Notification texts go here Contact Us Buy Now!

Baba Kiumbe Wa Ajabu sehemu ya 17

simulizi : BABA KIUMBE CHA AJABU
SUNDAY OFA
EPISODE 17
“Vipi kuna usalama?”
“Kiasi.”
“Kuna tatizo nyumbani kwenu?”
“Hapana, kwenu.”
“Kwetu kuna tatizo gani?” nilishtuka.
“Ndoto yako imekuwa na ukweli.”
“Ina maana baba amefariki?”
“Ndiyo, inaonekana hata ndugu zako walikuwa wakikutafuta kukupa taarifa.”
“Mmh! Sasa itakuwaje?”
“Mmh! Kazi ipo nataka nikueleze kitu kimoja kabla ya kufanya lolote turudi kwanza kwa mganga.”
“Kweli hilo wazo zuri. “
“Vipi mbona unanyanyuka?”
“Mambo yameharibika, japo alinitenda vibaya lakini kifo cha baba yangu kimeniuma sana.”
“Utafanyaje imeshatokea!”
“Lakini mganga si alisema mpaka tukikutana kimwili! Sasa imekuwaje?”
“Ndiyo maana nikasema twende kwanza tukamuulize kabla hatujafanya lolote.”
“Naona tusipoteze wakati.”
“Subiri basi tumalize kunywa chai.”
“Chai haipandi tena,” nilisema huku nikinyanyuka kwenye kiti.
“Pole mpenzi wangu.”
“Bado sijapoa, kifo cha baba kimeniuma sana,” nilijikuta nikidondokwa na machozi.
“Pole mpenzi,“ mpenzi wangu alinisogelea na kunibembeleza, kitu kile kiliniongeza uchungu moyoni na kuangua kilio cha sauti kilichowashangaza waliokuwepo hotelini. Ilibidi mpenzi wangu anipeleke chumbani.
*****
Nilipofika hotelini niliendelea kulia kwa sauti ya chini huku mpenzi wangu akiendelea kunibembeleza. Pamoja na yote niliyotendewa na baba, lakini kifo chake kiliniuma sana. Niliweka pembeni ubaya wake na kuyakumbuka mapenzi yake kwangu kipindi chote cha kukua kwangu.
Nilijua kilichomponza baba yangu ni tamaa ya mali ambayo masharti yake yaliiathiri familia yetu. Nikiwa bado nimeinama nikiendelea kumlilia baba yangu, mpenzi wangu aliniuliza:
“Kwa hiyo utakwenda kwenye msiba?”
“Hata sijui nifanye nini?”
“Lakini jambo hili ni zito si la kukurupuka.”
“Ni kweli, najua kabisa kifo cha baba ndugu zangu wanajua mimi ndiye mhusika mkuu. Unafikiri nikienda itakuwaje kama siyo kutiana aibu msibani?”
“Lakini kwa nini tusirudi kwa mganga ili atueleze tufanye nini?”
“Lakini si mganga alisema mpaka tukutane kimwili, sasa nini kilichomuua baba yangu?”
“Masalu swali hilo mimi siwezi kukujibu.”
“Basi twende kwa huyo mganga.”
Tulikubaliana kwenda kwa mganga kumpa taarifa ya kifo cha baba, tulipofika tulikuta watu wengi, hivyo ilitupasa kusubiri zamu yetu japo niliamini itatuchukua muda mrefu kuonana na mganga. Hatukuwa na budi kusubiri, lakini mganga alipita na mgonjwa akienda naye nyuma ya nyumba, nilijua anakwenda kumfanyia matibabu.
Baada ya dakika kama ishirini alirudi peke yake na kuniona, alionesha ishara ya kuniita. Nilinyanyuka na kumfuata ndani ya kilinge cha kutibia, baada ya kukaa alisema:
“Vipi, mbona umerudi mapema?”
“Baba amefariki jana.”
“Sasa tatizo nini?”
Swali la mganga lilinishangaza, baba yangu amefariki yeye haoni tatizo.
“Si ulisema mpaka tukutane kimwili ndipo baba angefariki, au hata kulala chumba kimoja?”
“Masalu sijakueleza hivyo kuwa muelewa, nilikueleza mpaka mkutane kimwili si kulala chumba kimoja.”
“Sasa kifo cha baba yangu kinatokana na nini?”
“Kwa amri ya Mungu.”
“Si ulisema mpaka tukutane kimwili?”
“Eeh, lakini na Mungu ana nafasi yake, huamini kuna kifo?”
“Naamini.”
“Sasa?”
“Lakini ndugu zangu waliniomba niokoe hali ya baba, kama amekufa bila mimi kufika si nitaonekana ndiye niliyechangia.”
“Huo ni wasiwasi wako, baba yako amejiua mwenyewe kwa msaada wa ndugu zako.”
“Una maana gani kusema hivyo?”
“Baada ya kushindwa kukudhuru walijaribu uchawi mmoja ambao ni mbaya kuliko kitu chochote. Ule ukifanyiwa huchukui muda lazima ufe, baada ya kuonekana hujali na unajiamini waliamua jambo moja, kukufutilia mbali. Kama si kinga niliyokufanyia sasa hivi ungebaki jina.”
“Ni uchawi gani?” Kauli ya mganga ilinitisha.
“Kweli ndugu zako wamekupania vibaya, uchawi uliofanywa ni wa kinyonga, anakamatwa kinyonga mzima anapasuliwa na kuchunwa ngozi. Kisha ngozi yake inawambwa na kupakwa dawa huku likinuizwa jina lako. Ngozi ikikauka na wewe uhai huna.”
“Du!” Nilishtuka.
“Ndiyo walivyofanya, kazi hiyo ilifanywa saa sita usiku ili asubuhi ukiamka ukutwe umekufa. Baada ya kutega uchawi wao walikwenda kulala huku mganga akiwahakikishia kuwa asubuhi wakiamka watasikia habari za kifo chako.
“Lakini ilikuwa tofauti na walivyo fikiria, kinga niliyokuwekea ilifanya kazi, nilikueleza kila watakachokufanyia kitawarudia. Uchawi uliotaka kukuua ndiyo uliomuua baba yako. Ndio maana nilikuambia kifo cha baba yako alijitakia mwenyewe akishirikiana na ndugu zako.”
“Unataka kuniambia bila kinga nisingeiona leo?”
“Hilo ni jibu uliza swali.”
“Kuhusu kwenda msibani itakuwaje?”

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.