Notification texts go here Contact Us Buy Now!

NISAMEHE RATIFA SEHEMU YA 12

NISAMEHE RATIFA 12


Huo ulikuwa mwanzo wa ukaribu wao, wawili hao, Latifa na Liban walikuwa pamoja kila sehemu walipokuwa. Walisoma darasa moja huku kila walipokuwa wakiingia darasani, walikaa karibukaribu hali iliyoyafanya wanaume wote kugundua kwamba wawili hao walikuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Hiyo haikuwa kazi nyepesi kwa Liban, ni kweli alimpenda mno Latifa lakini kila alipoingizia suala la uhusiano wa kimapenzi, Latifa hakutaka kukubaliana naye, bado maumivu ya Ibrahim yaliendelea kukumbushwa moyoni mwake.
Siku ziliendelea kukatika, Liban hakutaka kusikia wala kuelewa, kila alipoambiwa sitaki, hakukata tamaa, aliendelea kumwambia zaidi mpaka Latifa akachoka na mwisho wa siku, bila kulazimishwa, akajikuta akianzakubusiana na kijana huyo na hatimaye midomo yao kugusana, kilichofuata ni kubadilishana mate tu.
“Ninakupenda Latifa,” alisema Liban, alimkazia macho msichana huyo, hisia kali za kimapenzi zilionekana machoni mwake.
“Ninakupenda pia, lakini…..”
“Lakini nini?”
“Naomba usiniumize,” alisema Latifa kwa sauti ya chini.
“Siwezi kufanya hivyo, siwezi kukufanya kama huyo mpumbavu,” alisema Liban huku akiachia tabasamu pana.
Liban akawa mtu mwenye bahati mno, wanaume wengi chuoni hapo UCLA walijaribu kumfuatilia Latifa lakini mwisho wa siku walikataliwa katakata, kitendo cha Liban kumchukua kulikuwa na wanaume wengi walioumia.
Latifa hakutaka kuliacha penzi la Liban, kwa kipindi kichache alichokuwa naye alimfanya kujisikia amani moyoni mwake, ile furaha ya mapenzi ambayo watu wengi walikuwa wakiizungumzia, ikaanza kuingia moyoni mwake.
Siku zikaendelea kukatika, mpaka mwaka huo unakatika na mwaka mwingine kuingia, wawili hao waliendelea kuwa pamoja huku kila mmoja akimpa mwenzake ahadi ya kuoana na kuishi pamoja.
Mwaka wa pili ulipomalizika, wakati wa likizo ndipo Liban akamwambia Latifa kwamba angependa aende naye nchini India kwa ajili ya kuwaona wazazi wake na hatimaye waweze kufunga ndoa kwani umri ulikuwa unaruhusu.
Latifa hakuamini, hakumkatalia Liban, walikuwa wamebakiza mwaka mmoja tu wamalize chuo hivyo hiyo ikaonekana kuwa nafasi yake kujiandaa kwa ajili ya ndoa, baada ya wiki moja, wakapanda ndani ya ndege na kuelekea India.
Safari kutoka nchini Marekani mpaka India ilichukua masaa ishirini na saba ndipo ndege ilipoanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Indira Gandhi uliokuwa katika Jiji la New Delhi. Ndege iliposimama, abiria wakaanza kuteremka na kuelekea nje ya uwanja huo na kwenda kuchukua mizigo yao.
“Uliwaambia wazazi wako kuhusu mimi?” aliuliza Latifa huku uso wake ukitawaliwa na tabasamu pana.
“Hapana, ila niliwaahidi kwamba nitawafanyia sapraizi.”
“Mmmh!”
“Usiogope kipenzi, wewetwende tu, watafurahi sana mana’ke walinisisitiza sana kuhusu kuoa,” alisema Liban huku akionekana kuwa na furaha tele.
Walipofika nje ya uwanja huo, wakachukua teksi na kuanza kuelekea katika Mtaa wa Aurangzeb uliokuwa hapo New Delhi, mtaa uliokaliwa na matajiri wakiwepo waigizaji kama Aksey Kumar na Sunil Shetty.
Kutokana na wingi wa magari na Bajaj barabarani, walichukua nusu saa mpaka kufika katika mtaa huo. Teksi ikaelekea mpaka kwenye nyumba moja ya kifahari na kuanza kupiga honi, geti likafunguliwa na gari kuingizwa.
Wasichana wawili waliokuwa ndugu zake Liban wakalikimbilia gari hilo kwani walikuwa na taarifa kwamba kaka yao angefika nyumbani hapo siku hiyo.
