JINSI PAKA ALIVYOMALIZA FAMILIA YETU
SEHEMU YA 2
WHATSAPP 0655585220
ZANZIBAR
ILIPOISHIA:
Ni pale yule mtu aliyekua amekaa kwenye kiti kunigeukia huku uso wake ukiwa ni wa paka!!!
TUENDELEE PAMOJA:
Kwa kweli nilipiga kelele sana ila cha ajabu sauti yangu ikawa haitoki, nilitamani kukimbia lakini miguu yangu ilishika ganzi, mwili wote unatetemeka kama nimeingiwa na baridi, nikajikuta nadondoka pale pale.
Yule paka akavuta kiti nyuma akasimama, kwakweli sijui nikuelezaje mpenzi msomaji, ila kama unamfahamu paka vizuri basi vuta picha.... Paka kavaa nguo halafu asimame kama mtu na mkia wake uko vile vile.
Nilitamani walau iwe ndoto kwa kujaribu kufumba macho na kufumbua lakini wapi!!!, yule paka akawa anazidi kunikaribia tu. Hadi akafika mbele yangu....
"Naombaa nsaa.... Nsameheeeeee, usiniumizee!!!", Nilijaribu kumuomba msamaha asiniue lakini sauti yangu ikawa haitoki kabisa, yani nilikatwa kabisa sauti.
Yule " paka mtu " akafungua mdomo wake...
Mungu wanguuu!!! Alikua ana meno mawili marefu yamechongoka sana, ile anataka kunishika tu!!!
"Njwiiiiiiii'iii!!"... Mlango ukawa unafunguliwa, sikujua ni wa chumba kipi, kumbe alikua ni dada wetu wa kazi (anaitwa Mwajuma).
Nilishkuru mungu, kwa kuhisi msaada utakua umenifikia, baada ya kufika pale, nlishangaa Mwajuma kutoshtuka wala nini kuhusiana na yule paka, badala yale alishaangaa kuniona mimi nikiwa katika hali ile pale chini.
" Naomi vipi mbona uko hapo??"...Mwajuma aliniuliza.
"Kuna paakaaa......" Nilijaribu kumuonesha Dada Mwajuma kuna paka mbele yangu lakini haikutoka sauti yangu wala mkono haukuinuka.
"Mmmmnh hebu ngoja nikamuite baba na mama!!!!"..... Dada baada ya kuona haelewi haelewi ikabidi awahi kumuita baba na mama.
Mimi macho yote kwa yule paka mtu, akaiwekea kidole mdomoni kuashiria nisongee kitu kisha....
" pyuuuuuuuh!!!!".... Akayeyuka pale pale.
"Vipi Naomi una nini?!!!". Baba alivyofika tu alianza kuniuliza, huku akiwa na wasiwasi mkubwa.
Sasa wakati nataka niinue mdomo nimjibu na kumueleza kilichonisibu, mdomo wangu ukawa haufumbuki, nikitaka niinue mkono, mkono hauinuki.... Yani sijiwezi hata kujisogeza.
" Naomi!! Una nini binti yangu, hebu niambie mwanangu!!!"
"Naomiii!!! Naomii!!!".... Baba alinitikisa kwa nguvu walau niongee, niliishia kumuangalia tu, nilitamani nimjibu baba yangu ila nilikua sijiwezi kabisa.
Baba akaniinua haraka haraka tukatoka nje ananipakiza ndani ya gari, wakati wote huo mama alikua hajashtuka kutoka usingizini.
Ilikua ni usiku sana ila ikawa haina budi kuwahishwa hospitali, nguvu ilikua inaniishia mwilini wakati tukiwa njiani mpaka nikapotewa na fahamu.
*
Nakuja kuzinduka niko kitandani, mazingira yakiwa ni ya hospitali, nachoweza kuzungusha ni shingo tu, si mdomo wala kiungo chochote kingine cha mwili wangu nilichoweza kukisogeza.
" Pole sana Naomi!!", Baba alinishika kichwa huku akiwa pembeni yangu, kwa muangalia tu usoni alikua ametandwa na huzuni nzito.
Nilishangaa kutomuona mama muda ule, kama ingekua ni mfanyakazi wa ofisini sawa!! Lakini baba ndiye anafanya kazi na mama yeye muda mwingi shughuli zake ni za nyumbani. Ila nikajipa matumaini itakuwa yupo.
Lakini kabla sijajibu chochote, nahisi baba alitambua mawazo yangu kwa haraka...
"Usijali mama yako yupo!!"....Baba alinipa matumaini huku, nafsi ikimsuta machozi yakimtiririka kwa uchungu.. Kilio cha kwikwi kikamshika hapohapo, kwa aibu aliinamia kwenye kitanda.
Ilinipa ishara kuwa kuna kitu kibaya tu kimetokea, nilijikuta nikitiririkwa na machozi, huku kilio kikali kikibubujika ndani kwa ndani kwa kua hata sauti sauti ilishindwa kunitoka.
