MPENZI CHEUPE | WHITE LOVER.
MPENZI CHEUPE # 07 [SWAHILI].
MTUNZI: Sunday JoaquimContact: 0658 593 797
"Mh wewe si Brown wewe" aliuliza Dula " ah ndio mimi" alijibu Brown, mara Dula alimwita yule dereva tax pembeni "we bwana huyo jini" "kivipi sasa?" "huyo jamaa alikufa kitambo sana" mara Dula na yule dereva tax walianza kutimua mbio,pale kijiweni hakubaki hata dereva mmoja,wapita njia na wao waligeuza njia na kukimbia bila kujua sababu ya kukimbia.
Hali ya taharuki ilitanda pale maeneo ya Amana,habari zilisambaa maeneo ya jirani kuwa kuna jini Amana,watu walifurika maeneo ya jirani ili kumuona jini, wengi walipatwa na sintofahamu kwa kumuona jini aliyevaa shuka nyeupe tena zenye chapa ya bohari la madawa msd,Polisi walifika eneo la tukio, walimkuta Brown amekaa chini ame egemea masanduku ya barua " wewe ulitoroka hospitali?" aliuliza mmoja wa wale Polisi,Brown hakujibu kitu,Polisi walimwinua wakampakia kwenye gari na kuondoka naye na kuwaacha watu wakiongea maneno mengi yakiwamo maswali yasiyo na majibu.
Brown alifikishwa kituoni akiwa mwenye mawazo sana, alishindwa kuelewa wale madereva tax walivyodai alikufa wakati yeye anaona kuwa aliondoka kama siku tatu zilizopita,polisi walianza kumhoji lakini Brown alipotaka kueleza Salma alimtokea huku akiwa ameweka kidole cha shahada mdomoni kama ishara ya kumtaka asiseme chochote ,Brown alizidi kuchanganyikiwa,alianza kupatwa hasira, maisha aliyaona machungu.
Polisi walizidi kumwuliza maswali, lakini Brown alikuwa kimya hakuongea neno zaidi ya kutokwa machozi,Polisi walishindwa kumwelewa Brown, walikubaliana wamwache kwanza atulize mawazo kwanza.Baada ya kama saa mbili kupita,pale kituoni alikuja mkuu wa kituo " haya huyu vipi na mashuka yake" " afande huyu ni yule aliyeokotwa jana pale kando ya barabara ya uhuru" "sasa mbona yupo hapa?" "Afande amezua taharuki wananchi wanahisi ni jini" " jini? yaani huyu jini?" "Ndio afande " " jini gani ana nyusi anapepesa macho?" "Afande yaani watu wakimuona wanaweza kuumia au kumpiga hawana imani naye kabisa" "haya tufanyeje sasa?" "Afande....afande afande...." aliongea yule askari bila kumaliza kauli,aliona kitu cheusi angani,upepo mkali sana ulivuma, upepo ulitua mbele ya kituo Brown own own own own wn" sauti ilisikika kutoka katikati ya ule upepo,Polisi wote wapatwa na taharuki, wenye imani zao potofu bado kidogo kuzimia,iliwalazimu kumtoa nje Brown, upepo ukamzunguka Brown, ulizunguka kwa muda kama dakika moja, alafu upepo ulitoweka kwa kupanda juu sana angani,Brown alitoweka kwenye mazingira ya kutatanisha,baadhi ya askari waliogopa na waliamini Brown ni jini, habari zikasambaa, magazeti yakaandika habari za Brown.
Brown alijikuta katikati ya kundi kubwa sana la watu, walikuwa wamevalia kaniki nyeusi, weusi sana kama vile walipaka masizi,mapigo ya moyo wa Brown yaliongezeka, hakuwa akiwafahamu hata mmoja,mara alitokea mwanamke mmoja ameshika usinga mkononi "Brown pendapenda leo upo kwenye mikono yetu haaaaa haaaa " aliongea yule mama huku akimsogelea Brown, aliinua usinga wake juu ili amchape nao Brown lakini kabla hajashisha ule usinga kilisikika kishindo kikubwa sana,Salma alikuwa amefika.........ENDELEA KUSOMA SEHEMU YA 08 YA SIMULIZI HII YA MEPENZI CHEUPE.
WHITE LOVER #07 [ENGLISH VERSION].
" MH you are not brown you " asked dula " ah yes I am " replied brown, immediately dula called the driver taxi on the side " you sir that genie " " how is it now?" " that guy died a long time ago " mara dula and that taxi driver started Running the race, when the river was not left even one driver, they passed the path and they turned the path and ran away without knowing the reason to run.The State of panic went in the areas of deposit, news spread around the neighboring areas that there was a genie, people flooded nearby areas to see the genie, many were caught by seeing a genie on a white sheet with a brand of drugs, the police came to the area. On the incident, they found brown sitting down ame to silver boxes " you escaped from the hospital?" he asked one of the police, brown didn't answer anything, the police lifted him up and uploaded him to the car and left him and let people talk a lot of words when there are no answers.
Brown was reached to the station with so much thought, he failed to understand those taxi drivers claimed he died while he saw that he left like three days ago, the police started questioning him but brown when he wanted to explain salma appeared while he put a degree of degree in his mouth as a sign of asking him not to say anything, brown kept on Confused, he started getting angry, life saw bitter.
The police kept asking him questions, but brown was silent he didn't speak a word more than not tears, the police failed to understand brown, agreed to let him first take thought first. After two hours passed, when the station came to the head of the center " how is this with his sheets " " this officer is the one who was saved yesterday at the side of UHURU Road " " now why is he here?" " the officer has killed the panic citizens feel it Blood " " blood? I mean this genie?" " is the officer.... which genie has a eyebrows?" " if the officer is seeing him they can hurt or beat him, they have no faith in him?" " what should we do now?" " Officer.... Officer officer...." He spoke the policeman without finishing the statement, he saw something black in the sky, a very severe wind blew, the wind landed in front of the center brown own own own wn " the voice was heard from the middle of that wind, all the police got caught in panic, with their corrupt faith still a little bit to shut them , it was necessary to cast out brown, the wind surrounded brown, surrounded for a moment, then the wind disappeared from the sky, the brown disappeared from the sky, brown disappeared in a confusing environment, some soldiers were afraid and believed brown is a genie, the news were spread. Brown.
Brown found himself in the middle of a very big group of people, they were dressed in black cake, so black as they painted the jokes, the pulse of brown heart increased, he didn't know them even one, immediately one woman caught don't go in hand " Brown I love today you are in our hands haaaaa Haaaa " she spoke to the woman while swimming brown, she raised her head up so that she could beat her brown but before she finished the one that was a big bang, salma had arrived......... Salma had arrived......CONTINUE TO READ WHITE LOVER NARRATIVE PART 08.
