JINSI PAKA ALIVYOMALIZA FAMILIA YETU
SEHEMU YA 3
WHATSAPP 0655585220
ZANZIBAR
ILIPOISHIA:
Ni pale nilipokua nimelazwa kitandani na mama mkubwa, yeye akatoka nje kwenda kuniandalia chakula, mara mlango ukawa unafunguliwa na ghafla nikasikia mlio wa paka!.
TUENDELEEE PAMOJA SASA:
Kwanza nilishtuka sana!, nikatamani niinuke niangalie ni yule paka wa kule nyumbani ama la!!, kabla sijawaza chochote zaidi....
Mara nikarukiwa na kitu kifuani!, kucheck hivi.. Daaaah!! Alikua yule yule paka wa nyumbani, safari hii alikuja katika umbile la paka na si mtu!!
"Nimekuja kukupa taarifa tu!!!".... Nilitahamaki sana baada ya yule paka kuchezesha mdomo wake na kutoa sauti ya kike iliyozungumza maneno hayo.
Kwa kuwa nilikua si mwenye uwezo wa kufanya chochote, mwili mzima umepooza, nikawa ni mwenye kumsikiliza tu.
Yule paka akaendelea kuzungumza, alizungumza kauli ambayo kwa namna moja au nyingine nilianza kuelewa dhumuni la matatizo yote anayotaka atufanyie...
" Nitawamaliza wote kama nilivyoagizwa, ili huyu baba yenu akaoe mwanamke wazazi wake waliomridhia.... Na kuthibitisha hilo, muda si mrefu naanza na mama yako mdogo, wewe nitakuweka wa mwishoni".
Kumbe huyu paka alikua amewekwa makusudi na bibi oili atumalize sisi pamoja na mama, kwa kua mama si mwanamke ambaye alitakiwa aolewe na baba!!!, Dah!!! Ukifikiria Mara mbili suala hili linauma sana mpenzi msomaji.
**
Yule paka akashuka chini, akaelekea mpaka mlangoni kisha akakojoa, sikuelewa nia yake ni nini, nikabaki kushangaa tu.
Muda si mrefu Mama mkubwa Frida akawa anaingia, mkononi kabeba bakuli la mtori, pamoja na kijipleti cha matunda na kisu.
Ile kashatua tu mguu wake kwenye ule mkojo, Mara akaanza kubadilika, kama mtu aliyechanganyikiwa au kurukwa na akili, akatupa bakuli kulee!!, lilikua la udongo likavunjika, akaotoka kisu AKAJIKITA TUMBONI!!!!
Daaaah!!!!, siwezi kuelezea maumivu niliyopata pale, mama mkubwa kioenzi, ambaye nilihisi angalau anaweza akachukua nafasi ya mama yangu aliyepoteza maisha wiki chache zilizopita, Leo paka yule yule anasababisha kifo chake.
Inabidi kushukuru mungu kwa kizuri alichokupa, ila nilijikuta natamani upofu kwa machungu ninayoyashuhudia, michirizi ya machozi ilianza kutiririka mashavuni mwangu. Maumivu niliyopata siku hii baki kuyasikia tu ndugu msomaji!!!
Wakati huo huo baba akaingia, hi ni baada ya kusikia kelele la kuvunjika like bakuli, kwasababu alilitupia dirishani na dirisha lenyewe ni la kioo.
Roho ya binadamu ni kazi sana kutoka katika kiwiliwili chake, pamoja na mkito wa nguvu aliyoupiga tumboni kwake, mama mkubwa alikua bado anagalagala chini, damu zikiwa zimetapakaa sakafuni.
"Shemeji Fridaaaaa!!! Kuna nini????"....Baba alishtuka sana kwa tukio lile.
Aliinama hadi miwani yake ikadondoka, hakujali kuhusu hilo, akambeba mama mkubwa mzima mzima, akiwa amelowa damu kisha akatoka nae nje, nahisi alitaka kumuwahisha hospitali.
**
Baada ya wao kutoka tu, yule paka akaingia tena chumbani, haraka haraka akaenda mpaka pale damu zilipokua zimemwagika akaanza kuzilamba!, alilamba kama paka wa kawaida alambavyo maziwa.
Nilifumba macho, sikutaka kuushuhudia kabisa unyama aliokua anaufanya paka yule, nilitamani niinuke nimpigilie mbali!!!
Ghafla akapanda tena kifuani kwangu, akaniongelesha tena kwa sauti yake ile ile ya kike....
" Nimeshammaliza mama yako aliyebakia, na Leo usiku nakuja na zawadi yako nzuri kabisa!!!!"
***
JE NI ZAWADI GANI HIYO PAKA MWENYE ROHO CHAFU ANATAKA AMLETEE NAOMI??
