*♦Tendo la ndoa ni kitu ambacho watu hudhani kuwa kinatakiwa kufanywa usiku. Naam, unaweza kufanya tendo la ndoa muda wowote, lakini ukweli ni kwamba kulifanya tendo la ndoa usiku tu inaweza kutengeneza uchoshi kwa wanandoa.
FAIDA ZA TENDO LA NDOA LA ASUBUHI
Bila shaka utafurahi ukijua kwamba tendo la ndoa la asubuhi (kiamshio) sio tu kwamba ni jambo zuri, bali pia litakusaidia kimwili, kiakili na kiroho. Famasia yako ya Ndoa inakuletea baadhi ya sababu za umuhimu wa kufanya tendo hilo asubuhi mara kwa mara:
*1. URAHISI NA WEPESI:*
Wengi wetu tunapenda kulala kwa kujinafasi, huku tukiwa na nguo kidogo mwilini. Wengine hulala bila nguo kabisa, na nilieleza faida zake katika somo la FAIDA ZA KULALA BILA NGUO. Tendo la ndoa la asubuhi hukufanya usihitaji kuvua nguo, jambo ambalo kwa nyakati nyingine itakulazimu kuvua mzigo wa nguo.
Aidha, tendo la ndoa la asubuhi huwafanya mnapoingia bafuni kujisikia raha na ladha ya kipekee.
*2. UBORA:*
Tendo la ndoa la asubuhi ni bora kuliko wakati mwingine kwa sababu kadhaa. Mosi, nishati, utuvu na utulivu wa kiasili huwafanya kuwa na stamina kubwa ya kufanya vizuri na kuwafikisha kileleni kwa raha ya aina yake. Wanandoa wanaofanya tendo usiku kwa kawaida huwa wamechoka kutokana na shughuli za kutwa nzima, na hivyo kufanya viungo vyao kuwa na mwitikio mdogo wa kimahabba.
Pili, dakika chache baada ya kuamka, akili yako inakuwa bado haijaamka, na hivyo inakuwa haijakutana na mambo mengi. Matokeo yake, jambo hilo linaweza kukufanya kuwa kama bepari wa mahabba kitandani.