*Ukiona mtaani gari zimeandikwa ktk PLATE NAMBA kama ifuatavyo usiumize kichwa jua ni hivi:*
1. *NGAO* -Rais, makamu wa Rais na Waziri Mkuu
2. *S* -Spika wa bunge
3. *JM* - Jaji mkuu
4. *JR* - Jaji wa mahakama ya rufaa
5. *JK* - Jaji Kiongozi
6. *J* - Jaji wa mahakama kuu
7. *XXXX* -Mkuu wa majeshi(CDF)
8. *CAG* -Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali
9. *CS* - Katibu mkuu kiongozi
10. *W* mwanzoni inaashiria waziri kisha kifupi cha wizara yake hufuata
11. *NW* -Naibu waziri
12. *DFP* -Donor's Fund project
13. *ST* -Serikali ya Tanzania kisha herufi nyingine hufuata
14. *SMZ* -Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar
15. *PT* -Police of Tanzania
16. *SM* -Serikali za mitaa
17. *CD* - Magari ya ubalozini
18. *SU* -Shirika la Umma.
19. *JW* -Jeshi la Wananchi
20. *MT* -Magereza Tanzania
21. *CGP* -Commissioner General of Prison(Mkuu wa Magereza)
22. *KUB* - Kambi ya upinzani Bungeni
*NB* Gari nyingine za umma zina namba zaidi ya moja kwa kazi maalum
*NYONGEZA:*
Gari za biashara zina plate number nyeupe na zile za matumizi binafsi plate number ya njano.
Hii hapa video inayoelezea namba hizo kwa kina zaidi