Notification texts go here Contact Us Buy Now!

CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA PILI (02)

CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu)
 
MTUNZI: Minnah De Embaccas

 Whatsapp :0656282898

 SEHEMU YA PILI (02)

ILIPOISHIA SEHEMU YA KWANZA : Anaitwa Vicent Ngosha, ni mtoto wa mzee Emanueli Ngosha mfanya biashara mkubwa nchini Tanzania na nje ya nchi.Vincent alikuwa ni mvulana wa kisukuma, mama yake ni muhaya, Vicent ni mtoto pekee kwenye familia yao, ni familia yenye uwezo mkubwa, baba yake alikuwa mkoani kibiashara, hivyo alibaki pale nyumbani na mama yake, pamoja na house girl, Vicent alifika shuleni akiwa na mawazo lukuki. ENDELEA.........
Vincent alifika shule akiwa na mawazo kibao. Aliwaza kwamba alikutana na jini au mtu wa kawaida, hakika alikuwa hayupo sawa alishachanganywa na mtoto wa Kihindi, akujua afanye nini ili aweze kuwa karibu na binti yule, akika Vicent likuwa katika wakati mgumu, alijikuta anatembea bila kujielewaakinyoosha moja kwamoja mpaka darasani, “dah! nime kuwa mjinga sana, ninge omba namba, mbona demu alikuwa poa kabisa” alijilahimu Vicent, akiwa amekaa kwenye kiti chake, na kuegemea meza, kama vile anataka kulala, "hey! niggar vipi mbona umezubaa mwanangu?, yani tumekutafuta pande zote, mpaka kule bustanini, kumbe umekuja kujichimbia class, tena hata assemble ukuja" Vicent aligutushwa kidogo na kuinua kichwa kumtazama alie msemesha, japo sauti alisha itambua, kuwa alikuwa Richard, ni rafiki kipenzi wa vicent, nikama Vicent aliganda kidogo, akimtaza Richard, ambae alishangazwa na rafiki yake,Richard akageuka nakumtazama kijana mwingine alie kuwepo pembeni yake, "vipi Rich mbona leo amepoa sana, yani kama amemwagiwa maji, unanini wewe?" alidakia suma rafiki yake mwengine. maana awakumuelewa mwenzao, Vincent akujuwa amjibu nani kati yao, na awajibu nini, hivyo aliishia kutabasamu kisha akajikohoza kidogo, na kuanza kuwaambia "yani leo najiona kama nipo ndotoni, kwa nilichokutana nacho" ilikuwa sauti iliyo jaribu kuonyesha msisitizo wakile anacho kiongea, "hahahahaha! kashaanza sound zake huyu" alisema suma, huku wote wanacheka,kabla mmoja wao ajakumbuka jambo, "hoya! alafu nimekumbuka, Vannessa alikuwa anakuulizia" aliongea Richard, kama unge msikia unge juwa kuwa huyo Vannesa, alikuwa anainshu muhimu sana na Vicent, maana aliongea kwa msisitizo, "mmh! yani huyo Vanessa naomba usinitajie, maana leo ana nafasi ya kuzungumziwa hapa" alisema Vincent, ila kabla ya kuongeza neno, mara ikasikika "waoooh! jaman baby nilikutafuta huko nje kotesijakuona" wote watatu wakageuza shingo zaona kutazama upande wa mlangoni sauti iliko tokea, macho yao yaka mshuhudia binti mrembo wa ki afrika, alie kuwa anatembea taratibu kuja pale walipo kuwepo wakina Vicent, huyu ni Vanessa alie zungumziwa, “mpaka nikawa na wasi wasi kuwa leo auto kuja” aliongea tna Vanessa, kwa sauti iliyojaa furaha na mania moyoni, 
