Notification texts go here Contact Us Buy Now!

ONLY YOU SEHEMU YA 04

ONLY YOU
SEHEM YA 4
WHATSAPP 0655585220
“Mungu! Naomba unisaidie, sitaki mwanaume yeyote auchukue moyo wangu kutoka kwa Peter,” alisema Jackline.
Wakati mwingine mpenzi wake, Peter alipokuwa akipiga simu alikuwa akiiangalia tu, aliipokea na kumsikiliza. Mwanaume huyo hakuwa mchangamfu kama Daniel, hakuweza kumchombeza kwa maneno matamu kama kijana huyo, aliongea naye na alipokata tu, simu iliyofuata ilikuwa ni ya Daniel.
“Umekwishakula?”
“Leo sijisikii kula!”
“Kwa nini?”
“Nahisi kama naumwa!”
“Pole sana! Labda nikutoe lunch, unaonaje?”
“Lunch? Wapi?”
“Manzese, kuna mama ntilie mmoja anapika chakula safi sana,” alisema.
“Kwa mama ntilie? Manzese?”
“Yeah!”
“Are you serious?”
“Nakutania, naomba tuonane hapo Mlimani City!”
“Marry Brown au KFC?”
“KFC.”
“Sawa. Ndani ya nusu saa nitakuwa hapo,” alisema.
Siku zote hizo walikuwa wakiwasiliana kwenye simu tu, hawakuwa wameonana, kitendo cha kusema kwamba waonane Mlimani City kilimpagawisha Daniel, akakurupuka, akaingia bafuni kuoga harakaharaka na kujiandaa kisha kuondoka.
Daniel hakukisahau kikaratasi kile alichokiandika kwa mara ya kwanza alipomuona Jackline, alikichukua na kukiweka mfukoni, alihitaji kumuonyeshea msichana huyo ili ajue ni kwa kiasi gani alikuwa amempenda tangu siku ya kwanza alipomtia machoni mwake.
Tangu alipoanza kuoga, ni ndani ya dakika ishirini tayari alikuwa Mlimani City katika Mgahawa wa KFC akimsubiria Jackline ambaye aliingia baada ya dakika kadhaa. Haraka Daniel akasimama, akamkaribisha na kumkumbatia, wakakaa.
“Nimechoka sana kukwambia kitu kimoja kila siku,” alisema Daniel.
“Kipi?”
“Kwamba unapendeza sana! Yaani kila siku nikikwambia hivyo, nachoka, basi hata siku nyingine vaa kawaida,” alisema Daniel, Jackline akatoa tabasamu.
“Nashukuru!”
“Na unanukia vizuri sana! Kama Muingereza!”
“Hahah! Una maneno!”
“Sure! Jackline, wakati mwingine nahisi ni kama ndoto kufahamiana na wewe! Najiona muda wowote ule nitaamshwa na kuambiwa niende chuo,” alisema.
“Mimi mbona wa kawaida tu!”
“Najua! Hata Bill Gates anajiona ni mtu mwenye hali ya kawaida kiuchumi!”
“Jamani! Unanifanya nasikia aibu.”
“Hebu angalia macho yako, angalia lipsi zako, angalia mashavu yako, Jackline, nina uhakika hujazaliwa kama sisi, wewe umeshushwa kutoka juu,” alisema Daniel huku akimwangalia Jackline machoni.
“Jamaniiiiiii...”
“Na kama umezaliwa, basi si hospitalini, umezaliwa supamaketi kule Dubai!”
“Hahah! Jamani Daniel!”
“U mzuri sana mpaka unaboa!”
Daniel hakuacha kumsifia Jackline, uzuri wake ulikuwa ukionekana dhahiri, watu wengi waliokuwa mahali pale walikuwa wakimwangalia msichana huyo.
Alipendeza, alivutia na kikubwa zaidi alionekana kama msichana kutoka katika ulimwengu mwingine kabisa. Waliongea mambo mengi mahali hapo, Daniel hakutaka kumwambia kuhusu suala la uhusiano wa kimapenzi, alichokihitaji ni kumuonyeshea jinsi alivyokuwa akimpenda tu.
Daniel hakutaka kuchelewa, alichokifanya ni kuingiza mkono mfukoni na kukitoa kile kikaratasi alichokuwa amekiandika siku ya kwanza alipomuona Jackline na kumgawia.
Jackline akakichukua na kuanza kukisoma, alishangaa, alimwangalia Daniel, akatoa tabasamu, hakuamini kama kweli kijana huyo alikiandika kikaratasi kile siku ya kwanza alipoonana naye.
