MPENZI CHEUPE | WHITE LOVER.
MPENZI CHEUPE # 06 [SWAHILI].
MTUNZI: Sunday JoaquimContact : 0658 593 797
Alimuona kiumbe wa kutisha sana,wale wote waliokuwa pale hawakuwa wwanatisha kama huyo,yule kiumbe alimwangalia Brown kwa jicho kali sana kiasi cha kumfanya Brown aishiwe pumzi na kutaka kuzimia,Salma alichukuwa kipande kingine cha nyama ya binadamu na kumsogelea Brown,alimpelekea mdomoni,Brown hakuwa na namna zaidi ya kufungua mdomo,aliwekewa kipande cha nyama,alifumba macho,akataka kutapika lakini alijizuia "ooogggghhhh" alianza kutafuna akiwa mwenye kinyaa sana,alipomeza tu,shangwe za kijini ziliitawala eneo lile "sasa mpenzi umefaulu mtihani mkubwa njoo univike pete" Brown alisogea.mdomo wake ukiwa umelowa damu na michirizi mingine kwenye shati lake.
Brown alipokea pete toka kwenye mkebe maalumu mwekundu,alikuwa inawaka sana,dhahabu safi,aliishika mkononi na kuitumbikiza kwenye kidole cha Salma,na Salma alichukuwa pete yenye kito chekundu katikati na kumvisha Brown,ndipo yule kiumbe wa kutisha alimshika mabegani,Brown alipokea nguvu za kuzimu "mmmh mmmhhhffff" aligugumia Brown,shangwe ikaongezeka,nyama na damu zikanywewa,Salma alimshika Brown kimahaba na kuelekea naye kwenye chumba chake,kilikuwa chumba kikubwa sana,kilipambwa na vito vya thamani kubwa sana,palikuwa na kitanda cha malkia,dressing table iliyojaa kila ina ya manukato,chetezo za ubani "karibu mpenzi wangu hiki ni chumba chako kuanzia sasa jisikie huru" aliongea Salma huku akipunguza nguo za Brown mwilini.
Brown alikuwa hoi kwa matukio yale,Salma alimwonyesha Brown bafu ili aoge,lakini Salma yeye hakwenda kuoga,Brown alioga,alitoka na kujifuta maji kwa taulo safi jeupe,alipomwangalia Salma,alimwona ameshika vichupa mikononi mwake "ukimaliza sogea hapa nikupe maelekezo" aliongea Salma,Brown alisogea "nakusikiliza mpenzi wangu" alijibu Brown "sasa hapa pana miiko mitatu lazima uchague mwiko mmoja utakaoutekeleza maisha yako yote" "miiko gani mimi siwezi mambo hayo" "sikiliza Brown wewe umeshakuwa mume wangu na nilipokuwa duniani sikuwahi kuolewa hii ni ndoa yangu ya kwanza,kwa hiyo nataka nikupe mali ili usiteseke na maisha" "sawa lakini isjie ikawa kuuwa mtu sijui kutoa kafara mimi siwezi kabisa hayo mambo" "hapana wala si hayo haya ni rahisi tu" "sawa".
Salma alitabasamu "sawa sasa mwiko wa kwanza iwe marufuku maisha yako yote kuwa na mwanamke mwingine yeyote zaidi yangu na ukiwa naye tu nitamuuwa,mwiko wa pili nikufanye upate shepu ya kike na marufuku kuona aibu wala kujifunika usionekane,mwiko wa tatu,uwe hanithi ukiwa duniani na ukija huku utakuwa mzima" "duh ! bora nisiwe na mwanamke mwingine" "umejibu vizuri sasa hii chupa ya kwanza ni dawa ya kukuza biashara,hii ya pili ni kwa ajili ya ulinzi wako na hii ya tatu ni kwa ajili ya kufungua milango ya kuzimu ili uingie huku,lakini kabla ya kuitumia hii lazima utangulize yali la kuku wa kienyeji pale kwenye mlango,ndipo utaweza kufubgua mlango umenielewa" "sawa mpenzi nimekuelewa" wakati huo Salma alikiwa kwenye umo zuri sana la mwanamke isipokuwa meno yake tu yalikuwa marefu kuliko kawaida.Brown alishamzoea.
