*ROSTI YA MBUZI NA VIUNGO MBALIMBALI*
MAHITAJI YA KUPIKA ROSTI YA MBUZI
- *Kwa nyama*
- 500g/ nusu kg nyama ya mbuzi
- ½ limao
- Vijiko 1½ vya chakula majani ya kotimiri au
- giligilani
- Vijiko 1½ vya chakula majani ya mnanaa
- Vijiko 1 vya chakula kitunguu saumu
- Kijiko 1 cha chakula tangawizi ya unga
- ¼ kikombe mafuta ya mzaituni (olive oil)
- Chumvi kwa kuonja
- Viungo vya rosti
- Viazi ulaya vya wastani 3-4
- Nyanya 2
- Kitunguu 1 kikubwa
- Kijiko 1 cha chai kitunguu saumu
- Vijiko 2 vya chakula nyanya ya kopo
- Pilipili kichaa 1
- Vijiko 2 vya chakula mafuta ya samli au mafuta ya kupikia
- ½ kikombe vitunguu vya majani
- ¾ kijiko cha chai tangawizi ya unga (au fresh)
- Jani la bay 1 ( bay leaf )
- Karafuu punje 3
- Iliki 3
- Kijiko 1 cha chai giligilani ya unga (coriander powder)
- Kipande cha mdalasini
- Kijiko 1 cha chai garam masala
- Chumvi kwa kuonja
JINSI YA KUPIKA ROSTI YA MBUZI
- Andaa viungo vya marinate; Katakata majani ya kotmiri au majani ya giligilani; kamua limao; twanga kitunguu saumu
- Kwenye bakuli kubwa, changanya nyama na viungo vyote vya marinade vizuri. Funika bakuli, acha viungo vikolee kwa masaa kama manne au vizuri zaidi usiku kucha
- Andaa viungo vya rosti; katakata viazi roborobo; kata pilipili vipande virefu; twanga kitunguu saumu; katakata majani ya kitunguu vipande vyembamba, weka pembeni
- Weka nyanya na kitunguu katika mashine ya kusagia chakula kutengeneza rojo, weka pembeni
- Kwenye sufuria katika moto wa wastani, weka mafuta ya samli. Yakichemka ongeza kitunguu saumu na viungo vizimavizima; karafuu, iliki na mdalasini. Kaanga kwa dakika kama 2; au mpaka kitunguu saumu kiive vizuri
- Ongeza nyama iliyokuwa marinated. Kaanga kwa dakika kama 5, au mpaka iwe ya kahawia kiasi
- Ongeza jani la bay (bay leaf) rojo ya nyanya pamoja na viungo vikavu; giligilani ya unga, tangawizi ya unga na garam masala. Ongeza na chumvi kwa kuonja. Pika mpaka nyanya ziive vizuri kabisa
- Ongeza vikombe 2 maji. Funika na mfuniko, acha nyama iive moto wa chini kiasi kwa dakika 20 hadi 30; au mpaka ilainike kabisa na maji yaanze kukaukia
- Ongeza viazi. Pika mpaka viazi viive vizuri na sosi iwe nzito
- Ongeza majani ya kitunguu, pika kwa dakika 1 nyingine
- Pakua kama utakavyopenda
- Enjoy