Notification texts go here Contact Us Buy Now!

ONLY YOU SEHEMU YA 05

ONLY YOU
SEHEM YA 5
WHATSAPP 0655585220
Mwili wa Jackline ulikuwa mahali hapo lakini akili yake ilikuwa kwa Daniel. Ni kweli Peter alikuwa kijana mzuri, tajiri lakini kila alipokuwa akiongea naye, alionekana kuwa tofauti kabisa.
Alikuwa mwanaume wa usiriazi kila walipokuwa, alikuwa mwanaume ambaye hakutaka kumfurahisha, hakupenda utani tofauti na Daniel ambaye alijua kumfanya mwanamke kucheka na kujiona wa thamani katika dunia hii.
Walizungumza na walipomaliza, wakaondoka. Jackline alipofika nyumbani kwao, akajifungia chumbani kwake na kulala kitandani, kitu alichokisubiri kilikuwa ni simu kutoka kwa Daniel tu.
Alisubiri, wakati mwingine aliichukua na kuangalia jina lake, alitamani kumpigia lakini akasita, hakutaka kabisa kumuonyeshea mwanaume huyo kwamba hata na yeye alikuwa ameanza kuzimika.
Alimmisi Daniel lakini hakutaka kumpigia simu, alihisi kama angeonekana dhaifu hivyo kusubiri simu ya mwanaume huyo. Muda ulizidi kusogea, dakika, saa lakini bado simu yake haikuita, na mpaka analala, hakupokea simu kutoka kwa Daniel.
Hakulala kwa raha, usiku ulikuwa ni wa mang’amung’amu, kila wakati alikuwa akishtuka na kitu cha kwanza kabisa kuangalia kilikuwa ni simu yake, alihitaji hata kuona meseji ya salamu ili moyo wake uridhike.
Hakuwa amepigiwa simu wala kutumiwa ujumbe wowote ule. Moyo wake uliuma kupita kawaida, hakujua ni kitu gani kilitokea kwa Daniel, na mbaya zaidi hakutaka kumpigia kwa kuwa angekuwa ameonyesha udhaifu kwa mwanaume huyo.
Alikaa siku ya pili, kimya, siku ya tatu ikaingia, napo kukawa kimya. Moyoni aliumia lakini alivumilia, ilipoingia siku ya nne bila kupokea simu wala ujumbe kutoka kwa mwanaume huyo, akaamua kumpigia, hata kama angeonekana dhaifu, alikuwa radhi. Alipopiga tu, simu ikaita na kupokelewa.
“Halo Jackline,” alisikia akiitwa, moyo wake ukapata faraja kubwa kupita kawaida, mtu aliyeongea alikuwa daniel.
“Halo!”
“Nini kinaendelea huko! Naona umeifunga simu yangu, nakutafuta tangu majuzi, sikupati, meseji haziji, tatizo nini? Kuna lolote baya nililokufanyia?” aliuliza Daniel.
Hapo ndipo Jackline alipokumbuka kwamba siku ambayo alikwenda kuonana na Peter aliamua kuifunga simu ya Daniel ili isiweze kuingia kwa kupiga wala meseji, kwa siku zote alizokuwa akisubiri simu ya mwanaume huyo, si kwamba hakuwa akimtafuta, alimtafuta ila simu haikuwa ikiingia.
Alijiona mjinga, alihuzunika, hakuamini kama angesahau kama ilivyokuwa hivyo kuanza kumuomba msamaha kwamba alifanya hivyo kwa kuwa kuna mambo alikuwa akihitaji kuyafanya.
“Ndiyo unibloku?”
“Samahani sana mpenzi!” alisema Jackline, kwa kile kilichotokea, aliamini akimuita mpenzi ingesaidia, alivyofikiria ndicho kilichotokea, moyo wa Daniel ukaburudika na kujisikia faraja.
“Usijali! Nahitaji kukuona!”
“Leo?”
“Ndiyo!”
“Haina shida! Wapi?”
“Unaweza kuja nyumbani?”
“Wapi? Mwenge?”
“Yeah!”
“Sawa haina shida!”
Baada ya kukubaliana, Jackline akakata simu na kuanza kujiandaa. Moyo wake ulikuwa na shauku kubwa ya kukutana na mwanaume huyo, aliumia baada ya kuona kwamba kipindi chote hakuwa amewasiliana na kijana huyo kwa sababu ya uzembe wake.
Kipindi hicho, hakumfikiria tena Peter, kwake, Daniel ndiye alikuwa kila kitu. Alipomaliza kujiandaa, akatoka, akachukua gari na kuondoka nyumbani hapo kuelekea Mwenge alipokuwa akiishi Daniel.