Wakati hiuo tayariwanafunzi walishaanza kuingia darasani, Vanesa alienda moja kwa moja mpaka kwa Vicent na kumkumbatia kwa furaha, lakini cha kushangaza kijana huyu akuonyesha ushirikiano, ushirikiano kwa mrembo Vanessa, "baby una nini leo?" alihoji vannessa.kwa mshngao huku anajitoa kwenye kumbatiao lake kwa Vicent, "sina kitu"lilikuwa jibu la mkato,toka kwa Vicent, "sasa kwanini huko hivyo?" aliuliza tena Vanessa, kwa sauti iliyoanza kubadirika na kunyongea, huku wezao wakiwatazama, yani Richard na Ismail wenyewe wana mwita Suma, “nimekuambia niko sawa, unielewi wewe unataka nikuambieje” safari hii Vicent aliongea kwa sauti ya juu, iliyo jaa ukali wa wazi, kihasi cha kulitikisa darasa zima, sekunde kadhaa, wtu wote kimya, wakigeuza shingo zao na kuwatazama wakina Vicent, kwa mshangao.
Kitendo hiki akikuwashangaza walewanafunzi wenzao peke yao, ata Richard na Ismail, nao walishangaa, Vanesa alitanzana chini kwa aiu, maana macho yake haya kuweza kutazama, macho ya wanafunzi wenzake me darasani, tenamacho hayo yalishindwa kuya zuwia machozi, ambayo yalianza kumtoka, akika binti huyu, akashindwa kuendelea kusimama mbele ya mvulana ambe sikuzote ame nae karibu, hivyo akageuka na kuondoka zake, huku anakimbia, akielekea nje ya darasa, "una nini mwanangu, mbona kama umeurugwa?" alihoji Richard, huku suma akidakia "mbona si kawaida yako mshikaji wangu" akika wakina Suma walionekana kusikitishwa na kitendo kile, ambacho awakukitarajia, kutokana na ukaribu wa wawili awa, hapo Vicent alikuwa ametulia nikama anawaza jambo, kisha akainua usowake taratibu, "sikilizeni niwaambie washakaji, mimi toka zamani niliwaambia kuwa, Vanesa simpendi, nyie mkasema ooh! mkubalie sijuwi hooooh! mtoto mzuri yule, et! shule nzima wanamfukuzia, bahati imekuja kwako, mala ooh! sasa nimegundua leo kuwa, mwanamke ninaempenda yupo, tena nimemuona, kwa macho yangu" alijibu vincent.marafiki zake wakatazamana kwa mshngao, huku wakimsikia Vicent anaendelea, "leo nimekutana na mwanamke ambae naweza sema ni wa ndoto zangu, sijawahi kujihisi hivi kabla, ila kwasasa ndo naanza kuhisi nimependa kwa mara ya kwanza" Vicent alizidi kuwashangaza marafiki zake, lakini kabla ajawaeleza zaidi juu ya mtoto wa Niram, mara Mwalimu akaingia darasani, na mazungumzo yakaisha kwa muda huo. ******
Vanessa ni binti mmoja mzuri mwenye sura ya duara macho ya kusinzia ana kimdomo furahi hivi cha rangi ya pink, nyuma amefungashia balaha, kiasi cha kupendezwa na kunguo yoyote atakayo ivaa, kifupi kila mwanaume, iwe mtaani au hapa shuleni, alikuwa anammezea mate, na rangi yake ya chocolate ndo kabisa, ilichangia uzuri wake kwa kwa kihasi kikubwa, ikichangia na urefu wake wa wastani,ila binti huyu Vannesa alivutiwa sana vincent mpaka akawa anashindwa kujizuia, japo alikuwa akisumbuliwa na wanaume wengi hadi walimu ila yeye limfanya Vicent kuwa ndie mwanaume wa ndoto zake, Vannesa alijitahidi kufanya kila njia na ushwishi, mpaka akafanikiwa kumfata na kumwambia, ukweli kijana huyu, Ilikuwa ni vigumu kwa vicent kukubali, maana hakuwahi kumpenda msichana, na hakujua afanye nini, ila vishawishi vilimfanya akubali, kwa maana yeye aliona labda ndo inavyokuwa mapenzi yapo hivyo, japo alisumbuliwa na wanawake wengi, ila vicent akuwahi kujihusisha na msichana yeyote yule. Kwahiyo Vanessa ni mwanamke wake wa kwanza, kimahusiano,
lakini leo tangu amekutana na Niram alijihisi tofauti, yani kama kuna kitu kina Uchoma moyo wake, hapo ndipo alipojua kuwa, kumbe sasa huku ndiko kupenda kwenyewe, maana ukiachilia kuwa alisha ona waschana wazuri wengi katika maisha yke, yaliki yule binti alimwingia sana moyoni mwake, na kuivuruga hakiri yake,
