BAJIA ZA SAMAKI 🐟😋
MAHITAJI YA KUPIKA BAJIA ZA SAMAKI:
- Samaki wa mnofu vipande 2, vikubwa
- Pilipili manga kijiko cha chai
- Maji ya ndimu kiasi
- Baking powder vijiko 2 vya chai
- Unga wa ngano kikombe 1
- Chumvi kiasi chako.
- Kitunguu saumu kilichopondwa 1/2 kijiko cha chai
- Sukari 1/2 kijiko cha chai
- Kitunguu maji 1 kilichokatwa katwa Majani ya kotmir yalokatwa katwa vijiko 2 vya chakula
- Hoho zilizokatwa katwa kijiko 1 cha chakula
- Yai 1
- Maziwa ama maji 1/2 kikombe, utatia kdogo kidogo si lazima yatumike yote
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA BAJIA ZA SAMAKI:
1. Safisha samaki wako vizuri kisha mchemshe kidogo kwa chumvi, ndimu na pilipili manga.
2. Mnyambue samaki wako kupata chenga chenga unaweza mnyambua kwa mikono, blender au food processor.
3. Changanya unga, baking powder
katika bakuli, ukishachanganya vizuri tia mahitaji yalobaki isipokuwa maji/maziwa kisha changanya tena vizuri
4. Anza kutia maji ama maziwa taratibu ukiwa wachanganya hadi kupata uzito mzuri wa kuchoteka kwa kijiko au mkono usiwe maji maji sana.
5. Tia mafuta jikoni juu ya moto wa kiasi, yakipata moto chota mchanganyiko wako anza kuchoma.