Hakuchukua muda mrefu akafika Mwenge Mataa ambapo akawasiliana na Daniel na kumuelekeza mahali alipokuwa akiishi na kwenda huko. Alipofika, akaelekezwa kuliingiza gari ndani ya nyumba ya akina Daniel na kuteremka.
Wakasogeleana na kukumbatiana kwa furaha, kila mmoja hakuamini kumuona mwenzake mahali hapo. Moja kwa moja Daniel akamchukua na kuelekea naye ndani.
Kwa jinsi Jackline alivyovaa, Daniel alichanganyikiwa, kwake, siku hiyo alionekana kuwa msichana mrembo kuliko wote aliowahi kukutana naye.
Alivalia gauni refu jekundu, nywele zake alikuwa amezibana, chini alivalia viatu virefu kidogo na alikuwa amebeba mkoba wa rangi ya damu ya mzee.
Alikuwa akinukia vizuri kiasi kwamba alipoingia ndani ya nyumba hiyo, n harufu ya manukato yake tu ndiyo iliyokuwa ikisikika kila kona. Walikaa sebuleni kwa dakika chache huku akimtambulisha msichana huyo kwa wadogo zake na dada wa kazi kisha kuelekea chumbani kwake.
Macho ya Jackline yalikuwa yakiangalia huku na kule, kiukweli kwa jinsi Daniel alivyokuwa akiishi na familia yake, walikuwa wakiishi katika maisha ya kawaida sana, hayakufanana na maisha ya akina Peter lakini moyoni mwake hakutaka kuyafikiria maisha hayo kwa sana, kwake, kitu alichokuwa akikifikiria ni kuwa na mwanaume huyo tu.
Waliongea, wakachombezana, wakashikana hapa na pale mwisho wa siku wakabaki watupu kitandani, kilichosikika baada ya hapo ni sauti ya kitanda iliyokuwa ikilalamika.
Jackline hakutegemea kufanya mapenzi na Daniel lakini akajikuta akifanya naye kwa kuwa hakuona kama kungekuwa na mwanaume mwingine ambaye angestahili kufanya naye kwa kipindi hicho.
“Jackline! How do you feel,” (Unajisikiaje, Jackline?) aliuliza Daniel huku akimwangalia msichana huyo usoni.
“Normal!” (kawaida) alijibu msichana huyo huku akionekana kusikia aibu.
“Do you really love me?” (unanipenda kweli?)
“I need some time to answer such a question,” (nahitaji muda kulijibu swali kama hilo) alisema Jackline.
“Why?” (kwa nini?)
Jackline hakulijibu swali hilo, alibaki akiangalia pembeni tu, Daniel hakutaka kumuacha hivi hivi, alichokifanya ni kumvutia tena kwake na kuanza kubadilishana mate.
Wakati huo walikuwa watupu kabisa, kilichotokea ni kuanza kufanya tena mapenzi kitu ambacho kwa Jackline kilimfanya kumpenda zaidi Daniel lakini hakuwa radhi kumwambia ukweli kwamba alikuwa akimpenda mno.
Mtu ambaye alikuwa kichwani mwake ni Peter, aliona kabisa kwamba kulikuwa na kazi kubwa kuachana na Peter lakini kwa jinsi Daniel alivyokuwa akija kwa kasi kichwani mwake, aliona dalili zote kwamba hakuwa na muda mrefu wa kuwa na mwanaume huyo.
Walipomaliza kila kitu, tayari ilikuwa ni saa moja usiku, wakaenda kuoga, walipomaliza, msichana huyo akaaga na kuondoka kurudi nyumbani kwao.
Njiani, akachukua simu yake na kuiangalia, kulikuwa na missed calls nyingi kutoka kwa mpenzi wake, Peter, alikuwa amemtafuta zaidi ya mara kumi lakini hakuwa amepokea kwa sababu simu ilikuwa kwenye ‘silent’ lakini pia hakutaka kuishika kuogopa simu yoyote ya Peter kuonekana.
Alitamani kumpigia lakini akasita, kuzungumza na Peter ilikuwa ni lazima afike nyumbani kwanza ndipo ampigie. Akaiacha na kuendelea na safari yake.
Alimfikiria Daniel, ni kweli aliwahi kufanya mapenzi na Peter lakini kwa mwanaume huyu wa leo alikuwa balaa. Alijua kuuchezea mwili wake, alijua kuzishika sehemu zilizokuwa zikimchanganya, alijua kumlamba sehemu zote mwili mwake, kwa kifupi, kwake, Daniel alikuwa fundi zaidi ya mkandarasi.
