Notification texts go here Contact Us Buy Now!

Young Paster sehemu ya thelathini na saba (37)

YOUNG PASTER EP 37



Ilipoishia ……….

MCHUNGAJI MCHANGA

Aliongea mama huku akilia sana tu mana hajui maamuzi ya mtoto wake yatakuwa ni yapi,.. Kurudi katika dini ya kiislamu, au kubaki kua Mkristo
“mama…. Samahani sana…. Ila Kuanzia leo hii mimi sitaki ku….

SONGA NAYO………


Adam hakuwa mtu wa mzaha mzaha hata kidogo, kwasababu ukweli wote kesha ufahamu, hivyo hakukuwa na cha ziada zaidi ya kuamua upande upi unamhusu zaidi, Jessica alikuwa na wasiwasi juu ya adam kuwa anaweza kubadirika kurudi katika dini yake ya mwanzo, mama mwenyewe hofu mana anampenda sana mtoto wake hivyo hawezi kupingana na maamuzi yake binafsi, na hakuwa na budi kulijua hilo…

“mama…. Samahani sana…. Ila Kuanzia leo hii mimi sitaki kusikia jina la Sharbiny Rashidi kingazi,… Mimi naitwa adam Jacob Steven, na aimjui baba anaeitwa rashidi… Tena hata msingeniambia hili jambo lenu, nabaki huku ninako kujua,…. Baba ninaemjua ni mr jacob tu”

Mama na Jessica kuskia hivyo kila mmoja alipumua kwa nguvu huku wakimshukuru mungu kwa maamuzi yake, mana mama hampendi tena mumewe wa zamani na hataki hata mtoto aende huko,…
“naona sasa umekuwa mwanangu… Nashukuru kwa maamuzi yako juu ya kuchagua upande sahihi ambao wewe unaujua…”
Aliongea mama huku akiwa na furaha ya hali ya juu, mana adam kaendelea kubaki Ukristo na haujui Uislamu mana hajakulia huko,…
“mama, huyo mzee ni pepo, wala sitaki hata kumuona katika macho yangu,… Yaani kidoti tu ndio anikatae mimi sio mtoto wake… Leo nimtake wa kazi gani katika maisha yangu”
Aliongea adam tena kwa msisitizo mkubwa ili kudhihirisha kuwa hahitaji kujua kama ana baba tofauti na mr Jacob, japo ni kweli baba yake ni muislamu lakini hataki kulitambua hilo,
“Usijali baba, ni hilo tu ndilo nililokuitia hapa, hakuna kingine”
“sawa mama,… Ila naomba mujiandae, kesho naoa…. Staki tena kuchelewa, taarifuni watu kuanzia sasa hivi hapa, na eva ndio yule, maandalizi yafanyike”
Aliongea adam lakini wakati huo bado hajajua kuwa baba yake kapata balaa huko mjini…

Wakati huo huo simu ya adam iliita kuangalia ni mfanyakazi wa adam, alipokea
“tumsifu Yesu Kristo boss”
“milele amina,… Habari ya kazi mama”
“sio salama sana”
“kwanini unaongea hivyo sesi?”
“Boss… Wale watu wa mapato wamekuja tena, ila bili ya mapato imekuwa kubwa zaidi, mana inaonyesha kanisa, na nyumba pamoja na kampuni sasa sijui inakuwaje hapo”
“Jackson hayupo”
“yupo, lakini kashindwa cha kufanya mana ni pesa nyingi sana”
“ok nakuja hapo”
Adam alikata simu kisha akawasha gari yake na kuondoka,…