" Ngoja nikwambie ukweli tu mwanangu maana haina jinsi!!"....Baba ikabidi anilieleze tu hali halisi.
Kwa kweli ni taarifa chungu nisiyo isahau kipindi chote cha maisha, mama yangu alikua amefariki na wadogo zangu wote wawili wana homa sana.... Huku mimi mwenyewe madaktari wakishindwa kutambua nina tatizo gani zaidi ya MWILI KUPOOZA TU, na nilipoteza fahamu takribani wiki mbili... Hivyo walishamzika mama yangu kipenzi.
Oooh!! inauma sana kwa kweli, walau kilio kingepunguza machungu yangu lakini ndiyo vile hakitoki!!!.
Nilichukuliwa nikawekwa kwenye kiti cha wagonjwa, kwakua muda wa kukaa hospitali umeisha inabidi nikamalizie matibabu tu nyumbani.
Nilikokotwa huku nkiwa sijiwezi, mpaka kwenye gari na safari ya kurejea nyumbani ikaanza...
"Tumehamia Kawe kwa mama mkubwa wako sasa hivi"... Baba alinieleza.
Nilihisi mwanga wa matumaini unaingia ndani yangu, kwa kua moja kwa moja matatizo yote haya ni kutokana na yule paka ila kwasababu tumehama.... Kutakua na ahueni kidogo.
.......
Si muda tukawa tumeshafika nje ya nyumba ya kifahari ya Mama mkubwa Frida, nikapokewa vizuri huku nikiwa ni mwenye kubebwa tu. Sijiwezi kwa chochote yani.
Nilipelekwa mpaka chumbani nikawekwa juu ya kitanda na mama mkubwa, alikua na upendo kweli yani, ingawa na machungu ya kufiwa na mama yangu mzazi nilihisi faraja kidogo.
Mama mkubwa Frida na mama, ni watoto wa baba mmoja mama mmoja, na wana ufanani kidogo kwa mbali...
" Ngoja nikulete walau chakula kidogo!!"..Mama mkubwa aliongea kisha akatoka kwenda kuniandalia chakula.
Huku mawazo yakiwa yamenijaa, nikiwaza ntawezaje kula na picha ikanijia kichwani ya kulishwa kama mtoto mdogo, vilevile roho inaniuma kila napomkumbuka mama... Mara mlango ukasogea kidogo kama mtu anaingia vile...
Nikasikia....
"Ng'waaaaaaaaaaauuuuuh!!!"
JE NINI KITAENDELEA???
SEHEMU YA 2
WHATSAPP 0655585220
ZANZIBAR
ILIPOISHIA:
Ni pale yule mtu aliyekua amekaa kwenye kiti kunigeukia huku uso wake ukiwa ni wa paka!!!
TUENDELEE PAMOJA:
Kwa kweli nilipiga kelele sana ila cha ajabu sauti yangu ikawa haitoki, nilitamani kukimbia lakini miguu yangu ilishika ganzi, mwili wote unatetemeka kama nimeingiwa na baridi, nikajikuta nadondoka pale pale.
Yule paka akavuta kiti nyuma akasimama, kwakweli sijui nikuelezaje mpenzi msomaji, ila kama unamfahamu paka vizuri basi vuta picha.... Paka kavaa nguo halafu asimame kama mtu na mkia wake uko vile vile.
Nilitamani walau iwe ndoto kwa kujaribu kufumba macho na kufumbua lakini wapi!!!, yule paka akawa anazidi kunikaribia tu. Hadi akafika mbele yangu....
"Naombaa nsaa.... Nsameheeeeee, usiniumizee!!!", Nilijaribu kumuomba msamaha asiniue lakini sauti yangu ikawa haitoki kabisa, yani nilikatwa kabisa sauti.
Yule " paka mtu " akafungua mdomo wake...
Mungu wanguuu!!! Alikua ana meno mawili marefu yamechongoka sana, ile anataka kunishika tu!!!
"Njwiiiiiiii'iii!!"... Mlango ukawa unafunguliwa, sikujua ni wa chumba kipi, kumbe alikua ni dada wetu wa kazi (anaitwa Mwajuma).
Nilishkuru mungu, kwa kuhisi msaada utakua umenifikia, baada ya kufika pale, nlishangaa Mwajuma kutoshtuka wala nini kuhusiana na yule paka, badala yale alishaangaa kuniona mimi nikiwa katika hali ile pale chini.
" Naomi vipi mbona uko hapo??"...Mwajuma aliniuliza.
"Kuna paakaaa......" Nilijaribu kumuonesha Dada Mwajuma kuna paka mbele yangu lakini haikutoka sauti yangu wala mkono haukuinuka.
"Mmmmnh hebu ngoja nikamuite baba na mama!!!!"..... Dada baada ya kuona haelewi haelewi ikabidi awahi kumuita baba na mama.
Mimi macho yote kwa yule paka mtu, akaiwekea kidole mdomoni kuashiria nisongee kitu kisha....
