidogo na uvitoe 

4.Weka sufuria na mafuta kidogo uliokaangia vitunguu 

5.Yakipata moto mimina karoti kaanga kidogo 

6.Weka pilipili hoho kaanga kidogo 

7.Malizia kuweka kitunguu thomu 

8.Kisha mimina nyanya, chumvi kidogo na viazi acha vichemke kama dakika 3

9.Mimina nyama na supu yake acha kwa dakika kadhaa 

10.Weka nyanya ya Paket, vinegar na mtindi acha vichemke

11.Weka viungo vya pilau, biriani Masala na sukari koroga acha ichemke kidogo 

12.Malizia kuweka vitunguu ulivyo vikaanga 

13.Acha dakika 3 epua rosti lako acha lipoe


Jinsi ya kupika Wali wa Biriani 

1.Weka maji kwenye sufuria na chumvi 

2.Yakichemka weka mchele wako mpaka uive 

3.Nyunyizia mafuta na rangi nyekundu kwenye wali wako ufunike acha ukauke


Jinsi ya Kupakua Biriani

1.Changanya wali vizuri ili rangi ichanganyike na wali vizuri 

2.Chukua rosti la biriani vijiko vitano weka kwenye wali wako changanya vizuri 

3.Pakua wali kwenye sahani 

4.Koroga rosti vizuri pakua na weka katikati ya sahani 

5.Tayari kwa kula.```

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.