*1*. *Siku moja utastaafu*👴🏿👵🏿.
Hautakua ukienda kazini,hautakua na madaraka tena,hautakua/utapungukiwa na nguvu ya ushawishi,mzunguko wako wa pesa utapungua❌💱!
Chunguza/fuatilia 🧐 tarehe yako ya kustaafu kwenye risiti yako ya malipo ya mshahara🧾.
*2*. *Tumia siku zako za Likizo ya Mwaka*.📅
Chochote utakachokifanya Likizo ndio utakachokifanya ukistaafu.Kama unatumia likizo kulala 😴au kuagalia Luninga📺 ndicho utakachokifanya ukistaafu.Tumia wakati wako wa ziada kujifunza kitu👩🏿🏫,kitakuja kuwa na manufaa ukistaafu.
*3*. *Wekeza kwa ajili ya kustaafu kwako💰*.
👨👩👧👦Watoto wako sio uwekezaji kwa ajili ya kustaafu kwako.Usiwategemee watoto/ndugu/ marafiki kama benki yako🏧. Utapoteza heshima na utu wako😔.
*4.Tafuta shughuli unayoipenda/unaifurahia* wakati bado upo kazini ikuongozee katika kustaafu kwako mfano kufuga kuku 🐥🐓au miliki duka🏦.
📚Pata ujuzi unaojiuza (📄sio vyeti visivyo na matumizi)
*5.Utastaafia wapi*.
Jijengee nyumba.
🙅🏿♂Usistaafu ukiwa bado unapanga nyumba🏠.
🙅🏾Usigome kutoka kwenye nyumba ya serikali🏠.
*6.Ni nani watakua wategemezi wako*.
Wakati unastaafu watoto👨👩👧👦 wako wanatakiwa wawe wamevuka miaka 18 na wanajitegemea wenyewe👩🏾🌾👮🏾♀👩🏾⚕👷🏿👨🏾🍳👨🏿🏫👨🏿💻👨🏿🔧👨🏾✈.
*7.Usistaafu na ukaendelea kukaa katika jiji kubwa*
labda endapo unajimudu kweli kweli💪🏾
Utakua na vyanzo vya fedha hafifu na itakuwia vigumu❌💱.
Ikiwezekana Hamia mahali penye gharama ndogo za maisha ili 💵pensheni yako ikusogeze mbali kidogo.
*8.Miliki mali inayoweza kukodishika au inayoweza kubadilika na kuwa Fedha taslim*
Miliki hisa zinazokunufaisha📈⚖.
Panda Miti ya biashara mfano mirunda🌳, mitiki🌳 nk, Fuga🐓🐐🐑🐖🐄, lima mboga mboga🍆🥬🥒🥕.
Shughuli hizi zitakuingiza mapato💵 pamoja nakukufanya uwe mwenye afya💪🏾.
*9.Ishi maisha ya kawaida (maisha yasio na makuu🍕🍔🍟🍻)*
Kama hujajenga nyumba kijijini kwenu,
❌🏠usitumie pesa ya wastaafu kujenga,si busara kufanya hivyo, labda kama utageuza kijiji makazi yako ya kudumu📌.
*Tambua kwamba wastaafu wengi wanafariki 🚑mapema sababu ya mambo yafuatayo:-*
1.Hawajajiandaa🏋🏾🏋🏾♀ kiakili kustaafu.
2.Kukosa vipato❌💵.
3.Msongo wa mawazo🥺
4.Wanapatwa na shinikizo la juu la damu/kisukari kutokana na 😟wasiwasi,😣uoga n a sintofahamu nyingi🤔
*👨🏿💻MEZA YAKO PALE KAZINI SIO YA KUDUMU.🧰JIPANGE KWA AJILI YA KUSTAAFU.*