Notification texts go here Contact Us Buy Now!

BLACK AMERICA SEHEMU YA 20

RIWAYA:BLACK AMERICA
        (Mmarekani Mweusi)
MTUNZI:NELSON KIMOY
SIMU:0758638391
SIMU2:0625293917

{{ SEHEMU YA 20 }}
#Endelea_nayoo==>Baada ya dakika kumi general Brown alimwambia dereva kuwa asimamishe gari kando ya barabara kwani kwa jinsi anavyoona ramani katika laptop yake watakuwa wamefika.......
Dereva alitii wakati ambao
General aliona lacation inaposomeka jirani na wao kumbe ndo muda ambao Rocky alikuwa akitoka katika nyumba yake ambayo haikuwa mbali sana na barabara General Brown alipoangalia ramani katika laptop akachungulia dirishani mwa gari aliweza kuona usawa ambao anatokea Rocky.....
Akamtazama kwa makini alihisi mapigo ya moyo yakiwa yanadunda kutokana na furaha ya kumuona Rocky alimgeukia Jamali kisha akasema

"hey Mr Jamali yule kibaraka yule pale"

Jamali akasogea dirishani kumuona mtu huyo anayeonyeshewa...... 
Akamtathimini kisha akamgeukia General Brown

"yaani Mr Brown hicho kikaragose ndo kinakusumbulia akili yako? Kimtu chenyewe njiti hakina hata afya"

"usiseme hivyo Jamali yule sio mtu wa kumdharau yule ni jambazi sugu ooohoo"

Alisema General Brown kwa kumsisitiza Jamali kwani tayari ameona kama kamdharau asiyemjua hakumwambia tu ukweli Rocky ni mtu wa aina gani na hukumwambia Jamali yeye ni nani........
Jamali alihitimisha safari yao kwa kusema

"okay Brown hiyo kazi nitaifanya vizuri tena atakufa usiku wa kuamkia leo"

Muda wote huo wanaoongea Rocky hana hata habari alikuwa kasimama kando ya nyumba yake... 
Jamali akashuka kama mtu mwenye shida ili kwenda kumpeleleza Rocky alifika mpaka mahali alipokuwa Rocky na kumsemesha

"kwema ndugu?"
"kwema tu karibu"

"ahsante sana nilikuwa naulizia wapi wanapouza mafuta ya gari maanake mimi ni mgeni kijiji hiki nimeishiwa gari yangu mafuta yamebaki machache sana"

Rocky ambaye mwanzo wa riwaya hii alijulikana kwa Jina la Masanja alimuelekeza mtu yulee akijua kweli yule mtu ana shida......
Hakuwa na habari kuwa alikuwa akichorwa tu 

"sawa sawa ahasane sana ndugu yangu si vibaya tukifahamiana zaidi me naitwa Said Swalehe naishi dar es salaam nina kampuni ya uuzaji wa sampuri za magari nimekuja kutafuta vijana wa kazi hivyo naomba uwe mmoja wa vijana wangu tafadhari"

"ooooh ni vizuri sana lakini sihitaji kusafiri kwenda popote nyumba yangu nitamwachia nani sasa bwana kaka?"

"daaaah kweli kwahiyo hii nyumba unaishi pekee yako?"

Rocky hakuwa na wasiwasi na mtu huyu kwahyo hilo swali aliloulizwa alijikuta akimjibu kwa jibu la ndiyo naye bwana Jamali ambaye kajitambulisha kwa jina la Saidi Swalehe aliondoka mahali hapo huku akiwa kajipa uhakika wa kumuua Rocky kwa kuwatumia vijana wake ambao ni waharifu wakubwa katika wilaya ya Igunga........
Aliingia ndani ya gari kisha na kumuomba dereva aondoe gari.......

"tunaelekea wapi boss?"

Swali la dereva alilokuwa akimuuliza bosi wake Bwana Jamali naye alimjibu kijana wake huyo

"twende Nzega tukajipatie pongezi"

Dereva aliondoa gari na kushika rami kwa mwendokasi ndani ya gari General Brown alikuwa akimpa pongezi bwana Jamali kwa kazi nzuri japo hajaimaliza.,.....
 
"nakuambia hvi Jamali ukifanikisha hili swala nitakufanya ujione billionaire mkubwa kama billget"

General Brown Aliongea kwa furaha tupu isiyokuwa na hata nusu ya marinjirinji.......
Jamali alikuwa akitabasamu tu kupata ahadi kemukemu kutoka kwa Brown...  
Baada ya nusu saa waliweza kutimu katika wilaya ya Nzega
kitu kilichowapeleka ni kula bata na si vinginevyo......
Jamali alitoa simu yake ya mkononi kisha akatafta namba fulani akaipgia akisubiri ipokele baada ya kuita...

"eeeh haloo Michael naomba leo msiondoke nyumbani tafadhali nina kazi nataka kuwapa wewe na Steven sawa?"

"§awa boss"

Simu ikakatika Baada ya nusuu saa nzima ya kula na kunywa....
Walirudi ndani ya gari na safari ya kurejea wilaya ya Igunga ikaanza..... 
Geti la nyumba ya Bwana Jamali lilifunguliwa na gari likaingia ndani ya uzio......
Dereva...,Bwana Jamali pamoja na General Brown walishuka ndani ya gari na kuingia ndani ambapo Michael na Steven walikuwa wakiwasubiri mahali hapo........
Bwana Jamali ndiye aliyeanzisha maongezi na vijana wake 

"Michael pamoja na mwenzako Steven kuna kazi ya kufanya nadhani hamtaishindwa ni kazi ya kumsukuma mlevi tu kuna mtu anatakiwa auwawe usiku wa leo na ndio maana nimewachagua nyie nimewachagua nyie kwa sababu nawaamini sana na huyu mnayemuona hapa ni patena wangu anaitwa Brown kwahiyo msije mkawaza sana sijui kama tupo pamoja?"

"ndiyo boss"

"okay mtapelekwa na dereva mahali ambapo mnatakiwa mkafanye kazi hiyo hakikisheni mnamuua mtu huyo kwani si mtu wa kawaida ni jambazi sugu"

Jamali alimaliza kwa kuwasihi vijana wake....... 
Ni katika majira ya saa tano Steven pamoja na Michael waliizunguka nyumba ya Masanja ambaye kwa sasa tunamjua kwa jina la Rocky walimwagia petrol nyumba yote kisha wakasogea mpaka mlangoni wakafunga mlango kwa nje..... 
Masanja kwa ndani hakuwa anajua hili wala lile 
wasigogea umbaali wa hatua kama kumi wakawasha tambara ambalo wamelizungushia kwenye mti wakalitupia usawa wa nyumba ya Masanja nyumba ilishika moto.....
Ndani Masanja alishtuka kutoka kwenye wimbi zito la usingizi....
ITAENDELEA.......... 
Nimewaonyesha jinsi tukio lilivyokuwa yaani ni jinsi gani bwana Jamali pamoja na General Brown walivyokutana na nimewaonyeshea jinsi Michael na Steveni walivyofanya tukio sasa nikija na sehemu ifuatayo tutaendelea kwa Laizer Zuber naanisha hapo nilipoishia unganisha na sehemu ya kwanza ama vepi kama kuna swali uliza 
Na kama huna swali Basi usikose Muendelezo wa riwaya ......

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.