Notification texts go here Contact Us Buy Now!

MOYO ULIOJAA MAUMIVU SEHEMU YA 34

MOYO ULIOJAA MAUMIVU

SEHEMU YA 34

Aliishika, aliibeba kana kwamba alikuwa mtoto mzima, alilia huku ikiendelea kuwa mikononi mwake.

Hakujua ni kwa namna gani Mungu aliruhusu maumivu hayo katika maisha yake, alitamani arudishe mishale ya saa nyuma ili kila kitu kianze upya lakini si kupitia maumivu makali aliyokuwa akiyapitia.

“Nitakupenda maisha yangu yote Harry!” alisema Theo huku mwili wa mtoto wake ukiwa mikononi mwake.

Alikaa humo kwa dakika kadhaa, alipomaliza, madaktari wakamwambia kuhusu kumzika mtoto huyo. Hakutaka kufanya hivyo mpaka pale ambapo mke wake angerudiwa na fahamu. Hilo halikuwa tatizo, kulikuwa na jambo jingine ambalo dokta alihitaji sana kuzungumza naye.

Moyo wa Theo ukapiga paa! Hakuamini kama kulikuwa na jambo jingine tena, lilikuwa nini? Kuhusu hali ya mke wake ama?

Hakuwa na jinsi, akaondoka na marafiki zake na kuelekea katika ofisi ya daktari yule na kukaa pamoja.

Alijua kabisa kwamba Theo aliumia moyoni mwake, hakuwa na jinsi, alitakiwa kumwambia ukweli kuhusu jambo jingine, yaani kama kulia, alitakiwa kulia tena lakini si kumruhusu aondoke na siku nyingine amwambie kuhusu tatizo jingine, kilio kingeanza upya.

“Niambie kuna nini? Ni kuhusu mke wangu? Dokta, naomba usinifiche kitu, kama kuumia, nimeumia sana, na kama kulia nimelia sana, naomba uniambie, mimi mwanaume,” alisema Theo japokuwa moyoni mwake alijua hakuwa na moyo wa kuvumilia maumivu makali.
“Ni kuhusu mtoto wako!” alisema dokta.
“Nani? Rachel?”
“Ndiyo!”

“Amefanyaje?” aliuliza Theo, akaishiwa pozi, akabaki pale kwenye kiti huku akili yake ikizidi kuchanganyikiwa.

“Ana tatizo pia!”
“Tatizo gani?”
“Moyo wake umevimba, mishipa yake haina nguvu ya kusukuma damu vizuri,” alijibu daktari kitu kilichoanzisha kilio kingine kabisa ndani ya ofisi ile.

Hilo likawa jambo jingine jipya! Theo alilia sana, aliumia zaidi, hakuamini kile alichokisikia, yaani mtoto wake aliyebaki alikuwa na tatizo jingine tena, moyo wake kuvimba na mishipa yake haikuwa na nguvu ya kusukuma damu.

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.