MPENZI CHEUPE | WHITE LOVER.
MPENZI CHEUPE # 01 [SWAHILI].
MTUNZI: Sunday JoaquimContact : 0658 593 797
Saa nne za usiku kituo cha mabasi Kongo jijini Dar es salaam,upepo mkali ukivuma,wingu jeusi likiwa limtanda angani,kibaridi cha wastani kinapuliza,Brown akiwa amesimama kusubiri usafiri mara linasimama basi anashuka msichana mrembo,mweupe sana,mrefu,mwenye kunukia vizuri,anamvutia Brown,kabla hajafanya chochote mvua kubwa ya ghafla inashuka na kuwalazimisha abiria walikuwa kutoni kukimbilia chini ya baraza la ghorofa lililopo nyuma ya kituo.
Brown alijikuta yupo karibu na mrembo yule aliyeshuka kwenye Basi muda mfupi uliopita "hii mvua inataka kuharibu starehe za watu" Brown alijisemesha,mrembo alionekana kutoelewa alichozungumza Brown,alitabasamu na kumsogelea "unasema?" aliuliza mrembo "hii mvua inataka kuharibu starehe za watu" " ni kweli kabisa nilikuwa nawaza nikilowa naingiaje Billcanas" "oh na mimi naelekea huko....unaonaje tuchukuwe tax?" "sawa itakuwa vizuri maana hii hali ya hewa na muda huu usafiri mgumu itakuwa tabu".Brown aliita tax iliyokuwa inapita walipanda na kuelekea Club Billcanas.
Walifika Billcanas,Brown alilipa kiingilio wakaingia,wakiwa ndani "samahani unaitwa nani?" aliuliza mrembo "naitwa Brown" alijibu huku akinywa funda moja la kinywaji chake "okay vizuri nafurahi kukufahamu" "na wewe unaitwa nani?" "Salma... lakini maarufu Cheupe au ukipenda yote mawili Salma Cheupe ni sawa pia" "anhaa nimefurahi pia kukufahamu" waliendelea kucheza na kufurahi,hakika walipendezana sana,watu wengi ndani ya club walikuwa wakiwaangalia sana kwasababu Brown na yeye alikuwa mtanashati sana.
Hisia za mapenzi ziliibuka na kupiga kambi kwenye mioyo yao wote wawili,muda wote Salma alikuwa akitabasamu,Brown alimuona Salma anafaa kuwa mpenzi wake "unaishi wapi?" "mmh! naishi Kariakoo mtaa wa Mission Kota.... na wewe?" naishi ilala Shariff Shamba karibu na hospitali ya Amana" "sawa" "samahani umeolewa?" " mh! ningeolewa ningekuwa huku saa hizi? hapana sijaolewa hata mchumba sina" " haiwezekani huna mchumba uzuri wote huu?" aliongea Brown kwa mshangao mkubwa sana "kweli sijaolewa nipo alone ndio maana huwa nakuja huku kujifariji" "mh haya...mimi naomba tuwe tunakuja wote" "sawa hapana tabu nitashukuru" walikubaliana na kuendlea kuponda starehe.
Muda wa saa kumi alfajiri walitoka club ,Brown alichukuwa tax ili kurudi nyumbani,walikaa siti ya nyuma,baada ya tax kuanza kuondoka Salma alilalamika anahisi baridikutokana na upepo wa alfajiri,Brown alivua koti lake na kumvisha Salma "ahsante mpenzi wangu" alishukuru Salma maneno yaliyoshtua moyo wa Brown "usijali nakupenda sana nipo tayari kukulinda na chochote" "ahsante nami nakupenda pia" Brown alimchumu Salma shavuni "mmh ahsante na wewe mwaaah" Salma alirudisha lile busu,Bown alimkumbatia Salma na Salma aliegemeza kichwa chake kifuani mwa Brown.
Walifika mtaa wa Mission Kota kariakoo,Brown alishuka ili aagane na Salma "sasa mpenzi ?" aliuliza Brown "yaani unataka uishie nje? hapana bwana tafadhali ingia hata uone chuba changu" aliongea Salma huku akimvuta Brown mkono "hapana nitakuja kesho saa hizi muda umeenda sana" "unadhani nani atakuona hakuna aliye macho wote wamelala fofofo" mwanamke ana nguvu sana Brown alishindwa kuendelea kukataa,alijikuta akiingia ndani ya nyumba ya kina Salma "karibu sana hiki ni chumba changu jisikie huru wakati wowote karibu sana" "ahsante nitakaribia Mungu akipenda" Salma alifungua kabati lake na kutoa mkufu wa dhahabu,alimkabidhi Brown.