Brown na Salma waliangaliana kwa macho ya mahaba,licha ya kuwa Brown alikuwa amechoka ilimlazimu ashughulike hata kidogo,alimsogelea Salma,alimshiki kiunoni,Salama alijilegeza na kujiachia mikononi mwa Brown,walisogelea kitanda,Salma alilalia mgongo na Brown alikuja juu yake,walipiga mechi kali sana yaani ya kibabe,kwa muda wa saa tatu Brown alikuwa hoi,alijitupa pembeni na kupitiwa usingizi mzito sana,akiwa usingizini aliota viumbe wa ajabu wengi walikuwa wakimfurahia jambo liliomshangaza,alikuwa akiwaogopa kwasababu walikuwa wanatisha sana,kwa mbali alianza kusikia sauti "ee bwana ni mwanaume lakini bado anapumua njoo haraka tumsaidie" ziliambatana na kelele za watu wengine wengi "eehana nguo bwana sijui alikuwa anwanga wapi?" "itakuwa kachelewa kurudi" "wenzake walimwacha" "aliishiwa mafuta huyu" kila mtu alisema lake kwa waliokuwa eneo la tukio.
Brown alikutwa amelala kando ya barabara ya uhuru alfajiri,alikuwa hana nguo hata moja na alikuwa na masizi mwili mzima,aliokotwa na wasamalia wema,walimpeleka polisi,alihojiwa lakini hakuweza kueleza chochote,polisi waliamua kumpeleka Hopsitali ya Amana,alipokelewa na kupewa kitanda,alichukuliwa vipimo,baada ya muda majibu yalitoka kuwa hakuwa na tatizo lakini cha kushangaza alikuwa kama mtu aliyelewa,walimwacha apumzike,giza lilipoingia alitoroka na kwenda nyumba aliyokuwa akiishi,aalikuwa amejifunga shuka za hospitali,alipofika kwake alipotea,alikuta kuna ghorofa jipya limejengwa,alijiuliza kuwa ni pale au pengine maana palikuwa na nyumba ya kawaida tu sasa anaona ghorofa,alienda mpaka kwenye duka moja liliokuwa mtaani kwake alikuta muuzaji si yule anayemfahamu.
Aliamua kuuliza vijana waliokuwa wamesimama pembeni ya lile duka "za saa hizi jamani samahani naulizia nyumbani kwa Brown" :hapana hatumfahamu" alizidi kuchanganyikiwa "Brown aliyekuwa anaishi nyumba ile" aliongea Brown huku akionyesha kwa kidole pale ilipokuwa nyumba aliyokuwa anaishi "pale sisi tumelikuta hilo ghorofa" duh ! ilikuwa vigumu Brown kuamini anachosikia,alianza kuondoka taratibu bila kujua anapoelekea,alifika maeneo ya Amana posta,aliketi chini na kutafakaria,aliamua kumfuata mooja wa madereva tax waliokuwa wakipaki pale Amana "za saa hizi samahani naulizia nyumbani kwa Brown" alikuwa akiuliza hivyo kwa lengo la kuona kama watu watamkumbuka au watampa taarifa zozote muhimu kumhusu yeye "dah mimi brown simfahamu ila niliwahi kusikia stori kitamb sana,alikuwa anaishi mtaa huo lakini sijiu alikufa sijui ndugu zake walimtoa kafara wakauza nyumba yaani sina uhakika....kwani upoje naye wewe?"
"mimi ni ndugu yake nimekuja toka mkoani nikakutana na wahuni wakanivua nguo na kunichukulia kila kitu" aliongopa Brown ili apate msaada wa nguo "duh ! kweli Dar es salaam noma sasa hebu subiri kwanza.... oya Dula njoo mara moja" dereva tax aliita dereva tax mwingine "hebu msikilize huyu jamaa kwanza" "jamaa gani?" "si huyu hapa humuoni au?" "mh ! wewe si...................ENDELEA KUSOMA SIMULIZI HII YA MPENZI CHEUPE SEHEMU YA 07.
WHITE LOVER #06 [ENGLISH VERSION].
