ACHARI YA MBIRIMBI.
Roweka mbilimbi kwa maji ya moto kwa dakika 10 kisha zitoe,zikipoa zitoe moyo zote na uziweke pembeni.
Chukua nyanya,carrot,hoho na pilipili uziblend hadi upate paste nzito.
Weka mafuta kama nusu kikombe kwenye sufuria la mfuniko mimina ile paste yako pamoja na ginger/garlic paste na spices uzipendazo(curry powder/achar masala/manjano powder etc) na chumvi wacha ichemke kwa dakika 8 hivi mimina mbirimbi zako,(zisiwe na maji)wacha zichemke kidogo,zisivurugike halafu epua uache zipoe kabla hujamimina kwenye chombo cha kuhifadhia.
Nb:unapopika funika sufuria ili isimwagike kwasababu inaruka.
Enjoy .....