Sasa huku kwa mr Jacob, alishapelekwa kituoni, lakini mr Yohana hakumwacha rafiki yake, alifika nae na kufuata utaratibu wa kumshikia mtuhumiwa zamana,.. Kwa bahati nzuri zamana yake ikakubalika, hivyo walikuwa katika hoteli moja hivi, yaani hapo mr jacob hana hata mia… Yupo kama alivyo hajui afanye nini kwa wakati huo,..
“sasa mr Jacob, utafanya nini.. Mana sasa tayari upo uraiani sasa.. Tunafanyaje.. Mana bado kesi ipo pale pale”
Aliongea bwana Yohana huku mr Jacob kichwa kikimuuma kwa kuambiwa kuwa akaunti yake haipo, yaani hakujawahi kuwa na akaunti kama hio katika benki hio,..
“bwana yohana, we ulizani mimi nitafanya nini?, mana nategemea kulipa na pesa iliopo benki, sasa benki hakuna kitu, we ulizani nitafanyeje”
“mi naona uuze ile nyumba yako”
Aliongea bwana yohana huku mr Jacob akicheka
“haheheheheh… Sasa Unauza nyumba na wakati na nyumba yenyewe imo… Tena wakaniambia kuna hii nyumba mpya, na kanisa jipya.. Ambayo ni kanisa la adam na nyumba yake, pamoja na kampuni… Nikawaambia hizo mimi sihusiki nazo, kwasababu tayari nilisha kabidhi kwa mtoto wangu, nyumba ile alijenga mwenyewe, kanisa kajenga mwenyewe… Kwahio hivyo haya majengo matatu mfuateni mwenyewe”
Aliongea mr Jacob huku bwana yohana akicheka tu,.
“kwahio sasa kwa upande wakp tunafanya nini ili tuziokoe mali zako”
Aliongea mr yohana, lakini mr Jacob alikumbuka sauti ya jehova kuwa, endapo atashindwa kutekeleza matakwa yao.. Basi mali zote zitapotea na utabaki kama zamani,.. Hata pesa alizokuwa nazo benki hatozikuta tena mana hazikuwa pesa halali, ni pesa za miujiza
“ahahahahahahahah… Aaaahhhh bwana yohana, wala usihangaike… Mana hapa naiona jela mbele yangu, kwasababu jehova alisha niambia kuwa nikishindwa kufuata matakwa yao kwa kumkabidhi mtu, basi hata nifanye nini hazitorudi”
“skia, sio kuwa hazitorudi… Hapa hatuangalii kurudi kwa mali.. Bali tunaangalia uwepo wako katika uongozi…”
“hebu ngoja, niwapigie simu… Niwaombe kitu”
Mr Jacob alichukua na namba zao kabisa na kuwapigia…

“hallo habari yako ndugu”
“salama kabisa mr Jacob, vip… Una mwelekeo wowote juu ya malipo unayo daiwa”
Aliongea huyo afisa wa mapato TRA,
“hapana.. Ila ni hivi… Mnaonaje mkauza makanisa yangu yote mnibakishie moja, kampuni zangu pia mnibakishie moja.. Ili hizo zingine zilipe deni mnalonidai”
Aliongea mr jacob tena kwa huruma ya hali ya juu, yaani kama upo karibu ni lazima huruma ikujie…
“hapana ndugu… Sisi tunabinafsisha mali zako zoote, halafu tutaangalia umebakiza kiasi gani… Mana hata tukichukua mali zako zote, bado haziwezi kulipa gharama ya bilioni mia mbili point nne”
“aaahhh ndugu,.. Nina kampuni saba… Nina makanisa 50,… Vyote hivyo mchukue na bado mnidai”
“mpaka nyumba unayo ishi… Sio kampuni na makanisa tu, ni mpaka nyumba zako zote unayoishi na ulizo zipangisha… Tukishauza hivyo vyote, sasa hapo ndio unapigiwa mahesabu kimebaki kiasi gani cha pesa… Na hicho kama huna ndicho kitakacho kufunga”
“mmmmmhhhh sawa bwana… Hembu fanyeni vile mnavyo ona”
Aliongea mr Jacob huku akikosa nguvu kabisa
“sawa,.. Sasa tupo kwa mtoto wako hapa… ”
“mmmhh sawa mheshimiwa”
Mr Jacob amekuwa mtu wa kawaida Huezi mzania kuwa ni yeye… Yaani hapo alichobakiwa nacho ni hilo gari hapo na lenyewe lipo kwenye mpango wa kuuzwa na sio hilo tu bali ni magari yakw yote, yaani mashetani aliokuwa anayatumia yanaondoka na vitu vyake vyote, mpaka sifa alizokuwa akizipata nazo zinaondoka….
“bwana hali ni tete… Kile kijumba chako ulichohama ai bado kipo”
“ipi hio, ile ya kule mjini kati”
“ndio, Hio hio”
“mbona nilishauza tayari”
Aliongea bwana yohana kuwa nyumba hio alishauza tayari,.. Huku mr jacob akimuona mwenzie mjinga kwa kuuza nyumba…
“unauzaje nyumba za watoto sasa”
“heeeeee si nimeamua”
“aaahhhh sijui nitaishi wapi jacob mimi…. Hapa dawa ni kukimbia tu”
“Kiukweli mr jacob mimi sina msaada na wewe, kwasababu mimi utajiri wangu ni mdogo kuliko wewe.. Pesa unayodaiwa, mimi sijawahi hata kuiingiza kwa miaka yote hio… Mimi na utajiri wangu wote, kwenye akaunti nina bilioni moja point saba… Wewe unadaiwa bilioni mia mbili… Haaaa”
Aliongea me yohana huku mr Jacob akimlaumu kuwa
“lakini kosa ni lako… Mr jehova alituambia tuuwe watu watatu, wewe umeua mmoja, ndio mana utajiri wako ni hafifu.. Sasa hivi ungenisaidia matatizo”
“sasa mbona unanilazimisha kuua”
“aahhh we pumbavu sana… Nilikuwa nakwambia ua muumini mwingine hutaki..”
“wewe usiniite pumbavu wewe, kumbuka nimekushikia zamana ujue”
“haijalishi”
Walianza kugombana kwa kutupiana maneno ya hapa na pale,… Mr yohana alikasirika na kuondoka zake,.. Mr jacob nae kawasha gari yake na kuondoka, yaani hapo hata hilo gari likiisha mafuta Mara paaaaaap limeisha.. Hapo hana hata mia.. Chakula yenyewe kalipiwa na mr yohana, afu tayari keshamvuruga, na angelimsaidia siku mbili hizi kabla nae hajakutwa na dhahama…

