JINSI YA KUPIKA MZINGA WA NYUKI / BEE COMB BREAD
Mapishi ya upikaji wa MZINGA WA NYUKI au kwajina lingine BEE COMB BREAD
MZINGA WA NYUKI / BEE COMB BREAD
MAHITAJI YA KUPIKA MZINGA WA NYUKI / BEE COMB BREAD:
- 🍰Unga - Vikombe 3 ½ visivyojaa
- 🍰Maziwa ya maji - Vikombe 1
- 🍰Maji - Kikombe ½
- 🍰Yai - 1
- 🍰Sukari - Vijiko 2 ½ vya supu
- 🍰Mafuta - Kikombe ½
- 🍰Hamira - Kijiko ½ cha chai
- 🍰Chumvi - robo kijiko cha chai
- 🍰Cheese ya Cream - Kiasi utakavyotumia kujaza
MAHITAJI YA SHIRA
- 🍕Sukari - Vikombe 2
- 🍕Maji - Kikombe 1 ½
- 🍕Zaafarani - nusu kijiko cha chai (iroweke)
- 🍕Ipikie shira lakini isiwe nzito.
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA MZINGA WA NYUKI / BEE COMB BREAD
- 🍬Changanya vitu vyote hivyo isipokuwa cream cheese.
- 🍬Kanda kidogo tu kulainisha unga uwe mlaini kama mfano unga wa maandazi.
- 🍬Pakaza siagi katika sinia ya round utakayopikia
- 🍬Fanya viduara vidogo vidogo na tia ndani yake cheese ya cream kwa kutumia kijiko cha chai, na vifunge viduwara vizuri na kuvipanga katika sinia bila ya kuwacha nafasi.
- 🍬Iwache ifure
- 🍬Ipikie katika oven moto wa chini kwanza katika 350 Deg, kwa muda wa baina dakika 20 na 25 .Kisha washa moto wa juu kidogo tu uwive kwa juu.
- 🍬Toa katika oven na mwagia shira kama ifuatavyo.
- 📌Kama ni shira iliyopowa basi mwagia juu ya mkate uliomoto
- 📌Kama ni shira imoto basi subiri mkate upowe.Yaani mojawapo iwe moto au baridi.