“Daniel! You are the man,” (Daniel, wewe ni mwanaume) alijisemea Jackline huku safari ya kurudi nyumbani ikiendelea kama kawaida.
Kutokana na foleni kubwa iliyokuwa njiani, alichukua dakika arobaini mpaka kufika nyumbani, akaliingiza gari ndani, alipolipaki, akateremka na kuelekea sebuleni.
Alipoingia tu, macho yake yakagongana na macho ya Peter aliyeonekana kuwa na hasira mno, mbali ya mwanaume huyo, pia kulikuwa na wazazi wake, wao walikuwa wakimwangalia kwa jicho la kusikitisha, kwa jinsi hali ilivyoonekana, kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.
“Umetoka wapi?” aliuliza baba yake baada ya salamu!
Jackline alibaki kimya, aliogopa, mahali hapo hakukuonekana kuwa na amani, kuwaambia kwamba alitoka kwa akina Daniel lilikuwa jambo gumu, alibaki akiwaangalia watu wote waliokuwa humo kwa zamu.
“Nimekuuliza umetoka wapi?” aliuliza mzee Mwamanda huku akionekana kukasirika.
Akainuka kwenye kochi na kumsogelea Jackline pale alipokuwa amesimama, alipomfikia, akamzaba kibao. Mzee huyo alikasirika, si kwamba Peter alikuja mahali hapo tu bali msichana huyo aliondoka pasipo kuaga.
Peter alikuwa kimya, moyo wake ulimuuma kupita kawaida, alimpigia simu msichana huyo mara kadhaa lakini haikuwa ikipokelewa, alichanganyikiwa na kuhisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea na hivyo kuelekea nyumbani kwao.
Hapo nyumbani alipofika, hakumkuta, roho ilimuuma na kitu ambacho kilikuja kichwani mwake ni kwamba msichana huyo alikuwa na mwanaume sehemu fulani. Aliwaelezea wazazi wake kilichotokea na hivyo kumsubiri.
“Ulikuwa wapi?” aliuliza mzee Mwamanda lakini bado Jackline hakujibu kitu.
Jackline alikasirika, kwa hasira zake, akaondoka sebuleni hapo na kuelekea chumbani kwake ambapo akajifungia na kuanza kulia.
Peter aliyekuwa sebuleni akasimama, akaondoka kuelekea chumbani kwa Jackline, alijaribu kuufungua mlango lakini ulikuwa umefungwa kwa ndani hivyo kuanza kugonga akimtaka msichana huyo amfungulie.
Hakukubali, hakutaka kuzungumza na mtu yeyote kwa kipindi hicho, aliendelea kubaki chumbani huku Peter akiendelea kugonga kwa takribani dakika arobaini na tano lakini msichana huyo hakufungua mlango.
“Mama! Naondoka, nitazungumza naye kwenye simu,” alisema Peter huku akionekana kunyong’onyea.
Akaondoka huku moyo wake ukiwa na huzuni tele, alitegemea kwamba angezungumza na mpenzi wake na kumuuliza kilichokuwa kimetokea lakini ilishindikana.
Akaondoka nyumbani hapo, njiani, Peter alikuwa na mawazo tele, kichwa chake kilifikiria kuhusu kusalitiwa tu jambo ambalo hakutaka kuona likitokea katika maisha yake yote kwa kuwa tu alimpenda Jackline.
Alipofika nyumbani, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumpigia simu msichana huyo, hazikupokelewa, alipojaribu kumtumia meseji pia hazikujibiwa kitu kilichomfanya kuwa kwenye wakati mgumu kupita kawaida.
Wakati yeye akihuzunika, Jackline alikuwa chumbani kwake akilia, hakupenda kuona baba yake akimpiga kibao mbele ya mpenzi wake, kwake, ile ilionekana kuwa dharau kubwa.
Alikaa chumbani huku akilia, katika kipindi kigumu kama hicho alihitaji jambo moja tu, kufarijiwa na mwanaume, tena asiwe mwingine zaidi ya Daniel ambaye ndiye aliyekuwa moyoni mwake kipindi hicho. Wakati akiwa kwenye huzuni huku akisubiria faraja, mara simu yake ikalia mlio kuashiria kwamba kulikuwa na meseji iliyokuwa imeingia, akaichukua simu, ilitoka kwa Daniel.
“Ulifika salama mpenzi?” aliuliza Daniel kwenye simu kwa njia ya meseji.
