______________________________________
*waume wengi mnayo twabia hii utamkuta mkeo kakuandalia nguo za kuvaa kakupasia kafukiza kama ni udi au pafyum mashaallah*
____________________________________
*mwanamume akiingia chumbani utamsikia ah nguo gani hizo umeweka mi sizitaki nyoosha hii na ile subhaanallah mwanaume wewe jua ulioa tu lakini hujielewi wala hujitambui*
____________________________________
*hivi we mwanamume hujui kuwa mkeo ndie kioo chako?*
*hujui kuwa mkeo ndie mtu pekee wa kukukagua?*
*hujui kuwa mkeo ndie mtu pekee asietaka usipendeze?*
*hujui kuwa mkeo ndie mtu pekee anejali muonekano wako?*
*hujui kuwa mkeo ndie mtu pekee ane furahi ukipendeza?*
*hujui kuwa mkeo ndie mtu pekee ane pata faraja ukisifiwa?*
____________________________________
*mwanaume wewe acha kuwa mtawala kwenye ndoa yako mpe uhuru mkeo kwenye mwili wako hata akikwambia nguo hii siipendi basi mridhishe hayo ndio mapenzi msijue mapenzi ni kitandani tu laa hassha wakallah*
___________________________________
*ziko nyingi twabia mbaya ila leo hiyo yatosha muhimu kuyafanyia kazi lengo na madhumuni ni kuzilinda na kuzijenga ndoa zetu zipate dumu na ziwe salama kwa uwezo wa Allah swt*
__________________________________