JASTINA
SEHEMU 5
ILIPOISHIA
Alwin alitabasamu kidogo na kumwambia "unaonaje tukashindana yupi atakae maliza mwanzo", "sawa" alijibu Jestina na wote wakakaa chini na kuanza mashindano. "jamani Jestina na Alwin wako wapi" bi Prisca alikuwa alikuwa akiwauliza wafanya kazi ambao hata wao walisema hawajui.
ENDELEA
Bila kuchelewa aliekea kwa Mr Hendrix na kumwambia kuwa Jestina na Alwin hawaonekani, wala hakushtuka sana "usijali ni watoto na hawajotoka ndani ya nyumba,we nenda kapumzike mi nitawatafuta" alisema na kumwambia Mr Kelvin amfuate. Walizunguka nyumba nzima lakini hawakuwaona mpaka wasiwasi ukaanza kuwapata.
Upande wa pili huko mpambao ulikuwa mkali kupita maelezo, kwa sababu ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Alwin kucheza mchezo ule ilikuwa ni vigumu sana kushinda lakini akili yake ilionekana kutokubaliana na kusindwa hivyo alienedele kuminyana na puzzle hio huku kijasho chemba kikimtoka. Wakati wakiendelea kutafuta, wazo lilimjia Mr Hendrix na kumwambia mwenzie waelekee varanda. Walipokaribia tu waliwaona wawili hao wakiwa katika mtanange huo na Mr kelvi alipotaka kuenda kuwashtua Mr Hendrix alimzuia na kutoa simu na kuanza kurikodi pambano hilo.
Kila mpambno ulivyokwenda ulizidi kuwa mkali huku kila mmoja akihakikisha anamaliza mwanzo kuliko mwenzake. Lakini bahati ilikuwa mbaya kwa Jestina baada kushindwa na Alwin ambae ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kupanga puzzle ile. Kwa kweli llilikuwa pigo kubwa kwa Jestina, alianza kulia baada kuona kuwa ameshindwa wakati yeye ndie aliezoea hasa kupanga vibox hivyo. Mr Hendrix alimsogelea na kumbeba mwanae "mbona unalia", "baba kanishinda yule" alijibu huku akimnyooshea kidole Alwin. "kushindwa ni kawaida katika maisha, lakini ipo siku na wewe utamshinda" aliongea huku akimfuta machozi mwanae ambae alianza kutabasamu.
ITAENDELEA