Muda mwingine inatakiwa tukubaliane na ukweli kwamba hata uwe sahihi kivipi, yule mtu uliemuamini anaweza akakusaliti.
Lazima tukubaliane na ukweli kwamba hata kama ulikua mwanamke bora kwake, umemfanyia mengi, umempa mwili wako, umezaa nae, umekuwa ukimpikia chakula kizuri, umekua ukipendeza na kumpa mapenzi yote, bado anaweza akakuumiza akakutenda na kakusaliti!
Namaanisha kuna muda lazima uwe na ujasiri kiasi cha kujitizama kwenye kioo na kukubaliana na ukweli kwamba usaliti upo licha ya kumfanyia mtu mazuri mengi.
Sometimes lazima ukubaliane na ukweli kwamba usaliti hauepukiki katika maisha.
Hivyo inavyotokea umesalitiwa, usipoteze muda kujilaumu na kutafuta ni nini ulifanya kustahili usaliti baada ya kumfanyia mengi mazuri.
Hivyo, unaposalitiwa, usipoteze muda kujilaumu na kutafakari ulimkosea nini. Acha wasaliti wawe wasaliti, acha traitors wawe traitors, acha waongo wawe waongo. Kila mtu huvuna kile alichopanda.
Wewe kuwa kama Yesu Kristo, utasalitiwa leo, kesho kutwa utasahau na kuwa na furaha tena wakati aliyekusaliti atataabika kama vile Yuda alivyotaabika!!!