Notification texts go here Contact Us Buy Now!

CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA TATU (03)

CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu)
 
MTUNZI: Minnah De Embaccas

 Whatsapp :0656282898

 SEHEMU YA TATU (03)

ILIPOISHIA SEHEMU YA PILI : kas0ro Niram peke yake ambae alisema, "wala sina mpango huo, ntampeleka wapii mimi, ila nimemsifiatu! sababu katika wavulana niliowai kuwaona, kwa hapa mtanzania, yule kaka ni handsome sanaa" alisema Niram huku anawaangalia marafiki zake, ambao wakakubaliana nae, kwakiikisa vicwavyao juu chini, na wakati huo kengele ya darasani ikagongwa, wakasimama tayari kwa kuanza safari ya kuingia darasani, ENDELEA.......
Waliingia darasani, na vipindi vikaedelea kama kawaida. Niram alitafakari sana maneno ya rafiki zake,,akujua hata kwanini awazia lile jambo, maana hata sababu ya kuliwazia akuiona. "mmh mimi sasa ntakuwa nataka kurukwa na hakili haki ya Mungu" alijisemea kimoyo moyo Niram. Ila akaamua aachane na fikra zile, ambazo mwenyewe alizoziona za kipuuzi, na kuendelea na ratiba zake nyengine. ******
"hallo mmewangu nimekumisi mno utakuja lini?".ilikuwa sauti ya mama niram, aliye kuwa amepozi kwenye moja ya kochi zuri huku ameweka miguu juu ya meza. "ooh mkewangu kipenzi ratiba zinabana kazi zimekuwa nyingi mno hata mi nimekumisi kipenzi ila sina la kufanya mama".ilisikika sauti upande wa pili, ikiongea kwa masikitiko na mapenzi makubwa kwa mkewe. "ooh darling uwezi kuomba ruhusa ukaja hata kwa siku chache tu?".aliongea kwa kudeka mama niram huku akimpachika na swali mumewe huyo,aliyekuwa mbali na nchi ya Tanzania. "ooh sitawahi, unajua natakiwa kwenda india kuna Mahafali ya Razaki".ilisisitiza sauti ya baba niram. "ooh Mungu wangu nilisahau nasikitika sitoenda kwenye mahafali ya mwanangu".aliongea mama niram kwa unyonge ilionyesha hakuwa na furaha kuikosa hiyo sherehe ya mtoto wake wakiume. "usijali mke wangu, najua uwezi kuja sababu niramu hatokuwa na wakubaki nae wacha niende kukuwakilisha mimi sawa mamaa".aliongea kwakubembeleza baba niram huku akimfariji mkewe ili asijione mkosefu. "oky honey kazi njema nitafute baadae utapomaliza kazi".alisisitiza mama niram, "oky honey byeee ilove you"."love u too mume wangu byee". Waliagana mtu na mumewe, mama niramu akanyanyuka kuelekea jikoni,kuangalia kama msichana wake kama ameshamaliza kupika chakula cha mchana. *********
"eeeh ujue vincent ukumalizia story".alisikika suma akimuambia vicent, wakati huo walikuwa katika uwanja wa mpira, wakiangalia watu wanaofanya mazoezi, akiwemo Richard, yeye alikuwa akifanya mazoezi ya mpira wa kikapu, vicent na suma walikuwa wakimuangalia rafiki yao huyo, ambae alijua kuutumia uwanja vizuri aliku Hodari kweli kweli katika mchezo huo, "hahhhhah suma wewe mshkaji wangu mmbeya sana duuuh! yani kumbe ulisubiri tutoke tu!, yani wewe sikuwezi" aliongea vicent, vikafata vicheko vikaliii, suma alikuwa hana mbavuuu, ungewaona ungesema walikuwa wameona jambo la kuchekesha hapo walipo, "sasa mi nimesubiri we unihadithie naona kimya nikaona bora niseme yanini nife kiholo".aliongea suma huku anakalisha tako vizuri akimgeukua mlengwa. Basi vicent alimuadithia mwanzo mwisho, jinsi alivyokutana nae mpaka ilipofikia kusahau kumuomba namba. "hahahhhah hizo ndoto ndugu yangu yani ndo maana ukamzingua vanessa?".aliongea suma kwa mbwembwe, huku akumuona rafiki yake huyo kama anaota ndoto za mchana kweupe. "sikia suma vanessa mimi simpendi bora tu akate tamaa mapema kuliko nikaja kumuumiza zaidi huko mbele na kuhusu huyo dem ata asiponipenda baridi tu! ilimradi mi nimuekeze hisia zangu tu".aliongea vicent kwa msisitizo akimaanisha anachokisemaa. "aaah naona mnakula tu ubuyu". Aliingia Richard, katikati ya mazungumzo, mwili ukiwa umelowa jasho, aka kaa pembeni yao ilionyesha ashamaliza kufanya mazoezi *******
 "mama simu inaita".aliita msichana wa kazi wakina Vincent, akimpelekea simu bosi wake ambae alikuwa amekaa nje kwenye bustani. "asante karunde kaendelee na kazi". Alisema mama yake vicent huku anaweka mkonga sikioni. "hallow magreth niambia rafiki yangu".aliongea mama vicent, aikusikika upande wapili,mara mama vicent akaongea na kuaga"aaah! Sawa basi usijali ntakuambia tarehe ikufika nikutakie siku njema".simu ikakatwa.********
"hahahhhh!! Yani na wewe huo ubuyu tule tumekuwa shilawadu?".aliongea vicent huku anacheka, mabega yote yakifanya kazi ya kunesanesa."yani we acha tu katuchukuliaje huyu sijui huyu bwege".alijibu suma huku akimpiga kofi la bega la kiutani utani. "aaah!bac kausheni vipi ile story ya asubuh nimalizie basi mwana".aliongea Richard huku anajiweka sawa kusikiliza. Vilifwata vicheko hatari. "kumbe na wewe shilawadu" aliongea suma baada ya kumaliza kucheka. Basi story zikaanza upyaa, visent akampa fully data. Richard Akuwa na la kuchangia zaidi ya kumtia moyo na kumwambia akaze buti. mara wakasikia ...... Itaendelea......

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

إرسال تعليق

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.