Notification texts go here Contact Us Buy Now!

SAFARI YA KUZIMU SEHEMU YA KUMI (10)

SAFARI YA KUZIMU
NA ZUBERI MARUMA
10.
Whatsupp: 0767433106
:"Kinzungu nzinga nzaeeeeee!"
Akatamka kwa ukali!......
"Nzaeeeeee!" Wachawi wote wakaitika bi Seli akarudia.....
"kinzungu nzinga nzaeeeeee"
"Nzaeeeeee"
Taratibu bi Seli akakisogelea kile kibuyu ambacho Mara nyingi ujaribu kumpa mwanaye bila mafanikio na kukinyanyua wakati huu kilikuwa kinafoka moshi na kumwelekezea Irene angekipokea tu ingekuwa na maana ndo kashaweka agano
Naye bila kujielewa maskin Irene akanyoosha mkono tayari kukipokea!...
Pasina kujua ndo anaingia rasmi katika utawala wa kishetani....
ile yule binti anataka kukipokea ghafla shoti ya umeme ikapiga katika mikono yake akakiachia akisindikizwa na yowe kali)
Ghafla akazinduka!,
kumbe ilikuwa ndoto,kitendo cha kushtuka akapokelewa na milio ya paka walokuwa wakipokezana kulia
"IRINEEEE!!!!.....IRINEEE!!!...IRINEE!!.....
ghafla akaisikia sauti ya mama yake ikimwita akawasha taa ghafla pakawa kimya,
Aku acha kutetemeka!, akaweka njia ya msalaba na kuchukua bible yake na kuanza kuisoma taratibu kwa muda ule wa usiku kwani alijua wazi vita baina yake na mama yake ndo vimeanza rasmi
Hivyo kwa kutumia Imani yake ni lazima ajilinde!
***
Ilikuwa ni sebule pana ilosheheni vitu vya thamani!,Zuberi alikuwa amekaa katika kochi akiwasikiliza wasanii wake wawili!
Hawakuwa wengine zaidi ya Janerose na Merry wakimwelezea " directer" wao juu ya tabia ya Irene usiku
JANEROSE:@"kweli dir yani usiku anaweweseka!,mara apige kelele yani sijui ana matatizo gani"
ZUBER@Mlishawai kumdadisi pengine? akawambia kinachomsumbua?
MERY@Hapana dir yeye anadai ananyongwa na majinamizi tutakuwa tunawangiwa tu
Binti mwingine akajibu,moyoni mwake kijana yule aloamua kumsaidia binti yule akajua ndani ya moyo wa binti yule kuna jambo linalomsumbua na akapania kuwa naye karibu kujua juu ya jambo hilo pasina kujua kwa kufanya vile ndo kauwasha moto ambao hata PATA muda hata wa kusoma.
*
Ukaribu aliouanzisha Zuberi dhidi ya Irine ukazaa jambo lingine katika moyo wake!
Mapenzi!...
Akajikuta anapatwa na msukumo wa ajabu kwa binti yule, nashindwa kuzizuhia hisia zake na kumuomba watoke ambapo wakiwa hotelini anamdodosa na Irene anajikuta akimuelezea historia kamili ya maisha yake!
Toka akiwa shuleni kipindi icho akiwa na mpz wake Chriss alompa dawa ya kumdhibitishia kuwa mama yake ni mchawi na kila kitu alichokiona!
Mwili wa kijana ulisisimka, ila akuwa na budi kumpa moyo kwani ukipenda boga penda na ua lake!
Kwa kuwa yeye mwenyewe ( bint) alikiri kutopenda swala lile la uchawi ikamtoa khof kijana yule!,khofu ya kuwa naye ila Irene akaomba apewe muda zaidi wa kulifikiria swala lile!
SIKU CHACHE BAADAYE
Mapenzi kati ya Irene na Zuber yalishamiri kila mmoja alipenda kuwa na mwenzake!
Walilishana,walinyweshana na kucheza kila mchezo wa mahaba,
"Dear nikwambie kitu!"
"Niambie tu mpz"
"Nina ujauzito wako"
"Waoooh usinambie"
"Ni kweli sweet"
Zuber akuamin aliamka na kumkumbatia mpz wake yule kwa furaha kuu
"Sasa ni muda wa Mimi na wewe kufunga ndoa!"
Akaongea Zuber kwa furaha,wakati wakiwa katika furaha ile upande wa pili katika kundi lile la wachawi baada ya kugundua Irene yu mjamzito wakapania kumtoa kafara mtoto wake yule, na kumjazia mikosi kama walivyopanga hapo awali
***
Ilikuwa katikati ya usiku kundi l la wachawi watatu wakazuka pembeni ya binti yule!
Kwa mbali zile ngoma zao ziliskika zikilia nawo wakaendelea kucheza ngoma zile bila khofu ndani yake!
Wakambeba Irene toka pale kitandani na kumuweka chini
Wakaanza kumchezea lile tumbo lake,Mara wamkalie Mara wafanye hivi Mara vile!,mara wamlishe vitu vya ajabu baada ya kuridhika wakambeba na kumrudisha kitandani wenyewe wakatoweka
Sekunde ile ile walotoweka Irene akafumbua macho na kupokelewa na maumivu makali ya tumbo
Aka anza kwa kujibaraguza kadri muda ulivyokuwa ukienda ndivyo maumivu Yale yalivyozidi kukaza mwisho alishindwa kuvumilia na kuangua kilio kilicho wa amsha wenzake!
Haraka sana wakaenda kumgongea dir wao muda ule ule wakamuingiza garini tayari kwa safari ya hospitalini!
Wakafika na daktari akawah kumpokea wakamwingiza katika wodi wenyewe wakibaki nje kusubiria
Baada ya dakika chache Daktari akatoka hakiwa na uso wa huzuni Zuberi akamkimbilia...
.
"Daktari mgongwa anaendeleaje?!"
"Plzzz nifate ofisini,"
Dokta yule alijibu na kuelekea katika ifis yake;
Zuber akamfata kwa nyuma alipofika akapewa ishara aketi!
Bado alitetemeka pasina kujua ata ambiwaje na daktari
"Tumejaribu kwa kila njia ya uwezo wetu ila imeshindikana pole sana Zuberi....
Mmmmmh nini Tena?!
Irene amekufa?!
Nini kitaendelea
TUONANE KESHO KWA MWENDELEZO

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

إرسال تعليق

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.