She saw a very horrible creature, all those who were there were not scary like that, the creature looked brown with a very severe eye to make brown breath and wanted to kill them, salma took another piece of human flesh and swim brown, headed to her mouth, he was not brown. And more than opening his mouth, he was set a piece of meat, closed his eyes, wanted to cook but he stopped " Ooogggghhhh " she started chewing when he was very fat, when he swallowed up, the engine cheers took the place " now my love has passed on the big test " . Her mouth with blood and other games in her shirt.Brown received a ring from a special red branch, it was very lit, Pure Gold, caught it in his hand and threw it on salma's finger, and salma took a ring with a red masterpiece in the middle and dressed brown, then the terrible creature caught him in the breasts, he received the power of hell. "hmm mmmhhhffff" she hugged brown, cheers increased, meat and blood blood, salma caught brown romantic and towards her in her room, it was a very big room, it was decorated with very precious stones, there was a queen's bed, there was a queen's bed full of every table. Ya Spices, perfumes of incense "welcome my love. This is your room from now on feel free" she spoke salma while reducing brown clothes in the body.
Brown was helpless in those events, salma showed him brown bathroom to aoge, but salma she didn't go to bath, brown took a bath, came out and wiped himself water in a clean white towel, when she looked at salma, she saw him holding bottles in her hands "when you finish her, I spoke to you" Brown moved " I'm listening to you my darling " replied brown " now here are three months you have to choose one taboo that you will apply to your whole life " " listen to brown you have already been my husband and when I was on earth I never got married. This is my first marriage. , so i want to give you wealth so that you don't suffer with life " " ok but come it became to kill someone I don't know how to sacrifice. I cannot completely do that things " " " no and not that. These are just simple " " ok ".
Salma smiled " ok now the first taboo should be forbidden all your life to have any other woman other than me and if you have only her I will kill her, second taboo I make you get a shape of a female shape and forbidden to see shame nor cover yourself don't look, third taboo, be hanithi when you are on earth And if you come here you will be fine " " duh! As long as I don't have any other woman " " you have answered well now this first bottle is medicine to grow business, this second is for your protection and this third is for opening the doors of hell so that you can enter here, but before using this You have to put the traditional chicken chicken at the door, then you will be able to open the door you understand me "okay darling I understood you" at that time salma was in the most beautiful appearance of a woman except her teeth were longer than usual. Brown was already used to it
Brown and salma looked at each other in the eyes of affection, despite that brown was tired he had to handle it at all, she swim salma, took him on the foot, safely she washed himself and released himself in the hands of brown, they moved the bed, salma came back and took a great match on him. He mean, for three hours, brown was helpless, threw himself on the side and fell asleep, while in sleep he dreamed many amazing creatures were enjoying him, he was scared of them because they were so scary, by far he started hearing the voice " Oh Lord, he is a man. But he is still breathing come quickly let's help him " accompanied by many other people " eehana clothes Lord I don't know where he was started?" " it will be late to come back?" " his colleagues left him " " he was fed up " everyone said to those who were at the scene.
Brown was found lying beside UHURU's road dawn, he had no clothes and had a cover of the whole body, he was picked up by good men, they took him to the police, interviewed but could not explain anything, the police decided to take him to the deposit of deposit, when he received and given a bed, he was taken tests , after a while the answers came out that he had no problem but shocking he was like a man who was raised, they let him rest, when darkness entered and ran away and went to the house where he was living, when he came to him he lost, he found a new apartment built, he asked himself that it was Or probably because there was just a normal house now seeing an apartment, he went to a shop that was in his neighborhood and found a seller not aware of him.
He decided to ask the young men who were standing beside the shop " for now I am sorry I'm asking for the brown house ": no we don't know him " he kept confused " Brown who was living in that house " spoke brown while showing off his finger when it was the house where he was living " when we found that apartment " Whoa! It was hard brown to believe what he hears, he started leaving slowly without knowing where he was heading, he reached the deposit places, he sat down and looked, decided to follow the moods of taxi drivers who were at the deposit "of these hours sorry I ask for the brown home" he was asking so for the purpose of the To see if people will remember him or they will give him any important information about him " dah I brown I don't know him but I ever heard stories very well, he was living in that street but I don't know his brothers sacrificed him and sold the house I mean I don't know....
" I am his brother, I have come from the province and I met the wooden ones who opened my clothes and took me everything " who feared brown to get help of clothes " duh! Truly Dar es salaam is crazy now, let's wait first.... hey dula come once " a taxi driver called another taxi driver " just listen to this guy first " " which guy?" " isn't this one here you don't see him or?" " MH! You are not.........CONTINUE TO READ PART 07 OF WHITE LOVER NARRATIVE.
