Notification texts go here Contact Us Buy Now!

NISAMEHE RATIFA SEHEMU YA 20

NISAMEHE RATIFA EP 20


Leo hii alikuwa ndani ya gari la heshima, miongoni mwa magari yaliyopandwa na viongozi wakubwa nchini. Moyo wake ulifurahi mno, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea, wakati mwingine alihisi yupo ndotoni.
“Latifa…” aliita waziri, bwana Kibonde.
“Ndiyo mheshimiwa.”
“Umeliletea sifa taifa hili, japokuwa Wamarekani wamekuwa wakikung’ang’ania lakini utaendelea kuwa Mtanzania,” alisema bwana Kibonde.
“Nashukuru sana! Ninajisikia kupendwa, ninapenda na kuvutiwa kwa kila kitu kinachotokea katika maisha yangu, kama nilivyowasaidia watu wengine, ningependa niwasaidie na Watanzania pia,” alisema Latifa huku akiachia tabasamu.
“Mama yupo hai?”
“Hapana! Alifariki miaka mingi iliyopita baada ya kuugua Ugonjwa wa UKIMWI, niliambiwa kwamba alikuwa mlevi mno,” alijibu Latifa na kubaki kimya, machozi yakaanza kumlenga.
“Pole sana! Na vipi baba?”
“Sijajua yupo wapi, nahisi amekwishakufa!”
“Kwa nini uhisi?”
“Sikuwahi kumuona, niliambiwa na baba yangu mlezi kwamba baba alimfukuza mama baada ya kugundua kwamba alikuwa mjauzito, tena hapo ni baada ya mama kufukuzwa nyumbani na wazazi wake kisha alikuwa na mimba ya mtu mweusi,” alisema Latifa.
“Pole sana! Kwa hiyo hujui kama baba yako yupo hai au la?”
“Sijui chochote kile.”
Waliendelea kuzungumza ndani ya gari, Dominick ambaye naye alipewa heshima kubwa alikuwa ndani ya gari hilo, hakuzungumza chochote kile, alibaki kimya huku masikio yake yakiwa makini kusikiliza na ubongo wake kuwa makini kukariri.
Safari ile iliendelea mpaka walipofika katika Hoteli ya Kilimanjaro, wakateremka na kisha kuingia ndani. Hakukuwa na wateja wengi, wale waliokuwepo, walitakiwa kubaki haohao na hata wale waliotaka kupanga hotelini, hawakuruhusiwa mpaka Latifa atakapoondoka.
Ratiba ilikuwa imekwishapangwa, Latifa alitakiwa kukaa hapo hotelini mpaka kesho yake ambapo angechukuliwa na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, huko, angefanya ziara ya kuzungukazunguka kwa wagonjwa kisha baadaye kupelekwa katika Hospitali ya Mwananyamala na mwisho kabisa kuitwa katika Kituo cha Televisheni cha Global.
Mawazo juu ya Dominick hayakuisha, picha ya mtu huyo ilikuwa ikimjia kichwani, alimpenda mno, hakutaka kumwambia ukweli kwani alikumbuka maneno aliyomwambia nchini Senegal kwamba asije siku akamwambia kwamba alikuwa akimpenda.
Usiku ulikuwa mrefu, alibaki akiwa amekumbatia mto tu huku mwili wake ukianza kumtetemeka, hakuwa na hamu ya kuwa na mwanaume mwingine, aliyekuwa akimtaka kipindi hicho alikuwa Dominick tu.
Baada ya kukaa mpaka saa saba usiku, Latifa akashindwa kuvumilia, alichokifanya ni kuchukua simu yake na kwenda sehemu ya majina, akaanza kulitafuta jina la Dominick.
“Mungu! Naomba anielewe,” alisema Latifa.
Alipoliona jina la Dominick, hapohapo akapiga namba hiyo na simu kuanza kuita. Wakati ikiwa inaita, mwili wake ukaanza kumtetemeka, japokuwa kulikuwa na kiyoyozi kilichokuwa kikifanya kazi lakini kijasho chembemba kikaanza kumtoka.
“Hallo!” aliita Dominick kwenye simu.
“Hallo Dominick, naomba uje chumbani,” alisema Latifa kwa sauti ndogo.
“Kuna nini?”
“Wewe njoo tu!”
“Kuna amani lakini?”
“Ipo, tena nyingi tu, naomba uje,” alisema Latifa.
“Sawa!” alijibu Dominick na kukata simu.
Moyo wake ukapoa, akajisikia amani moyoni mwake, muda huo, usiku huo ulitulia alikuwa akimsubiri mwanaume aliyekuwa na mapenzi naye, Dominick afike chumbani humo.
Mara akasikia mlago ukigongwa, akashusha pumzi ndefu, akasimama na kuanza kuufuata mlango, alivalia nguo laini ya kulalia iliyoyafanya maungo yake kuonekana vilivyo, akaufuata mlango na kuufungua, alipomuona Dominick tu, mapigo ya moyo wake yakaanza kuongeza kasi, akahisi kama moyo ungeweza kuchomoka.