"hii cheni nakupa kama ishara ya upendo wangu kwako" aliongea Salma "ahsante sana nashukuru" Brown aliinuka na kumkumbatia Salma "utakuja lini tena ili nikupikie tule wote na ndugu zangu wakujue" "kesho jioni nitakuja" "sawa karibu sana" walitoka chumbani Salma alimsindikiza Brown mpaka kwenye tax "haya usisahau koti lako" aliongea Salma huku akilivua "hapana hapana na mimi hilo ni ishara ya upendo wangu kwako" "eh asante jamani" waliagana Brown aliondoka.
Wakiwa njiani kuelekea Ilala dereva tax alikuwa na neno la kusema "mwanangu lakini mbona kama.............................ENDELEA KUSOMA SEHEMU YA PILI YA SIMULIZI YA WHITE LOVER.
WHITE LOVER #01 [ENGLISH VERSION].
At pm the congolese bus station in dar es salaam, a fierce wind blowing, a black cloud blowing in the sky, average cold blowing, brown standing up waiting for transport immediately stands down then she goes down a beautiful girl, very white, tall, beautiful, attractive. Brown, before he does anything heavy rain comes down and forcing passengers were not rush down under the apartment council located behind the center.Brown found himself near the beautiful one who came down on the bus a short while ago " this rain wants to destroy people's comfort " Brown said, beautiful she seemed not to understand what he spoke brown, smiled and swim " you say?" she asked beautiful " this rain wants to ruin people's comfort " " it is very true that I was thinking when I was falling in billcanas " " oh and I am heading there.... how do you think we should be taken to the taxi?" " okay it will be well because this weather and this time hard transport will be a problem ". brown called the tax that was flowing they went up And heading to club billcanas
They came to billcanas, brown paid the entrance and entered, while they were inside " sorry who are you called?" she asked beautiful " my name is brown " she replied while drinking read one of his drink " okay well I'm glad to know you " " and what are you called?" " Salma... But the famous white or whether you love both salma white is the same " " I'm glad to know you " they kept playing and glad, they really loved each other, many people in the club were looking at them because brown and he was very handsome.
The feeling of love came up and camping in their hearts both of them, all the time salma was smiling, brown saw salma supposed to be her lover " where do you live?" " Mmh! I live in kariakoo the street of mission kota.... and you?" I live in ilala shariff farm near the deposit hospital " " OK " " I'm sorry you are married?" " MH! If I could get married, I would be here right now? No I am not married even a spouse I don't have " " it's impossible you don't have a spouse all this beauty?" she spoke brown with a big surprise " truly I am not married I am alone that's why I always come here to comfort myself " " okay... I pray that we all are coming " " ok no problem I will be thankful " agreed to continue to crush.
About ten o'clock in the morning they went out of the club, brown took a taxi to go back home, they stayed behind, after the taxi began to leave salma complained that he feels baridikutokana due to the dawn wind, brown took off his coat and dressed salma "thank you my love" he thanked the words that landed. Brown heart " don't worry I love you so much I am ready to protect you from anything " " thank you and I love you too " Brown alimchumu salma shavuni " mmh thank you and you kisses " salma brought back the kiss, bown and salma swallowed her head in the brown chest.
They came to mission street kota kariakoo, brown came down so that he can recognize and salma " now lover?" asked brown " I mean you want to end out? No Lord please come in and see my chula " he spoke salma while pulling brown hand " no I will come tomorrow right now the time has gone too much " " who do you think will see you no one has eyes all are asleep, " the woman is very strong brown failed to continue to refuse, she found herself entering the house Ya depth salma " you're welcome. This is my room. Feel free at any time welcome " " thank you I will approach if God wills " Salma opened her wardrobe and offered a gold necklace, she handed her brown.
" this chain I give you as a sign of my love to you " spoke salma " thank you so much I thank you " Brown arose and hugged salma " when will you come again so that I can cook all of you and my brothers to know you " " tomorrow evening I will come " " ok welcome " they came out of the room salma accompanied him Brown up to the taxi " okay don't forget your coat " spoke salma while raising it " no no and me that is a sign of my love to you " " eh thank you guys " they waliagana brown he left.
On their way to ilala driver taxi taxi had a word to say " my son but why if..........................CONTINUE TO READ PART 02 OF WHITE LOVER.
