Notification texts go here Contact Us Buy Now!

Noti Bandia | Sehemu ya 03

Nyamuswa kama ilivyo kwa miji mingine midogo, iliyoko Bunda, mkoani Mara, ulikuwa umechangamka kwa kiasi, wananchi kutoka sehemu mbalimbali zinazouzunguja mji huu walipishana huku na huku wakifanya mahitaji. Ilikuwa Jumapili ya mwisho wa mwezi. Siku ambayo kila inapowadia wenyewe huiita SIKU YA MTERA NYAMUSWA.
SEHEMU YA TATU

Na Nyakasagani Masenza

Nyamuswa kama ilivyo kwa miji mingine midogo, iliyoko Bunda, mkoani Mara, ulikuwa umechangamka kwa kiasi, wananchi kutoka sehemu mbalimbali zinazouzunguja mji huu walipishana huku na huku wakifanya mahitaji. Ilikuwa Jumapili ya mwisho wa mwezi. Siku ambayo kila inapowadia wenyewe huiita SIKU YA MTERA NYAMUSWA.

Nilikuwa nimewasili kijijini hapa dakika chache zilizopita, lakini barabara iendayo nyumbani kwa wazazi wangu ilikuwa imefungwa na wafanyabiashara waliokuwa wakiuza bidhaa mbalimbali. Kama ilivyo kawaida yangu, niliutwaa mkoba wangu nikaunjika begani, kisha nikamruhusu dereva aliyenileta aondoke, kwani hakukuwa na njia ya kupita.

Haikupita sekunde mkoba wangu ulipokelewa na Taabu dadangu kipenzi, sikumuona jinsi alivyotokea, alionekana mwenye furaha kupita kiasi, labda alifutahi kuniona tena baada ya kuwa mbali nae kwa muda.

"Pole na safari", alisema Taabu.

"Mungu amesaidia, habari ya nyumbani?" nilimuuliza wakati tunapita kwenye kundi la watu kuelekea nyumbani.

"Mama pia nilimuona". alisema akaangaza macho kumtafuta.

"Mwache, mwache asafishe macho. Atanikuta nyumbani". nilisema huku tukitembea na baadhi ya watu wakitusindikiza kwa macho.

Dakika kadhaa mama naye alifika, hakufanya ajizi moja kwa moja alikuja na kunikumbatia. "Pole na safari mwanangu", Akaanza kulia, "Ulizoea kutukuta na baba yako, sasa hayupo tena", alisema mama huku machozi yakianza kumtoka. "Ametuachia ukiwa", alilala.

Machozi ya mama yalinifanya niwe kimya kwa sekunde kadhaa nikitafakari hili na lile, "Nyamaza mama, kilichotokea ni kazi ya Mungu, baba yatu ametutangulia tu, siku moja tutamuona. Siku zote baba alikuwa akisema hatapenda tumtangulie sisi, alitaka atangulie yeye, kwa kuwa siku yake ilifika, mapenzi ya Mungu yalitimizwa, alihitajika kutoka miongoni mwetu", nilisema huku nikimuacha mama na kuliendea kaburi la baba kwa ajili yakufanya maombi mafupi.

Baada ya kumuombea mama, tulianza kuzungumza habari nyingine, mama alitaka kujua habari ya safari zangu nje ya nchi, nilimweleza kifupi kuhusu mafanikio ya safari hizo kwa nchi yetu na jinsi Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alivyonizawadia tuzo maalum nilipokuwa katika kazi ya ulinzi wa amani. Alionyesha kufurahishwa sana na maelezo yangu, japokuwa hakujua nini heshima ya tuzo hiyo.

Kwa vile nilikuwa nimetoa taarifa mapema niko njiani, mama na dada waliniandalia chakula nikipendacho, ugali na samaki aina ya ningu na nembe. Nimetokea kupenda aina hii ya samaki, ambao hupatikana sana Ziwa Victoria.

Ilipofika saa tisa mchana, nilipita mitaa kadhaa nikiangalia mji, nilivutiwa na maendeleo yaliyokuwa yakifanywa na baadhi ya vijana. Watu walikuwa wengi, na sehemu za starehe kama baa na hoteli zilikuwa zimejaa watu huku wengine wakicheza pool, karata na bao la solo. Nililazimika kumtembelea shemeji yangu mpendwa Mama Feka, ambaye kwa muda mrefu alikuwa na shauku ya kuniona.

"Ah, karibu sana molamu", alisema Mama Feka akinikumbatia.

"Nafasi ya upendeleo molamu, nina muda mchache sana wa kuwa hapa Nyamuswa, nimehofia jambo moja, nimeogopa usijesikia nilikuwepo na sikukutafuta, sidhani kama ungenielewa?", nilimuuliza.

"Nisingekuelewa kabisa, habari ya Dar... Nadhani umeingia leo".

"Yes, nimeingia leo na ratiba yangu imebana mno, lakini nitajitahidi kuwepo hapa kwa siku mbili tatu hivi", nilimwambia.

"Naamini utakuwa umekula, twende maduka saba nikupe japo bia mbili molamu", alisema. Kabla sijasema kitu haraka aliingia ndani. Hakuchukua hata dakika moja akatoka ameshika kitenge mkononi. "Haya togende molamu", akatangulia, nikamfuata, tukaelekea hapo maduka saba.

Sehemu hii ilikuwa imechangamka kiasi, vijana ninaowafahamu na nisiowafahamu walikuwa hapa wakiangusha moja moto moja baridi, nilipungiana mikono na vijana hao waliokuwa wakibisha kuhusu mchezo wa mpira, Ligi Kuu ya Tanzania Bara, kati ya Yanga na Simba. Mmoja wa vijana hawa alionekana mwenye jazba sana. "Mwamuzi alichangia kuharibu radha ya mchezo, huwezi kutoa kadi nyekundu dakika za mwanzo kama vile", alisema kijana huyo kwa ghadhabu.