“Yeah! Ila nilipigiwa!”
“Na nani?”
“Baba!”
“Kisa?”
“Niliondoka bila kuaga!”
“Pole sana mpenzi!
“Ahsante sana!”
“Nije nikuone?”
“Sasa hivi?”
“Yeah! Umepigwa, sidhani kama ni jambo zuri nikibaki nyumbani na wakati msichana nimpendaye amepigwa!” aliandika Daniel.
“Hapana! Ni usiku sana sasa hivi!”
“Hata ingekuwa saa kumi alfajiri, bado ningeweza kuja kwa ajili yako, naomba uniruhusu mpenzi!” aliandika Daniel.
“Hapana! Kesho mpenzi!”
“Sawa.”
Walichati tu mpaka ilipofika majira ya saa saba usiku. Moyo wa Jackline ulichanganyikiwa kabisa, kwake, Daniel alionekana kuwa kila kitu, yule Peter ambaye alikuwa kwenye moyo wake kwa kipindi kirefu alianza kuondoka na mwanaume huyo mpya kuanza kukalia kiti moyoni mwake.
Daniel alijua kila kitu, kuanzia kujali na hata kufanya mambo mengine ya kumdatisha msichana kama yeye. Hakumfikiria tena Peter na kitu pekee alichokuwa akikifikiria ni kumwambia mwanaume huyo ukweli kwamba hakutaka kuwa naye tena kwa sababu kulikuwa na mwanaume mwingine aliyeingia moyoni mwake.
Hakujua ni kwa jinsi gani angeanza kumwambia ukweli wa kilichokuwa kikiendelea. Alijaribu kufikiria njia nzuri, akawaza kumpigia simu, akaona njia hiyo si sahihi, akafikiria kuhusu kumtumia meseji lakini napo akagundua kwamba jambo hilo si zuri, alichokifikiria mara ya mwisho ni kumwambia kwamba waonane halafu amwambie ukweli kile kilichokuwa kikiendelea.
“Mmh! Nitaweza kweli?” alijiuliza.
Ilikuwa ni lazima afanye hivyo, moyo wake haukuwa na uwezo wa kuwaweka watu wawili na kuwapenda kwa upendo sawasawa, ilikuwa ni lazima mmoja aondoke, na huyo mtu aliyetakiwa kuondoka alikuwa Peter.
Hakutaka kuchelewa, akachukua simu yake na kumpigia, ilipopokelewa, akamwambia kwamba alitaka kuonana naye hivyo watafute sehemu kwani kulikuwa na mambo mengi waliyotaka kuzungumza.
“Kuna tatizo?” alisikika Peter akiuliza.
“Hapana! Ninataka kuzungumza nawe,” alisema Jackline na kukata simu.
Baada ya saa moja, wawili hao walikuwa katika mgahawa wa Jumanji uliokuwa Mbezi Beach, Jackline alionekana kuwa na hofu juu ya kile alichotaka kumwambia Peter. Ni kweli mapenzi kwake yalipungua lakini upande mwingine alimuonea huruma mwanaume huyo.
Alianza naye mbali, alimpenda, alimpa zawadi nyingi, alimfanya kuwa mwanamke mwenye furaha lakini hayo yote yalikuja kutoweka baada ya kumpata Daniel ambaye hakuwa na pesa sana, hakuwa na kitu chochote cha kumpa lakini mapenzi aliyomuonyeshea, jinsi alivyomjali ilikuwa ni tofauti na Peter.
Peter alionekana kuwa na wasiwasi, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea kwa mpenzi wake, alimwangalia, kwa jinsi Jackline alivyoonekana, alionekana kuwa na kitu fulani alichotaka kumwambia mahali hapo.
Walikula na kunywa kwani Jackline aliamini kwamba kama wasingekula, baada ya kuzungumza kusingekuwa na mtu ambaye angekuwa na hamu na chakula.
“Jack mpenzi, kuna nini?” aliuliza Peter huku akimwangalia msichana huyo usoni.
“Peter! Naomba usinielewe vibaya,” alisema Jack, akameza funda la mate na kuendelea:
“Nimekaa na kufikiria sana, naomba usipingane na uamuzi wangu kwa kuwa unaweza kupingana nao na baadaye kujuta,” alisema msichana huyo maneno yaliyomfanya Peter kuwa na hofu zaidi, mapigo yake ya moyo yakaanza kudunda kwa nguvu.
Je, nini kitaendelea?

By Ahmad Mdowe

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

إرسال تعليق

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.