*Kama wewe ni mlevi*, Jifanye kama unajikuna halafu piga hesabu zifuatazo........
Tufanye unakunywa bia 5 kwa siku yenye ujazo wa 350ml hivyo kwa siku unakunywa mililita 1750. Hivyo kwa mwezi unakunywa 1750x30 sawa na 52500ml sawa na Lita 52.5 za pombe. Kwa mwaka unakuwa umekunywa 52.5x12 sawa na lita 630. Pipa lina lita 200, hivyo kwa mwaka utakuwa umekunywa pipa 3.3 za pombe. Tufanye umeanza kunywa ukiwa na 20yrs mpaka 50yrs ndiyo ukaokoka hivyo kwa miaka 30 ya kunywa utakuwa umekunywa Pipa 93 halafu unaposhikwa na kisukari unalalamika umerogwa na shemeji yako kumbe umebeba sukari kwenye mapipa 93poleee,
Jitafakari ndugu