MAKARONI YA NYAMA YA KUSAGA
VIPIMO
Makaroni - 500 gm
Nyama ya Kusaga - 450 gm
Vitunguu - 2
Nyanya - 3
Nyanya kopo (Tomato Paste) - Vijiko vya supu 3
Kitunguu Thomu (Garlic) kilosagwa - Kijiko cha chai 1
Pilipili manga - Kijiko cha chai 1
Bizari ya oregano [Italian spice] - Kijiko cha chai 1
Parsely (aina ya kotmiri) - Misongo (bunches) 2
Sosi ya soya - Vijiko cha supu 2
Mafuta - Kikombe cha chai ¼
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Chemsha makaroni kama inavyoashiria paketi au hadi yaive lakini yasivurugike Chuja maji weka kando.
2. Katakata vitunguu, nyanya vipande vidogo vidogo weka kando.
4. Katakata parsley ndogo ndogo (Chopped) weka kando.
5. Weka mafuta katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi kidogo tu.
6. Tia nyama, kitunguu thomu, bizari zote endelea kukaanga hadi nyama iwive.
7. Tia nyanya pamoja na nyanya kopo, parsely, sosi ya soya endela kukaanga kidogo tu.
8. Tia makoroni changanya vizuri.
9. Pakuwa katika bakuli ikiwa tayari.