" pyuuuuuuuh!!!!".... Akayeyuka pale pale.
"Vipi Naomi una nini?!!!". Baba alivyofika tu alianza kuniuliza, huku akiwa na wasiwasi mkubwa.
Sasa wakati nataka niinue mdomo nimjibu na kumueleza kilichonisibu, mdomo wangu ukawa haufumbuki, nikitaka niinue mkono, mkono hauinuki.... Yani sijiwezi hata kujisogeza.
" Naomi!! Una nini binti yangu, hebu niambie mwanangu!!!"
"Naomiii!!! Naomii!!!".... Baba alinitikisa kwa nguvu walau niongee, niliishia kumuangalia tu, nilitamani nimjibu baba yangu ila nilikua sijiwezi kabisa.
Baba akaniinua haraka haraka tukatoka nje ananipakiza ndani ya gari, wakati wote huo mama alikua hajashtuka kutoka usingizini.
Ilikua ni usiku sana ila ikawa haina budi kuwahishwa hospitali, nguvu ilikua inaniishia mwilini wakati tukiwa njiani mpaka nikapotewa na fahamu.
*
Nakuja kuzinduka niko kitandani, mazingira yakiwa ni ya hospitali, nachoweza kuzungusha ni shingo tu, si mdomo wala kiungo chochote kingine cha mwili wangu nilichoweza kukisogeza.
" Pole sana Naomi!!", Baba alinishika kichwa huku akiwa pembeni yangu, kwa muangalia tu usoni alikua ametandwa na huzuni nzito.
Nilishangaa kutomuona mama muda ule, kama ingekua ni mfanyakazi wa ofisini sawa!! Lakini baba ndiye anafanya kazi na mama yeye muda mwingi shughuli zake ni za nyumbani. Ila nikajipa matumaini itakuwa yupo.
Lakini kabla sijajibu chochote, nahisi baba alitambua mawazo yangu kwa haraka...
"Usijali mama yako yupo!!"....Baba alinipa matumaini huku, nafsi ikimsuta machozi yakimtiririka kwa uchungu.. Kilio cha kwikwi kikamshika hapohapo, kwa aibu aliinamia kwenye kitanda.
Ilinipa ishara kuwa kuna kitu kibaya tu kimetokea, nilijikuta nikitiririkwa na machozi, huku kilio kikali kikibubujika ndani kwa ndani kwa kua hata sauti sauti ilishindwa kunitoka.
" Ngoja nikwambie ukweli tu mwanangu maana haina jinsi!!"....Baba ikabidi anilieleze tu hali halisi.
Kwa kweli ni taarifa chungu nisiyo isahau kipindi chote cha maisha, mama yangu alikua amefariki na wadogo zangu wote wawili wana homa sana.... Huku mimi mwenyewe madaktari wakishindwa kutambua nina tatizo gani zaidi ya MWILI KUPOOZA TU, na nilipoteza fahamu takribani wiki mbili... Hivyo walishamzika mama yangu kipenzi.
Oooh!! inauma sana kwa kweli, walau kilio kingepunguza machungu yangu lakini ndiyo vile hakitoki!!!.
Nilichukuliwa nikawekwa kwenye kiti cha wagonjwa, kwakua muda wa kukaa hospitali umeisha inabidi nikamalizie matibabu tu nyumbani.
Nilikokotwa huku nkiwa sijiwezi, mpaka kwenye gari na safari ya kurejea nyumbani ikaanza...
"Tumehamia Kawe kwa mama mkubwa wako sasa hivi"... Baba alinieleza.
Nilihisi mwanga wa matumaini unaingia ndani yangu, kwa kua moja kwa moja matatizo yote haya ni kutokana na yule paka ila kwasababu tumehama.... Kutakua na ahueni kidogo.
.......
Si muda tukawa tumeshafika nje ya nyumba ya kifahari ya Mama mkubwa Frida, nikapokewa vizuri huku nikiwa ni mwenye kubebwa tu. Sijiwezi kwa chochote yani.
Nilipelekwa mpaka chumbani nikawekwa juu ya kitanda na mama mkubwa, alikua na upendo kweli yani, ingawa na machungu ya kufiwa na mama yangu mzazi nilihisi faraja kidogo.
Mama mkubwa Frida na mama, ni watoto wa baba mmoja mama mmoja, na wana ufanani kidogo kwa mbali...
" Ngoja nikulete walau chakula kidogo!!"..Mama mkubwa aliongea kisha akatoka kwenda kuniandalia chakula.
Huku mawazo yakiwa yamenijaa, nikiwaza ntawezaje kula na picha ikanijia kichwani ya kulishwa kama mtoto mdogo, vilevile roho inaniuma kila napomkumbuka mama... Mara mlango ukasogea kidogo kama mtu anaingia vile...
Nikasikia....
"Ng'waaaaaaaaaaauuuuuh!!!"
JE NINI KITAENDELEA???