Notification texts go here Contact Us Buy Now!

Jinsi ya Kupika Biryani | Mapishi

Mahitaji ya kupika biriani 1 kilo mchele wa basmati 1 kilo nyama iwe ya kuku au ng'ombe au mbuzi kata katika umbo dogo la kutosha kula kisha ichemshe na tangawizi na kitunguu swaumu, unga wa binzari (turmeric powder) pili pili manga na chumvi ili kuweka ladha nzuri. Ikisha iva itoe iweke pembeni na mchuzi wake uweke pembeni utautumia baadae. 1 kilo ya vitunguu kata slice ( mviringo) 1 kilo nyanya nyekudu zilizoiva, osha vizuri kisha katakata saizi ndogo ndogo sana 1/2 lita ya mafuta ya kupikia 1/2 kilo ya samli au mafuta yeyote ya kupikia 2 maggi chicken soup cubes 3 kijiko kidogo cha chai unga wa pilipili mwekundu 1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa binzari 3 kijiko kidogo cha chai unga wa girigilani (giligilani) 2 kijiko kikubwa cha chakula mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu swaumu vilivyosagwa korosho iliyo kaangwa usizisage zibaki nzima robo kikombe
Kuna aina mbalimbali za upishi wa biriani ambapo mara nyingi hutofautiana kutokana na viungo vinavyotumika katika upishi.

Mahitaji ya kupika birian


  • 1 kilo mchele wa basmati


  • 1 kilo nyama iwe ya kuku au ng'ombe au mbuzi kata katika umbo dogo la kutosha kula kisha ichemshe na tangawizi na kitunguu swaumu, unga wa binzari (turmeric powder) pili pili manga na chumvi ili kuweka ladha nzuri. Ikisha iva itoe iweke pembeni na mchuzi wake uweke pembeni utautumia baadae.


  • 1 kilo ya vitunguu kata slice ( mviringo)


  • 1 kilo nyanya nyekudu zilizoiva, osha vizuri kisha katakata saizi ndogo ndogo sana


  • 1/2 lita ya mafuta ya kupikia


  • 1/2 kilo ya samli au mafuta yeyote ya kupikia


  • 2 maggi chicken soup cubes


  • 3 kijiko kidogo cha chai unga wa pilipili mwekundu


  • 1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa binzari


  • 3 kijiko kidogo cha chai unga wa girigilani (giligilani)


  • 2 kijiko kikubwa cha chakula mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu swaumu vilivyosagwa


  • korosho iliyo kaangwa usizisage zibaki nzima robo kikombe


  • majani ya girigilani kichanga kimoja


  • mbegu za nzima ya hiriki kiasi


  • Pili pili manga nzima kiasi


  • Chumvi kiasi


  • Jinsi ya kuanda biriani

    Weka mafuta katika sufuria yako iliyo juu ya moto tayari, kisha kaanga nyama yako iliyokwisha chemshwa mpaka iwe na rangi ya kahawia (golden brown)

    Kisha itoe nyama hiyo na ichuje mafuta ili mafuta yanayobaki weka kitunguu na endelea kukaanga kwa dakika 7-10 kisha weka unga wa binzali, unga wa pili pili mwekundu, unga wa girigilani, mbegu za hiriki na nusu ya mbegu za pili pili manga.

    Changanya vizuri mpaka utapata mchanganyiko mzuri mkavu miminia humo maji uliyotunza baada ya kuchemshia ile nyama yako na kuiweka pembeni ipoe. kisha weka nyanya fresh ndani ya sufuria yako pika mpaka maji yakauke na mafuta yaanze kuoneka kwa juu ndani ya sufuria.

    Kisha weka nyama yako ndani ya sufuria pole pole halafu punguza moto acha ijipike kwa muda mpaka mchuzi wako na nyama vikamate ladha pia usisahau kuweka chumvi kulingana na ladha unayopenda.