“Hii ilianza tangu siku ya kwanza, nilikuona kuwa wa tofauti sana,” alisema Daniel huku akiachia tabasamu.
“Kipi kimekuchanganya?”
“Uzuri wako, unatisha sana, yaani kama ni kuumba, nadhani siku hiyo Mungu alitulia sana, alihakikisha hakuna kazi yoyote anayoifanya siku nzima, ni kukuumba wewe tu,” alisema Daniel na wote kuanza kucheka.
“Jamaniiiiiiii!”
Walipomaliza kula, akamchukua na kumpeleka kwenye sinema ambapo kulikuwa na filamu nzuri ya mapenzi na kuingia. Walikuwa pamoja, walitembea pamoja na kukaa pamoja.
Jackline alijihisi tofauti kabisa, alikuwa huru na wakati mwingine hata Peter alipokuwa akipiga simu, aliifunika simu yake, hakutaka kuongea kwani alamini kwamba kama angeipokea, angemvurugia umakini wake kwa mwanaume huyo. Filamu ilipokwisha, wakatoka!
“Tutaonana siku nyingine! Ahsante kwa chakula na ahsante kwa filamu!” alisema Jackline.
“Usijali! Ila na wewe ahsante kwa kukubaliana nami kuja hapa,” alisema Daniel wakati huo walikuwa wamesimama pembeni ya gari alilokuja nalo Jackline.
“Usijali!”
“Kwa hiyo kuonana mpaka Yesu arudi au?”
“Hahaha! Tutaonana tu!”
“Lini? Mwaka kesho?”
“No! Hivi soon. Kuna vitu nitakuwa navyo bize kidogo, ila tutaonana.”
“Sawa. One last thing!” (kitu cha mwisho)
“What is it?” (kipi hicho?)
“Umependeza sana! You look stunning!” (unang’aa)
“Ahsante! Ila usichoke kuniambia hivyo!”
“Haina shida!”
“Sawa. Bye!”
“Bye!” alisema Jackline, akaingia ndani ya gari, Daniel akabaki amesimama nje huku akimwangalia kwa uso wenye tabasamu.
“Mbona huondoki?”
“Nataka mpaka uondoke, nisije kuondoka halafu watu wakakuiba! I have to keep you safe” (natakiwa kukulinda) alisema.
“Ooh! Sawa. Nashukuru kwa kunijali!”
“Nashukuru kwa kuniruhusu kukujali!” alisema Daniel, Jackline akawasha gari na kuondoka mahali hapo huku mwanaume huyo akibaki akiwa amesimama akimwangalia msichana huyo alivyokuwa akiondoka.
***
Japokuwa moyo wa Jackline ulianza kutekwa na kijana Daniel lakini hakutaka kuonyesha ishara yoyote ile. Kwake, alikuwa na mpenzi mmoja aliyekuwa akimpenda kwa moyo wake wote, mwanaume ambaye aliamini kuwa kuna siku angekuja kumuoa, mwanaume huyo alikuwa Peter.
Peter ndiye alikuwa mwanaume wake wa kwanza, walionana nchini Afrika Kusini walipokuwa wakisoma katika Chuo cha Pretoria kilichokuwa nchini humo.
Walipendana! Kwa uzuri aliokuwanao Jackline, wanaume wengi walimfuata na kumtongoza lakini hakutaka kukubaliana nao, kwake, mwanaume ambaye alionekana kuuteka moyo wake alikuwa mmoja tu.
Wakawa pamoja, wakafanya mambo mengi huku wakiwa wanatoka kwenda sehemu mbalimbali. Peter alikuwa na muda wa kuyafurahia maisha yake na mpenzi wake huyo.
Walipokuwa wakirudi Tanzania, walikuwa pamoja, walionyesheana mapenzi kemkem kiasi kwamba mpaka wazazi wa pande zote mbili walijua kile kilichokuwa kikiendelea.
Walipanga mambo mengi maishani mwao na kuahidi kwamba wangeishi pamoja mpaka pale ambapo wangefukiwa ardhini. Walikuwa na imani hiyo na kila mtu aliyekuwa akiwaangalia alijua dhahiri kwamba watu hao wangeishi pamoja siku moja.
Kwa kuwa walikuwa watoto wa matajiri, kila walipokuwa wakirudi nchini Tanzania, walikuwa wakiondoka kwenda Misri katika mapiramidi yaliyokuwa Giza na sehemu mbalimbali kuyafurahia maisha yao.
