Notification texts go here Contact Us Buy Now!

MOYO ULIOJAA MAUMIVU SEHEMU YA 27

MOYO ULIOJAA MAUMIVU

SEHEMU YA 27

“Na hiyo harusi itafanyikia hapa au Ufaransa?” aliuliza mwandishi.
“Hapahapa Tanzania!”

Kila walilolisema ndilo lililofanyika kwani baada ya kupita mwezi mmoja, hatimaye Theo na Violeth wakafunga ndoa kwenye Kanisa la St. Joseph lililokuwa jijini Dar es Salaam na watu hao kuwa mume na mke.

Harusi hiyo ilikuwa gumzo, kanisa hilo lilijaza watu wengi, kila mmoja alitaka kushuhudia kilichokuwa kikienda kutokea. Wengi walipiga picha kwa ajili ya kuweka kwenye mitandao yao ya kijamii, waandishi wa habari walikuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha wanapata picha ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea.

Wanandoa hao walikuwa na nyuso za furaha, walimshukuru Mungu kwa kutimiza ndoto walizokuwa wamejiwekea za kufunga ndoa na kuwa pamoja.
Kila mtu Tanzania alikuwa bize kufuatilia harusi hiyo iliyokuwa gumzo kila kona.

Masupastaa wengi duniani walihudhuria, walifurahi na kuona hatimaye yule msichana mrembo, ambaye mpenzi wake alikufa kwenye ajali ya ndege hatimaye alikuwa akiolewa na mwanaume mwenye pesa na maarufu mno barani Afrika.

“She is very beautiful,” (ni mrembo mno) alisema mwanamke mmoja, alikuwa ni Naomi Campbell, mmoja wa wanamitindo maarufu duniani.
|
|
Je, nini kitaendelea?

Kumbuka hii ni miongoni mwa simulizi zinazoumiza na kufundisha mno. Endelea kunifuatilia.

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.