    Chukua sufuria nyingine weka mafuta ya samli na vitunguu ilivyoslice kisha kaanga na majani ya girigilani, korosho funika kwa dakika 10 i, kisha weka mchele wako mkavu uliokwisha oshwa vizuri na uchanganye vizuri ongeza vikombe 5 vya maji na chumvi kidogo mchele ukishaanza kuchemka funika sufuria lako na punguza moto maji yakisha kauka kiasi weka mchanganyiko wa ile nyama yako nusu tu juu ya wali wa basmati acha wali uive kabisa kisha itakua tayari kula na pakua chakula chako kikiwa cha moto


    Fahamu pia jinsi ya kupika:


    -TAMBI ZA SAUSAGE NA KAROTI

    -JINSI YA KUPIKA SAMBUSA ZA NYAMA






    Jinsi ya kupika Biryani ya mbogamboga


    Mahitaji ya Biryani ya mbogamboga:


  • ½ kg mchele wa basmati


  • Kitunguu maji kikubwa 1


  • Nyanya 1 kubwa


  • Karoti 1 kubwa


  • Njegere robo kikombe


  • Kiazi ulaya 1 kikubwa


  • Tangawizi za kusaga kijiko 1


  • Kitunguu swaumu cha kusaga kijiko 1


  • Karafuu kijiko 1


  • Majani ya kotimili fungu 1


  • Maziwa ya mtingi ¼ kikombe


  • Chumvi na pilipili kiasi


  • Unga wa dhani kijiko 1 cha mezani


  • Juisi ya limao kijiko 1 cha mezani


  • Mafua ¼ lita


  • Maandalizi ya Biryani ya mbogamboga:

  • Chemsha mchele na kisha weka pembeni


  • Osha mbogamboga zote isipokuwa vitunguu na nyanya


  • Changanya mtindi na tangawizi pamoja na kitunguu swaumu viache vikae kwa muda wa saa moja


  • Chukua sufuria weka mafuta na kisha kaanga vitunguu maji, weka nyanya, chumvi, kotimili na limao halafu weka karafuu na kanga hadi vichanganyike vizuri


  • Miminia mchanganyiko wa mtindi na baadaye weka pilipili na baadaye weka unga wa dhania


  • Chukua mchele uliochemshwa changanya na mchanganyiko huo


  • Palia moto juu ya chakula chako na acha kwa muda wa dakika 30


  • Baada ya hapo chakula chako cha biriani kitakuwa tayari kwa kuliwa


  • Jinsi ya kupika Biryani ya nyama ya kuku

    Mahitaji ya kupika Biryani ya nyama ya kuku


  • Vikombe 2 mchele wa basmati


  • ½ kijiko cha chai mbegu za jira (cumin seeds)


  • Star anise 1


  • ¾ kijiko cha chai chumvi


  • Kilo 1 nyama ya kuku


  • Kijiko 1 cha chakula tangawizi


  • Kijiko 1 cha chakula kitunguu saumu


  • Kijiko 1 cha chakula chicken bouillon powder


  • ½ limao


  • ¼ kikombe mafuta ya mzaituni (olive oil)


  • Vijiko 2 vya chai tangawizi


  • Vijiko 2 vya chai kitunguu saumu


  • Kitunguu maji 1 kikubwa Vijiko 3 vya chakula mafuta ya samli/ mafuta ya kupikia


  • Pilipili kichaa 2


  • Nyanya 3 kubwa


  • ½ kilo viazi ulaya


  • ½ kikombe mtindi


  • ½ kijiko cha chai pilipili ya kukausha (chili pepper flakes)


  • Vijiko 2 vya chai garam masala


  • Kipande cha mdalasini


  • Bay leaf 2


  • Punje 4 karafuu


  • Punje 4 iliki


  • ½ kijiko cha chai mbegu za jira


  • Kijiko 1 cha chai unga wa giligilani


  • Kijiko 1 cha chai binzari ya manjano


  • Chumvi kwa kuonja.