“Karibu,” Latifa alimkaribishaDominick.
“Ahsante.”
Dominick akaingia ndani, yeye mwenyewe alichanganyikiwa, vazi alilovaa msichana huyo lilimuweka kwenye wakati mgumu, kila kitu maungoni mwake kilionekana wazi, wazimu ukampanda, kila alipojitahidi kujikaza kiume, akashindwa kabisa.
“Umependeza,” alisema Dominick, alishindwa kuvumilia, japokuwa lilikuwa ni vazi la kulalia tu lakini akakosa maneno, akaona bora asifie hivyohivyo tu.
“Na hili vazi?” aliuliza Latifa.
“Ndiyo! Koh koh koh…u mzuri sana Latifa,” alisema Dominick na kujikoholesha, akili yake ilihama, alichokuwa akikifikiria ni mapenzi tu.
“Nashukuru!”
Latifa alifikiri kazi ingekuwa kubwa, alijipanga vilivyo lakini mara baada ya Dominick kuingia humo ndani, akagundua kwamba kazi ilikuwa nyepesi mno, hata kumsukuma mlevi katika mteremko wa mlima ilikuwa ngumu.
Alichokifanya Latifa ni kumsogelea Dominick pale alipokaa, kabla mwanaume huyo hajajiandaa, akashtukia akivamiwa na Latifa, mwisho wa siku wakajikuta wakiangukia kitandani, kilichoendelea, kilichotokea, hakukuwa kingine zaidi ya sauti ya kitanda na mihemo ya mahaba kusikika tu.
Asubuhi kila mtu alikuwa hoi, hawakulala usiku kucha, walikesha huku wakibusiana huku na kule. Baada ya kuamka, ilipofika saa moja na nusu wakaletewa kifungua kinywa na kuanza kunywa.
Walifanyiana mapenzi ya njiwa, walilishana, walibusiana na kukumbatiana, muda mwingi Dominick alikuwa akimpakata Latifa na kumbusu kadiri alivyoweza.
“Siamini,” alisema Dominick.
“Huamini nini?”
“Eti na mimi nimelala na bilionea!”
“Haha! Hebu acha maneno yako kipenzi, niite Latifa tu jamani, hilo bilionea, wala silipendi kuitwa na mtu kama wewe,” alisema Latifa kwa sauti laini, ya mahaba, yenye kumtoa nyoka pangoni, sauti iliyozitetemesha ngoma za masikio ya Dominick.
Ilipofika saa mbili na nusu wakapigiwa simu na kuambiwa kwamba muda ulikuwa umefika hivyo walitakiwa kuanza ziara ya kuelekea katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Wakajiandaa na walipomaliza wakatoka ndani na kuelekea mapokezi ambapo huko wakakutana na dereva wa waziri ambaye akawachukua na kuanza kwenda huko huku wakitangulizana na Waziri Kibonde ambaye walimkuta garini.
Hawakuchukua muda mrefu, wakafika katika hospitali hiyo na moja kwa moja kuanza kile kilichokuwa kimempeleka nchini Tanzania. Kila alichokifanya, Dominick alikuwa akikichukua kwa kamera yake, bado alikuwa kwenye utengenezaji wa makala yake.
Baada ya kuzunguka huku na kule, kuwaona wagonjwa waliokuwa wakiteseka vitandani, Latifa akatoa msaada wa kiasi cha shilingi milioni mia tano ili kisaidie katika ununuaji wa dawa na kujenga maabara nyingine hospitalini hapo. Walipomaliza, wakaelekea katika Hospitali ya Mwananyamala, huko, alifanya kama alivyofanya Muhimbili na kuahidi kutoa kiasi kama kile kwa ajili ya utengenezaji wa maabara na kunua dawa kwa ajili ya wagonjwa katika hospitali hiyo.
“Tunashukuru kwa kila kitu. Nini kinafuata?” alisema Waziri Kibonde na kuuliza.
“Ahsante kwa kila kitu pia, tunatakiwa kwenda kwenye Kituo cha Televisheni cha Global kwa ajili ya mahojiano, baada ya hapo, nadhani tutakwenda kupumzika,” alisema Latifa.
“Sawa! Ila kuna kitu.”
“Kipi?”
“Rais amenipigia simu, amesema kwamba umealikwa ikulu kwenye chakula cha usiku na familia yako,” alisema waziri.
“Unasemaje?”
“Ndiyo hivyohivyo! Umealikwa.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Ikulu?”
“Hapohapo mjengoni.”
Latifa hakuamini, kile alichokuwa ameambiwa hakutarajia kukisikia. Leo hii aliambiwa kwamba alihitajika kwenda ikulu, hakuamini, msichana aliyekulia kwenye maisha ya kimasikini, leo hii alikaribishwa ikulu, kwake ilikuwa ni faraja tele.
“Nimefurahi, nitakuja,” alisema Latifa