Vanessa aliingia darasani kwao, huku akifuta machozi, kwakutumia kitambaa chakechepe, akiofia wenziewasije wakaona, na kugundua kuwa alikuwa analia, hilisiyo darasa ambalo Vincent yupo, maana walisoma madarasa tofauti, licha ya kuutamachozi na kujaribu kujizuwia kulia, lakini aikuwezekana, maana donge la uchungu lilikuwa lime laa shingoni mwa Vanessaalijikuta anashindwa na kuendelea kuangua kilio cha kwikwi,
Vanesa aliwai kwenyekiti chake na kukaa, huku akijizima uso kwakuegemea kwenye meza, akizuwia na mikono yake miwili, ilimuuma sana binti huyu, akika machungu haya ya ghafla, sizani kama nitaweza kuya eezea, "nimemkosea au anipendi tena" alijiwaziwa kimoyo moyo, binti huyu, huku machozi yakizidi kutililika machonimwake na kulowesha mikono yake,mala akastuka kunamtu akimshika begani,aka jifutamacho ziharaka na kumtazama alie mshika begani, "Vanessa una nini, mbona unaonekana kama umetoka kulia" aliuliza Maria, rakifi yake na Vanessa, huku anakaa chini kwenye kiti chakee, pembeni ya Vanessa alimwangalia rafiki yake kwa macho yenye majonzi, hakika kama ungemuona usingetofautisha na mtu aliefiwa, alinyongea kupita kiasi."Maria sijui nimemkosea nini vicent amenikaripia kama mtoto mdogo" aliongea Vanessa kwasautia mbayo nikama kilio kilitaka kurudi upyaa, ila alijitahidi kukizuwia, akaendelea kuzungumza "nilimtafuta sana nje, sikumuona, baada ya kuzunguka kwa muda mrefu, ndo likanijia wazo la kumfata darasani kwao, hakika niliingia kwa bashasha ila nikapokelewa kwa hasira na dharau" mpaka hapo Vanessa alishindwa kuendelea nakuanza kulia kwa kwikwi, ilibidi Maria aanze kumbembeleza kwa kumpiga piga mgongoni, inaonyesha wanafunzi wengine awakujuwa kunacho endelea kwa Vanessa, maana kila mtu aliendelea na mambo yake,********
Mida ya saa nne, ndani ya viunga vya Shadhiliya slamic internation school, yani shuleni kwa kina Niram, mambo yalikuwa shwari, ulikuwa wakati wa mapumziko, wanafunzi walikuwa wametawanyika kwenye viunga vya shule, mida hii binti mrembo Niram, alikuwa na rafiki zake watatu ndani ya canteen ya shule, wanapata chai, mara Niram akawa kama amekumbuka jambo fulani. "jamani mwenzenu leo nimepewa lift na kijana mmoja wa Kiswahili, lakini mzuri sijapata kuona" kabla ajamaliza kuongea binti Niram, akadakia shira huyu nae ni jamii ya kina Niram yani ni muhindi pure kasoro, hawa wengine hajra na Salma, ni tofauti, wakati Salma alikuwa mpemba mweusi, ila Hajra alikuwa Mwarabu kabisaaaaa, "ahhhhh usitake kusema umempenda mswahili, hivi mzee Popat uta mbebea mbebeo gani?, si ata kuchinjaa" alisema Shira, na hapo vikafata vicheko kwa woteee, kasro Niram peke yake ambae alisema, "wala sina mpango huo, ntampeleka wapii mimi, ila nimemsifiatu! sababu katika wavulana niliowai kuwaona, kwa hapa mtanzania, yule kaka ni handsome sanaa" alisema Niram huku anawaangalia marafiki zake, ambao wakakubaliana nae, kwakiikisa vicwavyao juu chini, na wakati huo kengele ya darasani ikagongwa, wakasimama tayari kwa kuanza safari ya kuingia darasani itaendelea ......

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.