Huku kwa adam, maskini alikuwa akishika kichwa kwa gharama alioikuta katika listi ya mapato anayotakiwa kuyalipa,… KAMPUNI, KANISA NA NYUMBA… ila nyumba na kanisa kinachodaiwa ni biwanja tu, mana kampuni yale ni majengo ya serikali,… Sasa adam yeye kwenye kampuni anatakiwa kulipia mapato, japo alikuwa analiapa lakini kulikua na mkono wa shetani ndani yake, sasa hakuna tena mkono wa shetani.
“lakini sawa, bilioni 19 sio kitu… Twendeni benki”
Adam anadaiwa bilioni 19 vitu vyote anavyomiliki mpaka gari yake, yaani kila kitu ni gharama ya vitu vyote, ni bilioni 19, mana ana kanisa moja, kampuni moja… Nyumba moja.. Sasa baba yake, ana makanisa 50, kampuni saba… Nyumba tano, alafu makanisa yote hakuna hata kanisa moja liliolipiwa uwanja.. Yaani viwanja vyoye alipewa na serikali, kwa nguvu za shetani, sasa hio haipo kwa kisheria mtu mmoja kupewa viwanja vyote hivyo tena vikubwa afu mijini mijini tu….

Adam kufika Bank,  ni vile vile vya baba yake, akaunti hazionekani hata moja,…
“haaaaaaa… Nyie wahudumu… Pesa zangu zimekwenda wapi… Acheni utani nyie”
Aliongea adam huku, akitamani hata kulia…
“Samahani kijana,… Baba yako ilikuwa hivi hivi… Sasa naona hii ni janja yenu wewe na baba yako…. Afande??… Piga pingu huyu ataeleza kila kitu”
“sasa jamani, muogopeni yesu jamani, kumbukeni yesu alisema atarudi kiutofaut sio kama zamani”
Aliongea adam lakini haikusaidia kitu
Lakini sasa, kuna afande aliona kitu kwa adam
“halafu huyu kijana anatuchezea akili… Hapa mkononi ana ATM kadi tatu… na hapa kajaribu mbili… Hii moja mbona hakujaribu”
Adam alikasirika kuskia wanataka kujua na hio akaunti nyingine…
“mkanifunge tu, lakini akaunti ya kanisa, ni hazina ya watoto yatima…ambayo ni sadaka za waumini wangu, Sipo tayari kuitumia… Twendeni tu”

Je? Adam atapelekwa jela? Na vipi kuhusu hio akaunti ya kanisa, ina pesa kweli au nazo zimetoweka?

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.