Bi Rachel alikuwa na furaha tele, kila alipomwangalia Latifa ambaye alifika nchini Tanzania kwa ajili ya ziara yake ya kuwatembelea Watanzania wengine, moyo wake ukafarijika mno.
Kila wakati alikuwa akitazama televisheni, alimkumbuka msichana huyo, aliishi naye, yeye ndiye aliyempeleka nchini Marekani ambapo huko alisoma na binti yake, Dorcas, leo hii, yule Latifa masikini, mtoto aliyezaliwa na mwanamke mnywa gongo alikuwa maarufu duniani, tena mwenye fedha nyingi.
Baada ya Latifa kutembelea hospitali hizo, akapigiwa simu na msichana huyo na kumwambia kwamba alitakiwa kujiandaa kwani walitakiwa kuonana katika Ofisi za Kituo cha Televisheni cha Global kwa ajili ya kuzungumza mengi.
Bi Rachel alifurahi kusikia hivyo, akahisi kuthaminiwa zaidi ya mtu yeyote yule. Alichokifanya ni kuwasiliana na mzee Issa, na bi Semeni ambao hao ndiyo waliomlea Latifa kule Manzese, ila katika kipindi hicho, hata nao maisha yao yalikuwa mazuri hasa mara baada ya Latifa kuwa bilionea.
Wakafika katika jengo la kituo hicho cha televisheni na kuanza kumsubiria. Wafanyakazi wa kampuni hiyo walipoambiwa kwamba watu hao waliokuja walikuwa ndegu zake na Latifa, walijisikia wivu sana kwa kuona walikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na bahati kubwa maishani mwao.
Ilipofika saa sita mchana, gari la kifahari likaanza kuingia katika eneo la kituo hicho, mlango ukafunguliwa na Latifa kuteremka, akaanza kutembea kuelekea ndani ya jengo hilo. Alipoingia ndani na kuwaona ndugu zake, kwa futaha akawakimbilia na kuwakumbatia, machozi ya furaha yakaanza kumtoka.
“Nashukuru sana mama, nashukuru sana mama kwa msaada wako, bila wewe, nisingekuwa hapa,” alisema Latifa huku akiwa amemkumbatia bi Rachel.
“Usijali Latifa, nilifanya yote kwa kuwa nilihisi kukusaidia,” alisema bi Rachel.
Wafanyakazi wote waliokuwa mahali hapo wakaanza kuwaangalia watu hao, kumuona Latifa katika ofisi zao walijisikia fahari sana, wengine wakachukua nafasi hiyo kupiga naye picha na kuzirusha mitandaoni.
Baada ya kumaliza ishu ya kupiga picha na wafanyakazi, akaitwa katika chumba kimoja ambacho kilikuwa maalumu kwa ajili ya kufanya interview ambayo ingerushwa moja kwa moja kwenye televisheni.
“Karibu Latifa,” alikaribishwa.

itaendelea.

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

إرسال تعليق

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.