SEHEMU YA NNE SI YA KUIKOSA!!
SEHEMU YA 3
WHATSAPP 0655585220
ZANZIBAR
ILIPOISHIA:
Ni pale nilipokua nimelazwa kitandani na mama mkubwa, yeye akatoka nje kwenda kuniandalia chakula, mara mlango ukawa unafunguliwa na ghafla nikasikia mlio wa paka!.
TUENDELEEE PAMOJA SASA:
Kwanza nilishtuka sana!, nikatamani niinuke niangalie ni yule paka wa kule nyumbani ama la!!, kabla sijawaza chochote zaidi....
Mara nikarukiwa na kitu kifuani!, kucheck hivi.. Daaaah!! Alikua yule yule paka wa nyumbani, safari hii alikuja katika umbile la paka na si mtu!!
"Nimekuja kukupa taarifa tu!!!".... Nilitahamaki sana baada ya yule paka kuchezesha mdomo wake na kutoa sauti ya kike iliyozungumza maneno hayo.
Kwa kuwa nilikua si mwenye uwezo wa kufanya chochote, mwili mzima umepooza, nikawa ni mwenye kumsikiliza tu.
Yule paka akaendelea kuzungumza, alizungumza kauli ambayo kwa namna moja au nyingine nilianza kuelewa dhumuni la matatizo yote anayotaka atufanyie...
" Nitawamaliza wote kama nilivyoagizwa, ili huyu baba yenu akaoe mwanamke wazazi wake waliomridhia.... Na kuthibitisha hilo, muda si mrefu naanza na mama yako mdogo, wewe nitakuweka wa mwishoni".
Kumbe huyu paka alikua amewekwa makusudi na bibi oili atumalize sisi pamoja na mama, kwa kua mama si mwanamke ambaye alitakiwa aolewe na baba!!!, Dah!!! Ukifikiria Mara mbili suala hili linauma sana mpenzi msomaji.
**
Yule paka akashuka chini, akaelekea mpaka mlangoni kisha akakojoa, sikuelewa nia yake ni nini, nikabaki kushangaa tu.
Muda si mrefu Mama mkubwa Frida akawa anaingia, mkononi kabeba bakuli la mtori, pamoja na kijipleti cha matunda na kisu.
Ile kashatua tu mguu wake kwenye ule mkojo, Mara akaanza kubadilika, kama mtu aliyechanganyikiwa au kurukwa na akili, akatupa bakuli kulee!!, lilikua la udongo likavunjika, akaotoka kisu AKAJIKITA TUMBONI!!!!
Daaaah!!!!, siwezi kuelezea maumivu niliyopata pale, mama mkubwa kioenzi, ambaye nilihisi angalau anaweza akachukua nafasi ya mama yangu aliyepoteza maisha wiki chache zilizopita, Leo paka yule yule anasababisha kifo chake.
Inabidi kushukuru mungu kwa kizuri alichokupa, ila nilijikuta natamani upofu kwa machungu ninayoyashuhudia, michirizi ya machozi ilianza kutiririka mashavuni mwangu. Maumivu niliyopata siku hii baki kuyasikia tu ndugu msomaji!!!
Wakati huo huo baba akaingia, hi ni baada ya kusikia kelele la kuvunjika like bakuli, kwasababu alilitupia dirishani na dirisha lenyewe ni la kioo.
Roho ya binadamu ni kazi sana kutoka katika kiwiliwili chake, pamoja na mkito wa nguvu aliyoupiga tumboni kwake, mama mkubwa alikua bado anagalagala chini, damu zikiwa zimetapakaa sakafuni.
"Shemeji Fridaaaaa!!! Kuna nini????"....Baba alishtuka sana kwa tukio lile.
Aliinama hadi miwani yake ikadondoka, hakujali kuhusu hilo, akambeba mama mkubwa mzima mzima, akiwa amelowa damu kisha akatoka nae nje, nahisi alitaka kumuwahisha hospitali.
**
Baada ya wao kutoka tu, yule paka akaingia tena chumbani, haraka haraka akaenda mpaka pale damu zilipokua zimemwagika akaanza kuzilamba!, alilamba kama paka wa kawaida alambavyo maziwa.
Nilifumba macho, sikutaka kuushuhudia kabisa unyama aliokua anaufanya paka yule, nilitamani niinuke nimpigilie mbali!!!
Ghafla akapanda tena kifuani kwangu, akaniongelesha tena kwa sauti yake ile ile ya kike....
" Nimeshammaliza mama yako aliyebakia, na Leo usiku nakuja na zawadi yako nzuri kabisa!!!!"
***
JE NI ZAWADI GANI HIYO PAKA MWENYE ROHO CHAFU ANATAKA AMLETEE NAOMI??
SEHEMU YA NNE SI YA KUIKOSA!!