Mimi ni kijana wa miaka 28 nimeoa na ndoa yangu ina miaka miw3ili sasa hivi, mimi na mke wangu tuko vizuri lakini shida nikuwa, Baba mkwe wangu ni kama hampendi mke wangu, shida kubwa ni hivi, Baba mkwe wangu anaa pes atena nyingi tu lakini hamshirikishi mke wangu kwa chochote kile. Wakati namuoa mke wangu tulipewa nyumba ambayo ndiyo tunaishi mpaka sasa, lakini pia mke wangu alikua na gari alilokua anatumia kipindi hicho ni la Baba yake na tunalitumia mpaka sasa.
Mke wangu mimi alikua anafanya kazi lakini kwakua ilikua mkoani nikamuambia aache kazi, alimuambia Baba yake akamapa mtaji wa milioni 15 akaanzisha Biashara lakini kwa bahati mbaya ile biahsara ilikufa. Sasa baada ya hapo Baba mkwe ni kama katussa, yaani hatushirikishwi kwa chochote, mke wangu ni wale watu wapole, hawezi kuongea wala kupigania haki zake.
Kinachotokea nikuwa ndugu zake wengine ndiyo wanafaidi, kaka zake wanashiriki katika Biashara za Baba yao, wanajenga majumba lakini mke wangu ukimuambia kuwa muambie Baba yako akupe gao wako hataki. Wasiwasi wangu nikuwa Baba yake akifa mke wangu anaweza asipate kitu, yaani nashindwa hata chakufanya, nimeongea na mke wangu mpaka nimechoka, nilikua anaomba uongee naye ili ajiongeze kwani mimis iwezi kumhudumia kila kitu wakati Baba yake yupo na ana uwezo!
