Nimempa kashindwa mwenyewe
..... Ep3
...... Kuhusu kaka yako Jalala.. songa nayoo .... Mimi nimetoka zangu saloon pale kwa Recho lakin story nilizozikuta ndizo zilizo nileta hapa maana nimejiskia uchungu sana
...... Zipi hizo dada Amina hebunieleze mbona unazunguka sana..
Amina akameza mate na kufikiria kidogo kisha akasema.... "Mwenzangu yaani tangu nimefika pale saloon, nimeseti, nimekaa kwenye draya story ilikuwa moja tuu ya kumkasfu kaka yako... kuwa jogoo lake halipandi mtungi, hivi ni kweli? ... "Hayo maneno wala cyo mageni hapa mtaani unajua waswahili wanapenda uwe Malaya ili ukipata ukimwi wakucheke, lakini kama umeamua kujitunza ndio utazushiwa mambo kama hayo hao walio kwamba hawana lolote wanamtaka tu kaka yangu na yeye hana mpango nao, kaka yangu cyo zoazoa kama wao walivyozoea leo wapo na mwanaume huyu kesho wapo na yule"alisema Mwajuma kwa upole.. "Mwenzangu basi habari ndio hiyo yani mpaka nikajuta kwanini Nimependa saloon ile maana wamejazana kibao hawana cha kuongea kazi kuchunguza mambo ya watu ila nikaona si vyema nikuchunie shoga bora nikuelezee ili ujue kinacho endelea......
...... " Asante dada ila kama nilivyo kueleza hatamimi huwa nausikia sana umbea huo ila huwa sina time nao"........ Story hiyo ilimuwwka katika wakati mgumu san Mwajuma baada ya Amina kuondoka, mwanzoni ilikuwa kama habari ndogo ya mzaha lakini sasa alihic inaelekea kuwa kashfa kubwa dhidi ya kaka yake.. alipanga amuulize ila alishindwa kufanya hivyo kwa kuchelea kuwa huenda ni kweli kaka yake ni hanithhivyo kumuarhiri zaidi kisaikolojia... Hata. hivyo baada ya wiki mbili lilitokea swala ambalo llilimuuma sana Mwajuma ingawa alijitahidi kuficha.. Bwa Akramu alitembelewa na Dada zake binamu kutoka kwao Mtwara, mmoja alikuwa akiitwa Asnati na mama Rau na mwingime mdogo mwenye umri kama wa miaka (20) alieitwa Amina ambaye alikuwa na mtoto mmoja wa miaka mitatu(3).. Dada zake hawa walikuwa wacheshi sana na walikuwa wakipenda kutaniana sana na Jalala, wakati mingine walicheza michezo mingine ambayo hata kaka yao angekuwwpo asingekubali utani kama huo uendelee........
....... Sikumoja Jalala akiwa ameshaeudi kutoka kazini Asnati na Amina kama kawaida walimuaga wifi yap, wakaenda kwenye chumba cha Jalala huku Asnati akisema... "Leo kaka yako nampelekea mdogo wangu alale nae maana tangu nine sijamiona akiingia mwanamke asije akazidiwa na chunusi bure wakati mademu tupo" lngawa kwao ulikuwa kama utani wa kawaida lakini Mwajuma kiroho kilimlipuka., kwa alivyo kuwa akiwajua mawifi zake walivyo machakaramu wanaweza kufanya jambo kama hilo kilicho mtisha zaidi cyo hilo la Asnati kutaka kumpa dem kaka yake ila alifikiri kama atafanya hivyo kweli na kaka yake akashindwa kumkabili kutokana na hali inayo zungumziwa mitaani kuwa nayo Itakuwa ni aibu iliyoje hakuwa na lakufanya kwani mawifi zake wakishaamuaga jambolao huwa hawabadili aliwaacha na kuwatazama kwa macho hadi walipopotelea kwenye nyumba aliyokuwa akiishi kaka yake ambayo ilikuwa upande wa pili wa mtaa ikitazamana na nyumba ya........ "Ehee leo nimekuja rasmi kukukabidhi mdogo wangu kwanzia leo atalala kwako na kwanzia kesho ataanza kupika na kupakua... ❤❤
Je, Amina tafanikiwa.. tukutane Ep4
..... Yajayo yanafurahisha....