"Ulitaka aachwe aendelee kufanya makosa uwanjani?", alihoji kijana mwingine ambaye pia alisimama kuonyesha msisitizo.

"Molamu, huwezi kuamini baada ya mchezo wa Yanga na Simba, ngumi zilipigwa hapa, wengine wakilalamikia kadi nyekundu iliyotolewa na mwamuzi, wengine walidai eti mwamuzi alikuwa sahihi kutoa kadi hiyo, yaani ni vurugu tupu", alisema Mama Feka nikimwangalia kwa makini.

"Molamu, wewe ni shabiki wa timu gani?", nilimuuliza.

"Aaah molamu... Mabingwa watetezi Yanga Afrika, nikuletee kadi yangu ya uanachama, usije kusema mimi ni shabiki kishoka".

"Umesema, nimekuelewa molamu", nikasimamam kuelekea mahali vijana hao walikuwa wakibishana bila mpangilio.

"Mimi nilijua kabisa kuwa mwanamke hawezi kuchezesha mchezo kama ule", alirukia kijana mwingine.

"Sikilizeni", niliwahadhalisha.

"Tumsikilize mzee, naamini alikuwa uwanjani, sisi tunabishana kwa kuona mchezo katika luninga", alisema Adul Light, mmoja wa vijana hao.

"Kwani luninga ina tofauti gani na kuwa uwanjani, si kila kitu kinaonyeshwa laivu", alidakia kijana mwingine.

"Ndio maana nikaomba mnisikilize... Lazima mtambue kuwa mchezo wa soka unaendeshwa kwa kanuni na sheria za mchezo, mnaweza kumlaumu mwamuzi wa mchezo huo kuwa alimtoa mchezaji wa Simba kwa kadi nyekundu, lakini ukweli ni kwamba mwamuzi hakutoa kadi nyekundu..."

"Unaona sasa. Inaonekana hukufika hata uwanjani, maana hujui kama mwamuzi alitoa kadi nyekundu, eti jamani mwamuzi hakutoa kadi nyekundu?" alihoji kijana huyo akionyesha kuwa na jazba.

"Ungenisikiliza kwanza", nilimsihi kijana huyo." akakubaliana nami. Haraka nikamuomba mtoa huduma awapatie vinywaji. "Kama nilivyotangulia kusema, mchezo wa soka unaendeshwa kwa kanuni na taratibu. Dakika chache baada ya mchezo huo kuanza, mwamuzi alitoa kadi ya njano, kimsingi mchezaji alipaswa kujihami, asifanye makosa. Lakini kabla hata dakika kumi hazijapita akafanya kosa lililostahili kadi ya njano, akapewa yelow card ya pili. Kanuni za soka zinasema, mchezaji akizawadiwa kadi mbili za njano, atapewa kadi nyekundu ili aende nje. Ndiyo maana nikasema hakupewa kadi nyekundu, ila kadi mbili za njano zilimfanya mwamuzi kutoa kadi nyekundu. Si matakwa yake, ni kanuni za mchezo", nilifafanua.

Vinywaji vikaletwa tukaanza kunywa,

"Hali hii iliwahi kuwakuta hata Yanga, wachezaji wake wawili walitolewa uwanjani kwa nyekundu, na hii si kwa Yanga na Simba tu, tumeshudia hata ligi za Ulaya", anabaisha Abdul.

"Yes, kadi nyekundu ni sehemu ya mchezo, ndiyo maana mwamuzi anakuwa nazo mfukoni. Lakini pia yafaa mfahamu kuwa mwamuzi anapowajibika pale uwanjani, kuna mamlaka zingine juu yake, kama atakuwa amekwenda kinyume na kanuni anaadhibiwa", niliwadokeza, wakaonekana kunielewa.

Mara ujumbe mfupi ukaingia kwenye simu yangu, Ujumbe ulisema. "UMEZUKA MOTO NA KUUNGUZA JENGO LA OFISI ZETU ZILIZOKO MTAA WA AZIKIWE, VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA HUSUSAN KIKOSI CHA ZIMA MOTO NA UOKOAJI KINAENDELEA NA KAZI YA KUZIMA MOTO HUO, UNATAKIWA KUREJEA HARAKA KWA AJILI YA TAtHIMINI", Col. Ben. Kwanza nilicheka, mapigo ya moyo wangu yakaongezeka.

"Molamu, nimepata ujumbe wa kushtua kidogo, natakiwa kurejea haraka Dar, es Salaam, hivi tunavyozungumza, moto umezuka ghafla unateketeza jengo la ofisi zetu mtaa wa Azikiwe, kwa hiyo nalazimika kuondoka sasa hivi", nilisema wote wakaonekana kushangazwa.

Aaah molamu, sina bahati na wewe, jitahidi kuvumilia uondoke kesho mapema".

"Muda huu utapata usafiri gani kaka?" alihoji Abdul Light.

"Kama nitaweza kufika Mwanza mapema, saa tatu usiku kuna ndege, bahati nzuri rubani wa ndege hii ni mtu wangu wa karibu, nitamjurisha aniwekee nafasi, nilipenda kuwa nanyi, lakini hali ndiyo kama mlivyoona", nikasimama na kuwaaga kwa mara nyingine nikaondoka.

ITAENDELEA

About the Author

Hello,I am Web Designer and Expert facebooktwitteryoutubeinstagramexternal-link

إرسال تعليق

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.