Notification texts go here Contact Us Buy Now!

Muongozo wa walimu wa Kujitolea

Serikali ya Tanzania yatoa Muongozo na Mikataba ya walimu wa kujitolea
Muongoza wa walimu wa kujitolea


Mwongozo wa Walimu wa Kujitolea umeandaliwa ili kutoa maelekezo ya namna ya kupata walimu wenye sifa stahiki na kuwaajiri kwa mkataba wa kujitolea, kutoa taratibu za mafunzo kabilishi, kupanga na kutoa maelekezo ya kutosha kitaaluma na kitaalamu ili kazi zifanyike kwa ufanisi. Aidha, Mwongozo huu unalenga kutoa maelekezo ya upatikanaji wa walimu wanaojitolea na huduma zao ikiwemo: posho, motisha na usimamizi wa nidhamu pahala pa kazi kwa kuzingatia masharti ya ajira za mkataba 
Inatarajiwa kuwa matumizi ya Mwongozo huu yataimarisha ushirikiano wa wadau wa elimu hususani Uongozi wa Elimu, jamii, walimu na wazazi. Pia Mwongozo utawezesha walimu wanaojitolea kutoa huduma stahiki za ujifunzaji na ufundishaji kwa kuzingatia matakwa ya elimu nchini. Hii itasaidia kutatua changamoto za ujifunzaji na ufundishaji na kuleta matokeo chanya yaliyokusudiwa katika elimu ya awali, elimu ya msingi, elimu ya sekondari na vyuo vya maendeleo ya wananchi Tanzania.

Chapisha Maoni

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.