Nyuso zao zilikuwa na tabasamu pana, hawakuamini kama kaka yao angefika siku ile nyumbani pale kutokea nchini Marekani alipokuwa akisoma. Walishindwa kuzizuia furaha zao, walipomuona akiteremka kutoka garini, wakamsogelea na kumkumbatia kwa furaha.
Hapohapo, mlango wa upande wa pili ukafunguliwa na Latifa kuteremka, hawakuonekana kushtuka kwa kuhisi kwamba yule hakuwa mgeni wao kwani teksi ile ilikuwa imekodiwa na Wahindi walikuwa na tabia ya kukodisha teksi moja zaidi ya watu watatu kutokana na idadi kubwa ya watu.
Wakamwangalia Latifa huku tabasamu yakiendelea kuwepo nyusoni mwao. Liban akaona kwamba hiyo ndiyo ilikuwa nafasi pekee ya kumtambulisha Latifa hata kabla hawajaingia ndani.
“Is she with you?” (Yupo pamoja nawe?) aliuliza dada mmoja.
“Yeah! She is my fiancee,” (Ndiyo! Ni mchumba wangu) alisema Liban huku akiwa na tabasamu pana.
“What do you say?” (Unasemaje?) aliuliza dada mmoja huku akijifanya kutokusikia kile kilichokuwa kimesemwa na Liban. Hivyo akarudia.
Hapohapo, tabasamu yakatoka nyusoni mwao, wakaanza kumwangalia Latifa kwa macho ya chuki, hawakuvutiwa naye hata mara moja. Liban akaligundua hilo, alichokifanya ni kumsogelea Latifa na kumvutia kwake kwani hakutaka ajisikie vibaya juu ya kilichokuwa kikiendelea.
“She is slut..” (Ni mwanamke mchafu..) alisema dada mwingine.
Mpaka kufikia hapo, hakukuwa na kitu cha kuficha kwamba Latifa hakuwa akihitajika ndani ya familia hiyo. Maneno yale yalimchoma mno lakini hakutaka kuonekana kama alichomwa sana, hivyo akaanza kulilazimisha tabasamu usoni mwake.
Hata nguvu za kuchukua begi lake hakuwa nazo, ni Liban ndiye aliyelichukua na kuanza kuelekea ndani. Si dada wale tu waliokuwa wakimchukia Latifa bali kila alipoonekana na watu ndani ya nyumba ile, alikuwa akichukiwa mno, hakupendwa hata kidogo.
Hakupokea mapokezi yale aliyoambiwa kwamba angepewa, mapokezi yale yalikuwa ni ya tofauti sana na maneno ya Liban, akabaki akisononeka moyoni mwake huku akitamani kurudi nyuma na kuondoka.
“Liban. Huyu ni nani?” aliuliza mama yake Liban, alikuwa amemvuta mtoto wake pembeni, japokuwa aliamini kwamba alizungumza kisiri, lakini Latifa aliweza kuyasikia maneno yale.
“Ni mchumba wangu.”
“Hapana. Huyu si mchumba wako, toka lini umeona ndugu zako wakioa wanawake wenye mchanganyiko? Hawa ni wachafu. Haiwezekani, huwezi kuwa na mwanamke mchafu. Mimi kama mama yako, nakwambia simtaki huyu mwanamke, hii ni laana,” alisema mama yake Liban.
“Lakini mama…”
“Nimesema simtaki…” mama Liban alisema kwa sauti kubwa kabisa.
Liban hakuwa na nguvu, alimheshimu sana mama yake na alimuahidi kwamba isingeweza kutokea hata siku moja akamvunjia heshima yake. Kitendo cha kuambiwa kwamba hakuwa akimtaka Latifa kuingia katika familia yao, kilimuuma sana.
Alichokifanya ni kuwapigia simu ndugu zake wengine ili waje wamwambie mama kwamba Latifa alikuwa ni chaguo lake. Kitu cha ajabu, kila ndugu aliyefika mahali pale na kumuona Latifa, hakumtaka, hawakutaka kumuona kabisa Latifa.
“Ni mwanamke mchafu, unatuletea laana kwenye ukoo,” alisema mjomba wake ambaye alimuamini kwamba alikuwa pamoja naye kwa kila kitu.
Ilikuwa ni afadhali kupigwa na risasi au kuchomwa moto, maumivu aliyoyasikia Latifa yalikuwa makubwa mno. Akajikuta akilengwa na machozi na hatimaye kuanza kububujika mashavuni mwake.
Alitamani kupotea ghafla kama mchawi na hatimaye kuibukia Tanzania, hilo halikuwezekana, kila ndugu aliyefika mahali pale, hakumtaka Latifa, sababu kubwa ikiwa ni mchanganyiko wa rangi, aina ya watu ambao walitengwa mno nchini India.
“Kwa nini mimi Mungu?” alijiuliza Latifa huku akianza kulia kama mtoto.