Hakukuwa na mtu aliyekuwa radhi kumuacha mwenzake, walipenda kupita kawaida. Walipambana, kulipokuwa kukitokea vishawishi vingi, walihakikisha wanashikama na kuvishinda ilimradi tu mwisho wa siku waendelee kuwa pamoja.
Huku maisha yakiendelea kama kawaida, Peter akaanza kuona tofauti kwa mpenzi wake, hakuwa kama alivyokuwa kipindi cha nyuma, yale ambayo hakuwa akitaka kuyaona kwa mpenzi wake, yakaanza kuonekana kitu kilichomtia hofu ya kumpoteza msichana huyo.
Alipokuwa akimpigia simu, msichana huyo hakuwa akipokea na wakati mwingine simu yake ilikuwa ikitumika kwa kipindi kirefu na kila alipokuwa akimuuliza, alimwambia kwamba alikuwa akizungumza na ndugu zake.
Hilo likamfanya Peter kukosa amani, akahisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea ambacho Jackline hakutaka kukiweka wazi.
Hakutaka kuliona penzi lao likipotea, alichokifanya ni kuwasiliana na Jackline na kumwambia kwamba walitakiwa kuonana kwani kulikuwa na mambo kadhaa walitakiwa kuyazungumza kama wapenzi.
“leo?” aliuliza Jackline.
“Ndiyo!”
“Mbona umenishtukiza sana mpenzi?” aliuliza msichana huyo kwa sauti nyembamba.
“Dakika kadhaa tu bebi!”
“Jamaniiii!”
“Basi nakufuata!”
Ni ndani ya dakika kadhaa tu tayari Peter alikuwa ndani ya eneo la nyumba ya mzee Mwamanda. Akateremka kutoka kwenye gari lake la kifahari na kuufuata mlango wa kuingilia sebuleni na kuingia ndani.
Kila mtu aliyemuona alifurahi, kijana huyo alionekana kuwa sahihi kwa Jackline, alipendwa kwa kuwa tu alionekana kuwa na penzi la dhati ambalo mwanaume alitakiwa kumuonyeshea mwanamke.
Jackline alikuwa chumbani kwake, aliposikia kwamba Peter amefika, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuchukua simu yake na kuzifuta meseji zote alizokuwa amewasiliana na Daniel.
Hilo lilimuuma kwa kuwa kila alipokuwa akimkumbuka kijana huyo alichukua simu hiyo na kuanza kuangalia jinsi walivyokuwa wakichati lakini kwa kuwa hakutaka kuona mpenzi wake akihisi kitu chochote kibaya, akaamua kuzifuta meseji hizo.
“Mmh! Asije akanipigia simu bure,” alisema Jackline, alichokifanya ni kuibloke namba ya Daniel, yaani kwa kifupi hakutaka kupokea ujumbe wala meseji kutoka kwa mwanaume huyo wakati akiwa na Peter.
Alipohakikisha amerekebisha kila kitu kwenye simu yake, akavaa nguo zake na kutoka chumbani kwake, alipofika sebuleni, akamkumbatia mpenzi wake na kutoka.
Ndani ya gari Jackline akajifanya kuwa na furaha isiyokuwa na kifani. Alitaka kumuonyeshea mpenzi wake kwamba hakukuwa na kitu chochote kilichokuwa kikiendelea upande wa pili.
Kile kikampa upofu Peter na kuona kwamba hakukuwa na kitu chochote kibaya kilichokuwa kikiendelea kwa mpenzi wake. Waliendelea na safari mpaka walipofika katika mgahawa wa kishua wa Brown Dolphin uliokuwa Masaki, wakaingia na kuanza kupata chakula.
“Kuna kitu gani kinaendelea mpenzi?” aliuliza Peter huku akimwangalia Jackline, wakati huo walikuwa wamekwishamaliza kula.
“Kivipi mpenzi?”
“Yaani naona kama kuna mabadiliko yameanza kujitokeza, kuna nini?” aliuliza Peter huku akimwangalia mpenzi wake huyo.
“Hakuna kitu!”
“Una uhakika?”
“Yeah! Kwani kuna lolote lile?”
“Kama hakuna haina shida. Unajua wakati mwingine nakuwa na wasiwasi sana,” alisema Peter na kuanza kucheka.
Mwili wa Jackline ulikuwa mahali hapo lakini akili yake ilikuwa kwa Daniel. Ni kweli Peter alikuwa kijana mzuri, tajiri lakini kila alipokuwa akiongea naye, alionekana kuwa tofauti kabisa.
Je, nini kitaendelea?

By Ahmad Mdowe

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.