MOYO ULIOJAA MAUMIVU
SEHEMU YA 41
“Iyanya...” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja kutoka kwenye gari moja la kifahari, Hummer nyekundu iliyokuwa imepaki pembeni ya duka moja la nguo lililokuwa Johannesberg nchini Afrika Kusini.
“Who are you?” (nani wewe?) aliuliza msichana aliyeitwa.
“Your Instagram friend! I liked your pictures yesterday and you connected me in you live video, do you remember me?” (Rafiki wako wa Instagram! Nilizipenda picha zako jana na uliniunganisha kwenye ile video ya moja kwa moja) alijibu mwanaume huyo.
Iyanya akasimama na kumwangalia mwanaume huyo, alikuwa chotara, mwenye asili ya Kiswahili na Kiarabu. Mwili wa Iyanya ukasisimka, alimwangalia mwanaume huyo, alikuwa mzuri wa asili.
Haraka sana akateremka kutoka ndani ya gari na kumsoegelea msichana huyo, alipomfikia, akamsalimia kwa kumpa mkono. Iyanya alipogusana naye tu akahisi mwili wake ukisisimka kupita kawaida.
Ni kweli aliwahi kukutana na wanaume wengi, alilala nao kitanda kimoja lakini wa siku hiyo alikuwa balaa, alikuwa mzuri kupita kawaida na kila alipomwangalia, moyo wake ulimwambia ni lazima kuzaa naye.