Latifa alitia huruma, kila muda Liban alipokuwa akimwangalia, alitamani kulia, hakukuwa na siku ambayo alimuonea huruma mtu kama siku hiyo. Moyo wake ulimpenda mno msichana huyo, kwake, alikuwa kama pumzi, alikuwa tegemeo kubwa mpaka kumpa ahadi kwamba angemuona na kuwa mama wa watoto wake, lakini mwisho wa siku, ndugu, na watu wengine wa karibu hawakumtaka msichana huyo.
Alitamani kubadilisha matokeo, ndugu zake wakubaliana naye na kuondokana na dhana potofu kwamba Latifa alikuwa na laana kutokana na mchanganyiko wake wa rangi. Ndugu wale hawakutaka kunyamaza, bado waliendelea kulalamika kwamba Liban hakutakiwa kuwa na mwanamke kama Latifa.
Latifa hakutaka kuendelea kubaki nyumbani hapo, alichokifanya ni kusimama, akachukua mabegi yake na kuondoka nyumbani hapo. Kitu kibaya ambacho kilimshangaza sana ni kwamba Liban hakuweza kumfuata, yaani ni kama mwanaume huyo alikubaliana na wazazi wake.
“Ninawachukia watu wa nchi hii,” alisema Latifa huku akilia kama mtoto.
Alitembea barabarani huku kichwa chake kikiwa chini, machozi yalikuwa yakimbubujika, kadiri alivyojitahidi kuyafuta, hayakukata, yaliendelea kutoka zaidi na zaidi. Safari yake hiyo ikaishia mbele ya hoteli kubwa ya Mumbai, hapo ndipo alipoamua kuchukua chumba, hakutaka kukaa sana, akapanga kuondoka kurudi Tanzania siku inayofuata.
****
Mapenzi yalikuwa motomoto, Ibrahim na Nusrat walijiona kuwa miongoni mwa wapenzi waliokuwa wakipendana kwa dhati kuliko watu wowote wale katika dunia hii. Muda wote walikuwa pamoja, walitaniana na kubusiana kila walipokuwa.
Kila mmoja kichwa chake kilifikiria ndoa tu, walipita vizingiti vingi vya wazazi, ndugu, jamaa na marafiki na mwisho wa siku, wote hao walikubaliana waache na hatimaye waweze kufunga ndoa na kuishi pamoja.
Kwa Ibrahim, furaha iliongezeka zaidi, kila alipokuwa akikaa, alimfikiria msichana huyo ambaye kwake alionekana kuwa kila kitu. Baada ya siku kadhaa kupita, Ibrahim akajikuta akianza kuwa karibu na mwanaume mmoja, alionekana kuwa mzee wa makamo, alikuwa na ndevu nyingi zilizokuwa na mvi, alionekana kuchoka hali iliyoonyesha kwamba maisha yalimpiga sana.
Alikutana na mzee huyu wakati akielekea Posta kwa ajili ya kukamilisha michoro yake ambayo alitakiwa kumkabidhi Balozi wa Uingereza kama zawadi pekee kutoka kwa Watanzania kabla ya kuelekea nchini mwake.
Alipokutana na mzee huyo aliyekuwa ombaomba barabarani, akajikuta akifunga breki na kuteremka. Hakujua sababu iliyomfanya kuwa na huruma kiasi hicho, alionekana kuvutiwa na mzee yule, akaufungua mlango na kuanza kumfuata.
“Naomba unisaidie hela ya kula,” alizungumza mzee yule, mavazi yake yalikuwa yamechakaa sana.
“Chukua hii,” alisema Ibrahim huku akimkabidhi mzee yule noti ya shilingi elfu kumi.
Hakutaka kukaa sana, ndani ya gari, alikosa amani, kila wakati alikuwa akimfikiria mzee yule ambaye kwake alionekana kuwa na uhitaji mkubwa. Hakutaka kuficha hisia zake, akampigia simu Nurat na kumwambia kuhusu mzee huyo

itaendelea.

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.