  • Maandalizi ya Biryani ya kuku


    Kumarinate nyama yako ya kuku


  • Toa ngozi na kuchanja nyama; Andaa viungo vya kuku; twanga kitunguu saumu na tangawizi; kamua maji ya limao


  • Kwenye bakuli kubwa, changanya vizuri kuku na viungo vyote vya kuku


  • Funika bakuli au weka nyama kwenye mfuko. Acha viungo vikolee kwa masaa 4 au inapendeza zaidi akikaa usiku kucha


  • Ukiwa tayari kupika, andaa mchele kwa kuuosha hadi maji yawe masafi kabisa. Loweka kwenye maji kwa muda wa dakika 30


  • Ukiloana, chuja maji weka pembeni


  • Andaa viungo vya sosi/ gravy; katakata pilipili vipande vidogovidogo vya mraba; katakata viazi ukubwa utakaopenda; twanga kitunguu saumu na tangawizi, weka pembeni


  • Weka nyanya na kitunguu maji kwa ajili ya sosi kwenye mashine ya kusagia chakula kutengeneza rojo, weka pembeni


  • Andaa viungo kwa ajili ya juu/ garnish; Katakata kitunguu maji vipande virefu; katakata na majani ya giligilani na majani ya mnanaa, weka pembeni


  • Loweka zafarani chache kwenye ¼ kikombe cha maji ya uvuguvugu. Weka pembeni


  • maandalizi ya nyama ya kuku


  • Washa oven katika joto la 150 degrees C. Kwenye sufuria katika moto wa juu kiasi, chemsha vikombe 4 vya maji. Ongeza mchele, mbegu za jira, star anise na chumvi. Pika mpaka wali ukaribie kuiva


  • Ipua, chuja maji. Weka pembeni


  • Kwenye kikaangio katika moto wa wastani kaanga kitunguu kwa ajili ya kuweka juu (garnish) mpaka kiwe na rangi ya kahawia ila kisiungue


  • Toa kitunguu kwenye mafuta, hamishia vitunguu kwenye sahani iliyotandazwa tissues za jikoni au chujio la bati ili mafuta yachuje. Weka pembeni kwa ajili ya kuweka juu ya biryani badae


  • Ukitoa kitunguu, weka viazi kwenye mafuta. Kaanga mpaka viive vizuri, ipua weka pembeni


  • Kwenye sufuria katika moto wa chini kiasi, weka mafuta ya kupikia au samli. Yakichemka ongeza kitunguu saumu, tangawizi na pilipili kichaa. Pika paka viive na harufu ya ubichi iishe, kama dakika 2


  • Ongeza kuku na viungo vizimavizima; mdalasini, mbegu za jira, karafuu na iliki. Kaanga kwa dakika 5, ukigeuza mara chache isishike chine


  • Ongeza rojo ya nyanya, majani la bay na viungo vikavu vilivyoandaliwa kwa ajili ya sosi; giligilani ya unga, pilipili ya kukausha, manjano na garam masala. Acha ipike mpaka nyanya ziive vizuri


  • Ongeza mtindi, koroga vizuri, ongeza na chumvi ikibidi


  • Funika sufuria, acha nyama iive taratibu kwenye moto wa chini kwa dakika kama 10, ukigeuza inapobidi; au mpaka sosi iwe nzito, ibakie kama kikombe 1 cha kuivisha wali


  • kupangilia biryani


  • Ongeza viazi changanya vizuri na sosi. Katika chombo cha kuokea au sufuria nyingine kubwa zaidi sambaza nyama chini ya sufuria


  • Sambaza wali juu ya nyama. Ongeza na majani ya giligilani, majani ya mnanaa yaliyakatwakatwa kwa ajili ya kuweka juu pamoja na kitunguu cha kukaanga. Nyunyizia kwa juu maji yenye zafarani


  • Funika na foil, acha wali uive kwenye oven iliyopata moto kwa dakika 20 hadi 30; au mpaka wali uive vizuri. (unaweza pia kupalilia kwa mkaa, au kuoka kwenye oven katika chombo chenye mfuniko)


  • Changanya vizuri


  • Tenga cha moto na kachumbari ya tango, nyanya na mtindi; au ya tango na mtindi










  • About the Author

    Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link
    Cookie Consent
    We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
    Oops!
    It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
    AdBlock Detected!
    We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
    The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
    Site is Blocked
    Sorry! This site is not available in your country.