Notification texts go here Contact Us Buy Now!

MOYO ULIOJAA MAUMIVU SEHEMU YA 36

MOYO ULIOJAA MAUMIVU

SEHEMU YA 36

Maumivu aliyokuwa ameyapata yalikuwa ni mara tano ya yale ambayo angeyapata mke wake. Aliumia, hakutamani kuona mke wake huyo akiumia kama atakavyoumia, alitamani kuona akiishi maisha ya furaha, yasiyokuwa na maumivu hata kidogo.

Siku ya kwanza ikapita, Theo hakuondoka hospitalini, taarifa zilianza kuzagaa mitandaoni kwamba Violeth alijifungua usiku uliopita lakini hakukuwa na mtu aliyepata taarifa kuwa mtoto mmoja alifariki dunia.

Theo hakutaka kumtaarifu mtu yeyote yule, na hata alipoongea na ndugu zake aliwaambia kwamba alijifungua salama kabisa. Alihitaji kumuona mke wake akifumbua macho na kuzungumza naye, ampe taarifa hiyo ili wajue ni kwa namna gani wangewaambia wananchi.

Siku hiyo ndiyo ambayo Violeth alipoyafumbua macho yake kitandani pale. Alionekana kuchoka mno, kitu cha kwanza kilichokuja kichwani mwake ni watoto wake, alijua alijifungua, alihitaji kuwaona wote wawili.

Akaangalia pembeni, kulikuwa na mtoto mmoja wa kike, lakini upande mwingine hakukuwa na mtoto. Haraka sana Theo akasimama na kumfauata mke wake mahali pale.

“Mume wangu! Nimejifungua....tumepata watoto mapacha mume wangu...wa kiume ataitwa Harry na wa kike ataitwa Rachel...” alisema Violeth kwa sauti ya chini, hakujua kilichotokea, badala ya Theo kumjibu, machozi yakaanza kumtoka hali iliyoanza kumtisha Violeth kitandani pale. |
|
|

Je, nini kitaendelea?
Tukutane siku nyingine.

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

إرسال تعليق

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.